• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Ofisi |
    • Malalamiko |
    • eoffice |
Dodoma Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Taasisi
      • Huduma Zetu
    • Huduma Zetu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Seksheni
      • Administration and Human Resource Management Section
      • Planning and Coordination
      • Infrastructure section
      • Management Monitoring and Inspection section;
      • Education and vocational Training section
      • Economic and productive sectors section;
      • Health, Social welfare and Nutrition services section
      • Industry, Trade and Investment section
    • Vitengo
      • Information Communication Technology (lcT) and Statistics
      • Government Communication Unit
      • Finance and Accounts unit;
      • Internal Audit unit
      • Legal services unit;
      • Procurement Management unit;
  • Wilaya
    • Bahi
    • Chamwino
    • Kongwa
    • Mpwapwa
    • Kondoa
    • Dodoma Mjini
    • Chemba
  • Mamlaka za Serikali za mitaa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bahi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chemba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa
    • Halmashauri ya Wilaya Mpwapwa
    • Halmashauri ya Mji Kondoa
    • The City Council of Dodoma (CCD)
  • Uwekezaji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Habari kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MWAMKO WA WANAWAKE KUGOMBEA SERIKALI ZA MITAA WAONEKANA DODOMA

Imetumwa : November 26th, 2024

Na. Hellen M. Minja,

       Habari – DODOMA RS

Wanawake wametajwa kuonesha mwamko mkubwa kwa kujitokeza kugombea nafasi za wenyeviti wa Vijiji, Vitongoji, Mitaa pamoja na wajumbe wa Halmashauri za Vijiji /wajumbe wa kamati za mitaa ambapo wanawake 260 wamejitokeza kugombea katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024 Mkoa wa Dodoma.

Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule alipokua akizungumza na waandishi wa Habari leo Novemba 26, 2024 katika ukumbi wa Ofisi yake, Jengo la Mkapa Jijini Dodoma kuutangazia Umma juu ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaotarajiwa kufanyika kesho Novemba 27, 2024.

“Katika ngazi ya Mitaa na Vijiji, wanawake 53 wamejitokeza kugombea nafasi za wenyeviti lakini katika ngazi ya vitongoji, wanawake 207 wamejitokeza kugombea nafasi hizo. Hii ni kuonesha kuwa angalau kumekua na mwamko sasa wa usawa wa kijinsia katika maeneo yetu”. Amesema Mhe. Senyamule.

Aidha, ametaja baadhi ya majukumu ya wenyeviti wa Serikali za mitaa kuwa ni pamoja na kutunza rejesta ya wakazi wa maeneo yao na nyaraka nyingine muhimu zinazohusu maendeleo ya maeneo yao pamoja na kumbukumbu za vizazi na vifo, kusimamia ulinzi na usalama wa watu na mali zao pamoja na nyingine nyingi..

Hata hivyo, Mkuu huyo wa Mkoa, ametoa shime kwa wananchi wa Mkoa wake kujitokea kwa wingi kutimiza haki yao ya Kidemokrasia kwa kuchagua viongozi watakaowafaa.

“Nitoe shime kwa Wanadodoma wote, wajitokeze kwa wingi kupiga kura ili kuhakikisha sauti zao  zinasikika na kwamba wanaweza kuchagua Viongozi wenye uwezo wa kuleta mabadiliko chanya katika jamii zao kwani vituo vya kupigia kura ni vya kutosha kwa ujumla wake  ni 4,011” Mhe. Senyamule

Kadhalika, ametoa shukrani kwa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuimarisha demokrasia ya Nchi yetu kwa vitendo, na kutangaza siku ya tarehe 27/11/2024 kuwa siku ya mapumziko, ili Watanzania wapate nafasi ya kushiriki fursa hii adhimu ya kupiga kura.

“Serikali za Mitaa, Sauti ya Wananchi, Jitokeze Kushiriki Uchaguzi”


#kurayakosautiyako    

#ujanjanikupigakura                 #dodomatukotayarikupigakura

#mtiwangubirthdayyangu

Matangazo

  • "WANANCHI JITOKEZENI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU 2025" - RC SENYAMULE February 17, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MADEREVA WA SERIKALI WATAKIWA KUZINGATIA SHERIA ZA USALAMA BARABARANI

    May 17, 2025
  • WATANZANIA WATAKIWA KUILINDA NA KUIDUMISHA AMANI NI KURUHUSU MAENDELEO NCHINI

    May 15, 2025
  • MKURUGENZI WA ‘WATER FOR PEOPLE ‘ AMTEMBELEA RAS MMUYA

    May 16, 2025
  • WANAFUNZI KIDATO CHA SITA WAASWA SAFARI YA ELIMU BADO NI NDEFU

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

RC SENYAMULE AKIZUNGUMZA KWENYE UZINDUZI WA SERA YA ELIMU NA MAFUNZO YA MWAKA 2014 TOLEO LA 2023.
Video Nyinginezo

Kurasa za Karibu

  • Speeches
  • mission and vision
  • Photo Gallery
  • Videos
  • Press Releases
  • Organization Structure
  • Reports
  • Client Service Charter
  • Acts

Tovuti Muhimu

  • PO-RALG
  • Public Service Management
  • Parliament of Tanzania
  • UDOM
  • Government Portal
  • Prime Minister's Office Website

World Visitors Tracker

world map hits counter

Rejesta ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Jengo la Mkapa (Mkapa House) Barabara ya Hospitali ya Mkoa

    Anuani ya Posta: 914 DODOMA

    Simu: +255 26 232 4343/232

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@dodoma.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya eneo

Hakimiliki©2016 GWF . Haki zote zimehifadhiwa.