• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Ofisi |
    • Malalamiko |
    • eoffice |
Dodoma Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Taasisi
      • Huduma Zetu
    • Huduma Zetu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Seksheni
      • Administration and Human Resource Management Section
      • Planning and Coordination
      • Infrastructure section
      • Management Monitoring and Inspection section;
      • Education and vocational Training section
      • Economic and productive sectors section;
      • Health, Social welfare and Nutrition services section
      • Industry, Trade and Investment section
    • Vitengo
      • Information Communication Technology (lcT) and Statistics
      • Government Communication Unit
      • Finance and Accounts unit;
      • Internal Audit unit
      • Legal services unit;
      • Procurement Management unit;
  • Wilaya
    • Bahi
    • Chamwino
    • Kongwa
    • Mpwapwa
    • Kondoa
    • Dodoma Mjini
    • Chemba
  • Mamlaka za Serikali za mitaa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bahi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chemba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa
    • Halmashauri ya Wilaya Mpwapwa
    • Halmashauri ya Mji Kondoa
    • The City Council of Dodoma (CCD)
  • Uwekezaji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Habari kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WAKANDARASI TEKELEZENI SHERIA NA TARATIBU ZA UTUMISHI KWA WAFANYAKAZI WENU -RC SENYAMULE

Imetumwa : November 9th, 2023


Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe.Rosemary Senyamule ametoa wito kwa wakandarasi wote waliopata nafasi ya kutekeleza miradi ya kimkakati katika jiji la Dodoma kuhakikisha wanakua na usimamizi mzuri kwa Watumishi wao kwa kufuata kanuni na taratibu za kiutumishi.

Wito huo umetolewa leo Novemba 8, 2023 wakati wa ziara ya kikazi ya ukaguzi wa miradi ya ujenzi wa barabara zilizo chini ya Wakala wa Barabara nchini (TANROADS) pamoja na Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) katika mradi wa barabara ya mzunguko wa nje (outer ringroad) ikiwa ni muendelezo wa ziara zake ambazo amekua akizifanya katika miradi inayoendelea kutekelezwa ndani ya Mkoa wa Dodoma.

"Niendelee kutoa wito kwa wote wanaopata nafasi za kutekeleza miradi mbalimbali ya kimaendeleo, muhakikishe munafuata taratibu za utumishi ,tusingependa kuona masuala ya unyanyasaji kwa wafanyakazi hivyo hakikisheni mnatatua migogoro yote ili kuwezesha kukamilisha miradi kwa wakati " Ameeleza Mhe. Senyamule

Aidha, amewahimiza wakandarasi wakati wanapoendelea na utekelezaji wa Ujenzi wa barabara hiyo, kuhakikisha wanapanda miti yenye kuvutia pembezoni mwa barabara ili kupendezesha barabara, pia ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa agenda ya kutunza Mazingira katika jiji la Dodoma.

Pia, Mhe. Senyamule amewasisitiza wakandarasi kukamilisha miradi kwa wakati na ubora unaotakiwa na ikiwezekana kuhakikisha wanakamilisha kabla ya muda uliopangwa wa miradi kukamilika .

Kwa Upande Wake, Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mjini Mhe.Jabir Shekimweri amewataka waajiri kuhakikisha wanajali maslahi ya Watumishi ili kuepusha changamoto za wizi wa vifaa vya kufanyia kazi .

Miradi ya Barabara iliyokaguliwa chini ya (TARURA) ni eneo la Mlimwa Ringi-Road yenye urefu wa Km 2.7 inayojengwa kwa kiwango cha Lami awamu ya tatu inayogharimu kiasi cha shilingi 2,577,534,902 ambapo hadi sasa umefikia asilimia 63, Barabara ya Bima yenye urefu wa Km 2.0 inayojengwa kwa kiwango cha Lami ngumu (asphalt concrete) inayogharimu kiasi cha 2,409,187,951.00 ambapo imefikia asilimia 33 hadi sasa na Barabara ya Mlimwa C (kuzunguka Makazi ya Waziri Mkuu) yenye urefu wa Km 2.6 inayogharimu kiasi cha 2,990,540,068.8 ambayo imefikia asilimia 72 kukamilika .

Awali alianza na barabara za Uwanja wa ndege wa Kimataifa Msalato na kumalizia barabara ya Mzunguko wa nje wa jiji la Dodoma yenye jumla ya urefu wa kilomita 112,3 kipande cha Veyula -Mtumba hadi Ihumwa yenye urefu wa kilomita 52.3 ambayo ilianza Septemba 20,2021 na inatarajiwa kukamilika Desemba 07,2024 na inagharimu kiasi cha shillingi 100,840,778,592.00 Ujenzi huo una lengo la kupunguza msongamano wa magari ndani ya jiji la Dodoma.

Matangazo

  • "WANANCHI JITOKEZENI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU 2025" - RC SENYAMULE February 17, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MADEREVA WA SERIKALI WATAKIWA KUZINGATIA SHERIA ZA USALAMA BARABARANI

    May 17, 2025
  • WATANZANIA WATAKIWA KUILINDA NA KUIDUMISHA AMANI NI KURUHUSU MAENDELEO NCHINI

    May 15, 2025
  • MKURUGENZI WA ‘WATER FOR PEOPLE ‘ AMTEMBELEA RAS MMUYA

    May 16, 2025
  • WANAFUNZI KIDATO CHA SITA WAASWA SAFARI YA ELIMU BADO NI NDEFU

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

RC SENYAMULE AKIZUNGUMZA KWENYE UZINDUZI WA SERA YA ELIMU NA MAFUNZO YA MWAKA 2014 TOLEO LA 2023.
Video Nyinginezo

Kurasa za Karibu

  • Speeches
  • mission and vision
  • Photo Gallery
  • Videos
  • Press Releases
  • Organization Structure
  • Reports
  • Client Service Charter
  • Acts

Tovuti Muhimu

  • PO-RALG
  • Public Service Management
  • Parliament of Tanzania
  • UDOM
  • Government Portal
  • Prime Minister's Office Website

World Visitors Tracker

world map hits counter

Rejesta ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Jengo la Mkapa (Mkapa House) Barabara ya Hospitali ya Mkoa

    Anuani ya Posta: 914 DODOMA

    Simu: +255 26 232 4343/232

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@dodoma.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya eneo

Hakimiliki©2016 GWF . Haki zote zimehifadhiwa.