• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Ofisi |
    • Malalamiko |
Dodoma Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Taasisi
      • Huduma Zetu
    • Huduma Zetu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Seksheni
      • Administration and Human Resource Management Section
      • Planning and Coordination
      • Infrastructure section
      • Management Monitoring and Inspection section;
      • Education and vocational Training section
      • Economic and productive sectors section;
      • Health, Social welfare and Nutrition services section
      • Industry, Trade and Investment section
    • Vitengo
      • Information Communication Technology (lcT) and Statistics
      • Government Communication Unit
      • Finance and Accounts unit;
      • Internal Audit unit
      • Legal services unit;
      • Procurement Management unit;
  • Wilaya
    • Bahi
    • Chamwino
    • Kongwa
    • Mpwapwa
    • Kondoa
    • Dodoma Mjini
    • Chemba
  • Mamlaka za Serikali za mitaa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bahi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chemba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa
    • Halmashauri ya Wilaya Mpwapwa
    • Halmashauri ya Mji Kondoa
    • The City Council of Dodoma (CCD)
  • Uwekezaji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Habari kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WAZIRI JAFO ATOA MAAGIZO MAZITO KWA MARAS, MADED NA MAAFISA MAWASILIANO WA SERIKALI

Imetumwa : March 17th, 2018

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mhe. Selemani Jafo ametoa agizo kwa Ofisi za Mikoa na Halmashauri zote nchini kutenga fedha kwa ajili ya ununuzi wa vifaa kwa vitengo vya Mawasiliano ili viweze kutekeleza majukumu yake.

Mhe. Jafo ametoa agizo hilo Jijini Arusha alipokuwa akifunga Kikao Kazi cha 14 cha Maafisa Mawasiliano Serikalini uliohudhuriwa na Maafisa Mawasiliano 300 kutoka katika Taasisi, Idara na Wakala wa Serikali, Mikoa, Majiji, Miji na Halmashauri zote nchini.


“Kuanzia mwaka ujao wa bajeti Makatibu Tawala wa Mikoa na Wakurugenzi wa Halmashauri, Majiji, Manispaa na Miji waweke kipaumbele kwa kutenga fedha za kununua vifaa muhimu kwa ajili ya Maafisa Habari na Mawasiliano ili waweze kutekeleza majukumu yao ipasavyo,” alisema Mhe. Jafo.

Vile vile ameagiza Maafisa Habari wapewe ushirikiano wa kutosha na Wakuu wa Idara kwa kuwapa taarifa na takwimu za idara zao ili kuwawezesha Maafisa hao kutoa taarifa muhimu za Serikali kwa vyombo vya habari na wananchi kwa wakati na bila vikwazo.

Aidha, amewataka Viongozi wa Mamlaka ya Serikali za Mitaa kutambuua kuwa Afisa Habari ndiye Mtendaji Mkuu katika masuala ya uandaaji wa habari, hivyo ni muhimu Maafisa hao kuingia katika vikao mbalimbali ili wapate uelewa wa masuala mbalimbali ya kimaamuzi yanayofanywa na uongozi.


Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo, Susan Mlawi amesema mada mbalimbali zimetolewa kwa lengo la kuwajengea uwezo Maafisa hao, ambapo miongoni mwa mada hizo ni pamoja na umuhimu wa Mawasiliano ya kimkakati katika kuisemea Serikali na tathmini ya utendaji katika mwaka 2017, maadili ya usalama katika kazi ya kuitangaza na kuisemea Serikali pamoja na wajibu wa Maafisa Habari katika mkakati wa kitaifa wa kupambana na maafa.

Nae, Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Gambo amesema ofisi yake itashirikiana na Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo kuhakikisha maazimio yote yaliyoafikiwa katika mkutano huo yanatekelezwa katika vitengo vyote vya Mawasiliano vya Halmashauri zote za Mkoa wa Arusha.

Mkutano wa Maafisa Mawasiliano Serikalini unafanyika kila mwaka, ambapo kwa mwaka huu unafanyika kwa mara ya 14. Mkutano huo umeandaliwa na Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo kwa kushirikiana na Chama cha Maafisa Mawasiliano
 

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE (CSEE) 2020 January 15, 2021
  • MATOKEO YA MTIHANI WA MAARIFA (QT) 2020 January 15, 2021
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021 SHULE ZA BWENI (WASICHANA NA WANAUME) . December 20, 2020
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA YA KIDATO CHA PILI (FTNA) 2020 January 15, 2021
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • KATIBU TAWALA SINGIDA AKABIDHI OFISI KWA KATIBU TAWALA DODOMA

    March 23, 2023
  • MACHINGA DODOMA WAMPONGEZA DKT. SAMIA SULUHU HASSAN

    March 23, 2023
  • KIWANDA CHA AINA YAKE KUJENGWA KONGWA

    March 17, 2023
  • WAFANYAKAZI WAASWA MSHIKAMANO MAHALA PA KAZI

    March 15, 2023
  • Tazama Zote

Video

Mkuu wa Mkoa akiongoza siku ya maombi jijini Dodoma
Video Nyinginezo

Kurasa za Karibu

  • Speeches
  • mission and vision
  • Photo Gallery
  • Videos
  • Press Releases
  • Organization Structure
  • Reports
  • Client Service Charter
  • Acts

Tovuti Muhimu

  • PO-RALG
  • Public Service Management
  • Parliament of Tanzania
  • UDOM
  • Government Portal
  • Prime Minister's Office Website

World Visitors Tracker

world map hits counter

Rejesta ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Jengo la Mkapa (Mkapa House) Barabara ya Hospitali ya Mkoa

    Anuani ya Posta: 914 DODOMA

    Simu: +255 26 232 4343/232

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@dodoma.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya eneo

Hakimiliki©2016 GWF . Haki zote zimehifadhiwa.