• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Ofisi |
    • Malalamiko |
    • eoffice |
Dodoma Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Taasisi
      • Huduma Zetu
    • Huduma Zetu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Seksheni
      • Administration and Human Resource Management Section
      • Planning and Coordination
      • Infrastructure section
      • Management Monitoring and Inspection section;
      • Education and vocational Training section
      • Economic and productive sectors section;
      • Health, Social welfare and Nutrition services section
      • Industry, Trade and Investment section
    • Vitengo
      • Information Communication Technology (lcT) and Statistics
      • Government Communication Unit
      • Finance and Accounts unit;
      • Internal Audit unit
      • Legal services unit;
      • Procurement Management unit;
  • Wilaya
    • Bahi
    • Chamwino
    • Kongwa
    • Mpwapwa
    • Kondoa
    • Dodoma Mjini
    • Chemba
  • Mamlaka za Serikali za mitaa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bahi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chemba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa
    • Halmashauri ya Wilaya Mpwapwa
    • Halmashauri ya Mji Kondoa
    • The City Council of Dodoma (CCD)
  • Uwekezaji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Habari kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

UZINDUZI WA MAONESHO YA NANE NANE KANDA YA KATI

Imetumwa : August 3rd, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule ametoa wito kwa wananchi wa Mikoa ya Dodoma na Singida kutembelea mabanda ya maonesho ili kujifunza mbinu na teknolojia mbalimbali za kilimo na ufugaji bora kutoka kwa wakulima na wafugaji wenzao, Taasisi za Kitafiti, bodi za mazao na mashirika mbalimbali ya umma, watu binafsi kwakuwa ni darasa la kujifunza .

Wito huo umetolewa Agosti 2, 2023 wakati akizundua wa Maonyesho ya 15 sherehe za nanenane Kanda ya kati Mwaka huu katika viwanja vya nane nane Nzuguni Jijini Dodoma.

"Utaratibu huu unatoa fursa kwa wananchi wanaotembelea mabanda ya maonesho kujifunza mbinu na teknolojia mbalimbali za kilimo na ufugaji bora kutoka kwa wakulima na wafugaji wenzao, Taasisi za Kitafiti, bodi za mazao na mashirika mbalimbali ya umma na watu binafsi. Hivyo, nawapongeza sana wote mliojiandaa na kujitolea kushiriki katika maonesho haya yenye mafunzo mengi "ameeleza Senyamule

Aidha, Mhe. Senyamule amesema Serikali imepanga kubadilisha kilimo kutoka kilimo cha kujikimu na kuwa kilimo cha kibiashara ambapo amesema mabadiliko hayo yanafanyika kwa kuzingatia malengo ya kitaifa kama yalivyoainishwa kwenye Dira ya Taifa ya Maendeleo 2025, Mpango wa Pili wa Taifa wa Maendeleo 2015 -2025, Sera ya Kilimo ya Mwaka 2013 na Ilani ya Chama cha Mapinduzi 2021-2025.

"Juhudi hizi za Serikali, zinatarajiwa kusaidia wakulima kuanzisha Viwanda vidogo vya kusindika mazao ya kilimo na Mifugo ili kuyaongezea thamani kabla ya kuingizwa sokoni. Kwa kuwa ni rahisi kwa Serikali kusaidia wazalishaji wakiwa kwenye vikundi/ ushirika/ umoja, hivyo nawahamasisha wazalishaji kujiunga katika vikundi ili iwe rahisi kupewa ruzuku au mikopo yenye riba nafuu ambayo itasaidia kuboresha shughuli za uzalishaji na hivyo kuongeza kipato kwa mtu mmoja mmoja na taifa kwa ujumla."amesisitiza Senyamule

Katika hatua nyingine, Mkuu Mkoa huyo amewaagiza wananchi kutunza mazingira kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho kwa kuzuia mmomonyoko wa udongo kwa kuepuka matumizi mabaya ya kemikali, kuacha ukataji miti ovyo, kuchoma moto, ufugaji holela, kulima kwenye vyanzo vya maji na kuzingatia matumizi sahihi ya zana za kilimo na pembejeo.

Kwa Upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhe. Peter Selukamba amesema pato la Mkoa wa Singida linategemea wakulima, wafugaji na wavuvi hivyo maonesho hayo yatakuwa chachu ya maendeleo kwani yanatoa ujuzi na elimu za teknolojia wezeshi.

Amesema shughuli za kilimo zinatekelezwa kwa lengo la kuhakikisha upatikanaji wa chakula cha ziada kwa matumizi ya chakula na biashara kupitia mbinu mbalimbali ikiwani pamoja na kilimo cha umwagiliaji kinachorahisisha kilimo kwa mwaka mzima.

Naye, Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mhe.Jabir Shekimweri akizungumza kwa niaba ya Wakuu wa Wilaya ya Mikoa hiyo ametoa wito kwa Wananchi kujitokeza kwa wingi kujionea teknolojia mbalimbali za kilimo zitakazo wawezesha kufanya kilimo chenye tija na manufaa ya vizazi vijavyo.

Matangazo

  • "WANANCHI JITOKEZENI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU 2025" - RC SENYAMULE February 17, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MADEREVA WA SERIKALI WATAKIWA KUZINGATIA SHERIA ZA USALAMA BARABARANI

    May 17, 2025
  • WATANZANIA WATAKIWA KUILINDA NA KUIDUMISHA AMANI NI KURUHUSU MAENDELEO NCHINI

    May 15, 2025
  • MKURUGENZI WA ‘WATER FOR PEOPLE ‘ AMTEMBELEA RAS MMUYA

    May 16, 2025
  • WANAFUNZI KIDATO CHA SITA WAASWA SAFARI YA ELIMU BADO NI NDEFU

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

RC SENYAMULE AKIZUNGUMZA KWENYE UZINDUZI WA SERA YA ELIMU NA MAFUNZO YA MWAKA 2014 TOLEO LA 2023.
Video Nyinginezo

Kurasa za Karibu

  • Speeches
  • mission and vision
  • Photo Gallery
  • Videos
  • Press Releases
  • Organization Structure
  • Reports
  • Client Service Charter
  • Acts

Tovuti Muhimu

  • PO-RALG
  • Public Service Management
  • Parliament of Tanzania
  • UDOM
  • Government Portal
  • Prime Minister's Office Website

World Visitors Tracker

world map hits counter

Rejesta ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Jengo la Mkapa (Mkapa House) Barabara ya Hospitali ya Mkoa

    Anuani ya Posta: 914 DODOMA

    Simu: +255 26 232 4343/232

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@dodoma.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya eneo

Hakimiliki©2016 GWF . Haki zote zimehifadhiwa.