• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Ofisi |
    • Malalamiko |
    • eoffice |
Dodoma Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Taasisi
      • Huduma Zetu
    • Huduma Zetu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Seksheni
      • Administration and Human Resource Management Section
      • Planning and Coordination
      • Infrastructure section
      • Management Monitoring and Inspection section;
      • Education and vocational Training section
      • Economic and productive sectors section;
      • Health, Social welfare and Nutrition services section
      • Industry, Trade and Investment section
    • Vitengo
      • Information Communication Technology (lcT) and Statistics
      • Government Communication Unit
      • Finance and Accounts unit;
      • Internal Audit unit
      • Legal services unit;
      • Procurement Management unit;
  • Wilaya
    • Bahi
    • Chamwino
    • Kongwa
    • Mpwapwa
    • Kondoa
    • Dodoma Mjini
    • Chemba
  • Mamlaka za Serikali za mitaa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bahi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chemba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa
    • Halmashauri ya Wilaya Mpwapwa
    • Halmashauri ya Mji Kondoa
    • The City Council of Dodoma (CCD)
  • Uwekezaji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Habari kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mkoa Dodoma Mwenyeji ,Maadhimisho Ya Siku Ya Mtoto wa Afrika

Imetumwa : June 16th, 2022

Mkoa wa Dodoma umekua mwenyeji wa maadhimisho ya siku ya Mtoto wa Afrika Kitaifa ambayo yamefanyika katika viwanja vya Nyerere Square huku mgeni rasmi akiwa Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dorothy Gwajima (Mb).

Akiwasilisha salamu za Mkoa, mwenyeji  wa maoenesho hayo ya kitaifa, ambaye ni Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Anthony Mtaka , amesema  anayofuraha kubwa kwa Mkoa wake kuchaguliwa kuwa mwenyeji wa maadhimisho hayo na ataomba kuwa mwenyeji wa maadhimisho mengine zaidi.

Akizungumzia suala la matukio ya kikatili wanayofanyiwa watoto, Mhe. Mtaka amesema: “Viongozi wa Serikali za Mitaa katika Mkoa wangu wanafanya jitihada za kuhakikisha haki za watoto zinalindwa na wazazi tujitahidi kupambana na mmomonyoko wa maadili hasa kwa watoto wetu kwa sasa kwani tukiifumbia macho hali iliyopo sasa, tutakuja kutengeneza kizazi cha chokoraa na ombaomba wazee wa baadae”

Wanafunzi kutoka Shule ya Sekondari ya Bunge walipata nafasi ya kusoma risala waliyoiandaa mbele ya Mgeni rasmi ambapo imeelezea kuwa watoto wamekua wahanga wa matukio ya kikatili yanayoendelea katika jamii na wanaumia kusikia matukio hayo yakiendelea kushika kasi kila uchao na wameitaka Jamii kutoa ushirikiano pindi vinapotokea vitendo hivi. Pia wamewataka wadau wa maendeleo ya Jamii kuendelea kutoa ushirikiano ili kutokomeza vitendo vya kikatili kwa watoto.

Nao wadau wa masuala ya haki za watoto ambao nao walishiriki katika maadhimisho hayo, walitoa pongezi kwa Serikali kwa kuanzishwa kwa miongozo itakayowezesha upatikanaji wa haki za watoto kwa urahisi ambapo miongozo hiyo pia italeta mabadiliko makubwa katika kutokomeza ukatili kwa watoto waliopo ndani na nje ya shule.

Mgeni Rasmi Mhe. Dorothy Gwajima, alipata nafasi ya kuongea katika hafla hiyo ambapo alisema kuwa amesikia kilio cha watoto kutokana na risala yao kwa kusikitishwa na vitendo vya kikatili wanavyofanyiwa watoto wenzao hivyo ametoa salamu za Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kuwa ameapa kuwalinda watoto , kwani kupitia Wizara yake tayari kunautungaji wa sheria ikiwemo ile Na. 21 ya mwaka 2019 ambayo imerekebishwa na inaendelea kurekebishwa ili iweze kuwawajibisha zaidi wale wote watakaobainika kutenda ukatili kwa watoto.

Mhe. Gwajima ameongeza kuwa baadhi ya vifungu kwenye sheria vimebadilishwa ikiwemo kile cha adhabu kwa mtu atakayebainika kumpa ujauzito mwanafunzi na kuna vituo 427 vya dawati la Jinsia vimeanzishwa kwa lengo la kuwapa nafasi watoto kwenda kutoa taarifa pindi wanapobaini mtu anatenda au anataka kutenda ukatili kwa mtoto au watoto. Mwisho amewaasa wananchi na kuwataka kila mtu afanye kazi katika eneo lake kulinda haki za watoto.

MWISHO

Matangazo

  • "WANANCHI JITOKEZENI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU 2025" - RC SENYAMULE February 17, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MADEREVA WA SERIKALI WATAKIWA KUZINGATIA SHERIA ZA USALAMA BARABARANI

    May 17, 2025
  • WATANZANIA WATAKIWA KUILINDA NA KUIDUMISHA AMANI NI KURUHUSU MAENDELEO NCHINI

    May 15, 2025
  • MKURUGENZI WA ‘WATER FOR PEOPLE ‘ AMTEMBELEA RAS MMUYA

    May 16, 2025
  • WANAFUNZI KIDATO CHA SITA WAASWA SAFARI YA ELIMU BADO NI NDEFU

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

RC SENYAMULE AKIZUNGUMZA KWENYE UZINDUZI WA SERA YA ELIMU NA MAFUNZO YA MWAKA 2014 TOLEO LA 2023.
Video Nyinginezo

Kurasa za Karibu

  • Speeches
  • mission and vision
  • Photo Gallery
  • Videos
  • Press Releases
  • Organization Structure
  • Reports
  • Client Service Charter
  • Acts

Tovuti Muhimu

  • PO-RALG
  • Public Service Management
  • Parliament of Tanzania
  • UDOM
  • Government Portal
  • Prime Minister's Office Website

World Visitors Tracker

world map hits counter

Rejesta ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Jengo la Mkapa (Mkapa House) Barabara ya Hospitali ya Mkoa

    Anuani ya Posta: 914 DODOMA

    Simu: +255 26 232 4343/232

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@dodoma.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya eneo

Hakimiliki©2016 GWF . Haki zote zimehifadhiwa.