• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Ofisi |
    • Malalamiko |
    • eoffice |
Dodoma Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Taasisi
      • Huduma Zetu
    • Huduma Zetu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Seksheni
      • Administration and Human Resource Management Section
      • Planning and Coordination
      • Infrastructure section
      • Management Monitoring and Inspection section;
      • Education and vocational Training section
      • Economic and productive sectors section;
      • Health, Social welfare and Nutrition services section
      • Industry, Trade and Investment section
    • Vitengo
      • Information Communication Technology (lcT) and Statistics
      • Government Communication Unit
      • Finance and Accounts unit;
      • Internal Audit unit
      • Legal services unit;
      • Procurement Management unit;
  • Wilaya
    • Bahi
    • Chamwino
    • Kongwa
    • Mpwapwa
    • Kondoa
    • Dodoma Mjini
    • Chemba
  • Mamlaka za Serikali za mitaa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bahi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chemba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa
    • Halmashauri ya Wilaya Mpwapwa
    • Halmashauri ya Mji Kondoa
    • The City Council of Dodoma (CCD)
  • Uwekezaji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Habari kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MACHINGA DODOMA WAMPONGEZA DKT. SAMIA SULUHU HASSAN

Imetumwa : March 23rd, 2023

 MACHINGA DODOMA WAMPONGEZA DKT. SAMIA SULUHU HASSAN

Kundi la Machinga Mkoa wa Dodoma leo tarehe 23/03/2023 wamefanya maandamano ya amani ya kumpongeza Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuwaheshimisha ndani ya kipindi cha miaka miwili ya uongozi wake.

Akipokea maandamano hayo ya amani Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule amewapongeza wafanyabiashara wadogowadogo (Machinga) kwa kufanya kazi zao kwa utulivu na juhudi na kutambua mchango wa Rais Mama Samia Suluhu katika kipindi cha miaka miwili madarakani.

"Ninayo furaha kwasababu kundi hili ambalo nchi yetu imekuwa ikihangaika nalo leo ni kundi ambalo linafuraha na amani na linafanya kazi zake kwa utulivu katika mkoa wetu niwapongeze kwa juhudi, Utashi, busara na hekima na ndio maana leo hii mmeona umuhimu wa kumpongeza Mhe. Rais wetu.

"Jambo mlilofanya Leo linaipa fahari Dodoma kama ambavyo risala yenu inasema Mambo yaliyofanyika ni mengi mno na yataandikwa kwenye historia ya nchi ya Tanzania lakini huenda Afrika Mashariki kwasababu Machinga Dodoma ni sehemu ya mfano na nyie mmewaona wageni mbalimbali wakitembelea hapa kufanya utalii."Amesema Senyamule

Kwa upande wake Mwenyekiti Msaidizi Machinga Mkoa wa Dodoma Bw. Christian Msumari ameishukuru Serikali ya awamu ya Sita kwa kuwatambua kama kundi rasmi na kuwaweka chini ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalumu jambo ambalo linawapa urahisi wa kutimiza majukumu yao kwa kusimamiwa na kupatiwa Mafunzo mbalimbali.

"Tunashukuru kwa kututambua kama kundi rasmi na kutuweka chini ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalumu na kwa kufanya hivo imetumefanya tuweze kupata Mafunzo ya uongozi na tumepata Wizara ya kutulea na kutusaidia.

"Tunamshukuru mama kwa kutupatia mikopo ya asilimia 10 ya Halmashauri za Wilaya, Miji na Majiji inayolenga makundi ya vijana, wanawake, walemavu na Machinga tukiwa kundi jipya lililoongezwa kunufaika na mikopo na sisi tumenufaika nayo kupitia vikundi vya watu watano na kila aliyekidhi vigezo amepatiwa shillingi milioni 1" Amesema Bw. Msumari

Aidha Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mjini Mhe. Jabir Shekimweri amewaasa wamachinga wa soko hilo kutunza miundombinu ya soko hilo ili kuendelea kufanya kazi zao kwa urahihisi na kuhakikisha linadumu kwa muda mrefu.

Hafla hiyo imeadhimishwa kwa kaulimbiu ya "miwili ya mama fur-SAMIA kwa wamachinga" huku mgeni rasmi akiwa ni Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe Rosemary Senyamule, halfa iliyofanyika katika soko la Machinga Complex Dodoma na kuandaliwa na wafanyabiashara wenyewe.

Matangazo

  • "WANANCHI JITOKEZENI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU 2025" - RC SENYAMULE February 17, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MADEREVA WA SERIKALI WATAKIWA KUZINGATIA SHERIA ZA USALAMA BARABARANI

    May 17, 2025
  • WATANZANIA WATAKIWA KUILINDA NA KUIDUMISHA AMANI NI KURUHUSU MAENDELEO NCHINI

    May 15, 2025
  • MKURUGENZI WA ‘WATER FOR PEOPLE ‘ AMTEMBELEA RAS MMUYA

    May 16, 2025
  • WANAFUNZI KIDATO CHA SITA WAASWA SAFARI YA ELIMU BADO NI NDEFU

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

RC SENYAMULE AKIZUNGUMZA KWENYE UZINDUZI WA SERA YA ELIMU NA MAFUNZO YA MWAKA 2014 TOLEO LA 2023.
Video Nyinginezo

Kurasa za Karibu

  • Speeches
  • mission and vision
  • Photo Gallery
  • Videos
  • Press Releases
  • Organization Structure
  • Reports
  • Client Service Charter
  • Acts

Tovuti Muhimu

  • PO-RALG
  • Public Service Management
  • Parliament of Tanzania
  • UDOM
  • Government Portal
  • Prime Minister's Office Website

World Visitors Tracker

world map hits counter

Rejesta ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Jengo la Mkapa (Mkapa House) Barabara ya Hospitali ya Mkoa

    Anuani ya Posta: 914 DODOMA

    Simu: +255 26 232 4343/232

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@dodoma.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya eneo

Hakimiliki©2016 GWF . Haki zote zimehifadhiwa.