• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Ofisi |
    • Malalamiko |
    • eoffice |
Dodoma Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Taasisi
      • Huduma Zetu
    • Huduma Zetu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Seksheni
      • Administration and Human Resource Management Section
      • Planning and Coordination
      • Infrastructure section
      • Management Monitoring and Inspection section;
      • Education and vocational Training section
      • Economic and productive sectors section;
      • Health, Social welfare and Nutrition services section
      • Industry, Trade and Investment section
    • Vitengo
      • Information Communication Technology (lcT) and Statistics
      • Government Communication Unit
      • Finance and Accounts unit;
      • Internal Audit unit
      • Legal services unit;
      • Procurement Management unit;
  • Wilaya
    • Bahi
    • Chamwino
    • Kongwa
    • Mpwapwa
    • Kondoa
    • Dodoma Mjini
    • Chemba
  • Mamlaka za Serikali za mitaa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bahi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chemba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa
    • Halmashauri ya Wilaya Mpwapwa
    • Halmashauri ya Mji Kondoa
    • The City Council of Dodoma (CCD)
  • Uwekezaji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Habari kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

“DODOMA TUMEJIANDAA KUWAHUDUMIA ABIRIA WA SGR “ - RC SENYAMULE

Imetumwa : November 1st, 2024



Na. Hellen M. Minja,        

       Habari – DODOMA RS

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary S. Senyamule, leo Novemba Mosi, 2024, amewapokea abiria 320 waliosafiri kutoka Dar es Salaam hadi Dodoma kwa mara ya kwanza na treni ya SGR (mchongoko) katika stesheni ya Mkonze, Jijini Dodoma.

Akizungumza mbele ya waandishi wa habari punde baada ya kupokea treni hiyo, Mhe. Senyamule amesema;

“Abiria tuliowapokea leo ni 320, ndio mashuhuda wa kwanza kupanda treni hii inayokamilisha Dodoma kuwa na trip nne za kutoka na kuingia kila siku. Niwakaribishe Wanadodoma, lakini na Mikoa yote jirani inayotumia treni kupitia Dodoma, kwani tuna huduma nyingi na tumejiandaa kuwahudumia” Mhe. Senyamule.

Aidha Mkuu wa Mkoa ameongeza kuwa, uchumi wa Dodoma umekua na mabadiliko makubwa tangu kuanza kwa safari za treni za mwendo kasi kwa kuongeza mzunguko wa fedha kwa kiasi kikubwa.

“Sisi Mkoa wa Dodoma, tumeendelea kuona mabadiliko makubwa ya wanachi wakifurahia ongezeko la mapato kwani zaidi ya abiria 900 wanaondoka mara tatu kwa siku, ukiongeza na hawa wa mchongoko ni abiria 3,000 kwa siku. Kila mmoja anakua na hela hivyo katika kukaa kwao hapa wanachangia uchumi wa Dodoma”

Treni hiyo yenye madaraja mawili (Royal na Bussiness), inabeba abiria 583 kwa safari moja, inaongeza idadi ya safari kutoka mbili hadi nne kwa siku huku ikitumia takriban saa tatu kutoka Dar es Salaam hadi Dodoma, na kufanya ratiba za safari kuwa; saa 11:15 Alfajiri, saa 08:10 mchana, saa 11:15 jioni na ya mwisho ni saa 12:40 jioni

Sambamba na mapokezi ya abiria, Mhe. Senyamule, amepata fursa ya kutembelea baadhi ya maeneo ya kutolea huduma yaliyopo ndani ya stesheni hiyo ya kisasa, ikiwa ni pamoja na sehemu ya kupumzikia wageni mashuhuri, eneo la kujiburudisha abiria wakati wakisubiri safari pamoja na mgahawa


#kurayakosautiyako              

#ujanjanikupigakura              

#dodomatukotayarikupigakura

#mtiwangubirthdayyangu

Matangazo

  • "WANANCHI JITOKEZENI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU 2025" - RC SENYAMULE February 17, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MADEREVA WA SERIKALI WATAKIWA KUZINGATIA SHERIA ZA USALAMA BARABARANI

    May 17, 2025
  • WATANZANIA WATAKIWA KUILINDA NA KUIDUMISHA AMANI NI KURUHUSU MAENDELEO NCHINI

    May 15, 2025
  • MKURUGENZI WA ‘WATER FOR PEOPLE ‘ AMTEMBELEA RAS MMUYA

    May 16, 2025
  • WANAFUNZI KIDATO CHA SITA WAASWA SAFARI YA ELIMU BADO NI NDEFU

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

RC SENYAMULE AKIZUNGUMZA KWENYE UZINDUZI WA SERA YA ELIMU NA MAFUNZO YA MWAKA 2014 TOLEO LA 2023.
Video Nyinginezo

Kurasa za Karibu

  • Speeches
  • mission and vision
  • Photo Gallery
  • Videos
  • Press Releases
  • Organization Structure
  • Reports
  • Client Service Charter
  • Acts

Tovuti Muhimu

  • PO-RALG
  • Public Service Management
  • Parliament of Tanzania
  • UDOM
  • Government Portal
  • Prime Minister's Office Website

World Visitors Tracker

world map hits counter

Rejesta ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Jengo la Mkapa (Mkapa House) Barabara ya Hospitali ya Mkoa

    Anuani ya Posta: 914 DODOMA

    Simu: +255 26 232 4343/232

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@dodoma.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya eneo

Hakimiliki©2016 GWF . Haki zote zimehifadhiwa.