• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Ofisi |
    • Malalamiko |
    • eoffice |
Dodoma Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Taasisi
      • Huduma Zetu
    • Huduma Zetu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Seksheni
      • Administration and Human Resource Management Section
      • Planning and Coordination
      • Infrastructure section
      • Management Monitoring and Inspection section;
      • Education and vocational Training section
      • Economic and productive sectors section;
      • Health, Social welfare and Nutrition services section
      • Industry, Trade and Investment section
    • Vitengo
      • Information Communication Technology (lcT) and Statistics
      • Government Communication Unit
      • Finance and Accounts unit;
      • Internal Audit unit
      • Legal services unit;
      • Procurement Management unit;
  • Wilaya
    • Bahi
    • Chamwino
    • Kongwa
    • Mpwapwa
    • Kondoa
    • Dodoma Mjini
    • Chemba
  • Mamlaka za Serikali za mitaa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bahi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chemba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa
    • Halmashauri ya Wilaya Mpwapwa
    • Halmashauri ya Mji Kondoa
    • The City Council of Dodoma (CCD)
  • Uwekezaji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Habari kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

DKT.MPANGO,MGENI RASMI MAOMBI YA KULIOMBEA TAIFA JIJINI DODOMA

Imetumwa : April 21st, 2024

Mkuu wa MKoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule, leo Aprili 21, 2024, amefanya mkutano na waandishi wa habari kuutangazia umma juu ya dhamana iliyopewa Mkoa wa Dodoma kuandaa na kufanya maombi na dua ya kuliombea Taifa katika kipindi hiki cha kuelekea Maadhimisho ya miaka 60 ya Muungano wa Tanzania.

Mkutano huo uliofanyika kwenye uwanja wa Jamhuri Jijini Dodoma ambao ndipo hafla hiyo itafanyikia mnamo Aprili 22, 2024, Mkuu wa MKoa ametoa hamasa kwa waumini wa Madhehebu ya dini zote na wananchi wote wa Dodoma kufika kwenye uwanja huo kuungana na viongozi wa dini mbalimbali watakaoshiriki maombi hayo.

“Heshima tuliyopewa ni kubwa na inapaswa kuthaminiwa na wanadodoma na tunatakiwa kuonesha thamani hii kwa kujitokeza kwa wingi, tujae uwanjani hapa ili kufanya maombi ya kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa Muungano kuendelea kuimarika lakini pia kuuombea Muungano wetu uendelee kuwa wa mfano.

Mkuu wa Mkoa ameongeza kuwa maombi haya ni kwa ajili ya kuombea tudumu katika umoja, amani na utulivu kama ilivyo historia yetu kutoka kwa waasisi wa Muungano huo. Aidha, wanadodoma wanaotarajiwa kushiriki maombi hayo wanafikia 30,000 hivyo, shime imetolewa kwa wananchi wote kufika na kushiriki pamoja.

“Tuhamasishane sote kufika hapa kwani maombi huleta Baraka. Tujitokeze kwa wingi ili tuendelee kuifaharisha Dodoma kwa matendo haya makubwa. Karibuni pia mikoa ya jirani tufanye maombi kwa ajili ya Taifa letu” Amesisitiza Mhe. Senyamule.

Mgeni rasmi kwenye hafla hiyo anatarajiwa kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango. Tukio hilo litaanza saa 1:00 asubuhi kwa wananchi kuanza kuingia viwanjani hapo. 


Matangazo

  • "WANANCHI JITOKEZENI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU 2025" - RC SENYAMULE February 17, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MADEREVA WA SERIKALI WATAKIWA KUZINGATIA SHERIA ZA USALAMA BARABARANI

    May 17, 2025
  • WATANZANIA WATAKIWA KUILINDA NA KUIDUMISHA AMANI NI KURUHUSU MAENDELEO NCHINI

    May 15, 2025
  • MKURUGENZI WA ‘WATER FOR PEOPLE ‘ AMTEMBELEA RAS MMUYA

    May 16, 2025
  • WANAFUNZI KIDATO CHA SITA WAASWA SAFARI YA ELIMU BADO NI NDEFU

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

RC SENYAMULE AKIZUNGUMZA KWENYE UZINDUZI WA SERA YA ELIMU NA MAFUNZO YA MWAKA 2014 TOLEO LA 2023.
Video Nyinginezo

Kurasa za Karibu

  • Speeches
  • mission and vision
  • Photo Gallery
  • Videos
  • Press Releases
  • Organization Structure
  • Reports
  • Client Service Charter
  • Acts

Tovuti Muhimu

  • PO-RALG
  • Public Service Management
  • Parliament of Tanzania
  • UDOM
  • Government Portal
  • Prime Minister's Office Website

World Visitors Tracker

world map hits counter

Rejesta ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Jengo la Mkapa (Mkapa House) Barabara ya Hospitali ya Mkoa

    Anuani ya Posta: 914 DODOMA

    Simu: +255 26 232 4343/232

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@dodoma.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya eneo

Hakimiliki©2016 GWF . Haki zote zimehifadhiwa.