• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Ofisi |
    • Malalamiko |
    • eoffice |
Dodoma Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Taasisi
      • Huduma Zetu
    • Huduma Zetu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Seksheni
      • Administration and Human Resource Management Section
      • Planning and Coordination
      • Infrastructure section
      • Management Monitoring and Inspection section;
      • Education and vocational Training section
      • Economic and productive sectors section;
      • Health, Social welfare and Nutrition services section
      • Industry, Trade and Investment section
    • Vitengo
      • Information Communication Technology (lcT) and Statistics
      • Government Communication Unit
      • Finance and Accounts unit;
      • Internal Audit unit
      • Legal services unit;
      • Procurement Management unit;
  • Wilaya
    • Bahi
    • Chamwino
    • Kongwa
    • Mpwapwa
    • Kondoa
    • Dodoma Mjini
    • Chemba
  • Mamlaka za Serikali za mitaa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bahi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chemba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa
    • Halmashauri ya Wilaya Mpwapwa
    • Halmashauri ya Mji Kondoa
    • The City Council of Dodoma (CCD)
  • Uwekezaji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Habari kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

UONGOZI WA KLABU YA MICHEZO OFISI YA MKUU WA MKOA WA DODOMA WAKUTANA NA RAS KAZUNGU

Imetumwa : September 25th, 2025

Na. Hellen M. Minja

       Habari – DODOMA RS

Viongozi wa Klabu ya Michezo ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma wakiongozwa na Mwenyekiti wake Dr. Nassoro A. Matuzya, leo Septemba 25, 2025 wamefanya mazungumzo mafupi na Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma juu ya ushiriki wao kwenye Mashindano ya Shirikisho la Michezo ya Wizara na Idara za Serikali (SHIMIWI) 2025.

Sambamba nae, pia ameongozana na Viongozi wengine ambao ni Katibu wa Klabu Bw. Majuto Msekela, Nahodha wa Timu ya Michezo ya Wanaume Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Bw. Prosper Sanga na Mjumbe wa Kamati ya Michezo ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Dodoma Bw. John Kidasi kwenye Ofisi ya Katibu Tawala Mkoa Jengo la Mkapa Jijini humu.

Lengo la mazungumzo hayo ni kumpatia taarifa ya ushiriki wao katika Mashindano hayo ambayo mwaka huu, yamefanyika Mkoani Mwanza, huku timu ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma ikifanikiwa kushiriki michezo hiyo kwa kupeleka Timu ya Wanaume ambayo iliwakilisha katika michezo ya Mpira wa Miguu na kufika hatua ya16 bora.

Aidha, Mchezo mwingine ambao Timu hiyo ilishiriki ni wa kusukuma kete (Draft) kwa Wanaume ambapo walifanikiwa kufikia hatua ya robo fainali na Timu kukabidhiwa Cheti, Medali ya ushiriki sambamba na Jarida la taarifa ya Shirikisho hilo kwa mwaka uliopita wa 2024.

Hata hivyo, Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma Dkt. Khatibu Kazungu, ametoa rai kwa Viongozi hao kujiandaa vizuri na mapema kwa ajili ya mashindano ya mwakani kwa kuhakikisha wanapeleka timu yenye uwezo thabiti wa kurudi na ushindi kwa sababu Mkoa una Watumishi wa kutosha na wenye uwezo wa kushiriki mashindano hayo ipasavyo.

Michezo ya SHIMIWI ni maelekezo ya Rais wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan - aliyoyatoa Agosti 14, 2025 kwa kuelekeza Wizara ya Sanaa, Utamaduni na Michezo kuhakikisha Wizara, Taasisi na Idara zote za Serikali zinashiriki na mwaka huu

ilianza Septemba Mosi na kuhitimishwa Septemba 16 na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda.


#dodomafahariyawatanzania

#keroyakowajibuwangu

#nimejiandikishanitapigakura

Matangazo

  • No records found
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • DODOMA NI SEHEMU NZURI YA UWEKEZAJI

    October 01, 2025
  • CCTV CAMERA KUFICHUA WAVUNJIFU WA SHERIA KATIKA JIJI LA DODOMA

    September 30, 2025
  • DODOMA YAADHIMISHA SIKU YA UTALII DUNIANI KWENYE MICHORO YA MIAMBANI KONDOA

    September 27, 2025
  • JUHUDI KUDHIBITI VIFO VYA WAJAWAZITO ZAPAMBA MOTO

    September 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

RC SENYAMULE AKIZUNGUMZA KWENYE UZINDUZI WA SERA YA ELIMU NA MAFUNZO YA MWAKA 2014 TOLEO LA 2023.
Video Nyinginezo

Kurasa za Karibu

  • Speeches
  • mission and vision
  • Photo Gallery
  • Videos
  • Press Releases
  • Organization Structure
  • Reports
  • Client Service Charter
  • Acts

Tovuti Muhimu

  • PO-RALG
  • Public Service Management
  • Parliament of Tanzania
  • UDOM
  • Government Portal
  • Prime Minister's Office Website

World Visitors Tracker

world map hits counter

Rejesta ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Jengo la Mkapa (Mkapa House) Barabara ya Hospitali ya Mkoa

    Anuani ya Posta: 914 DODOMA

    Simu: +255 26 232 4343/232

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@dodoma.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya eneo

Hakimiliki©2016 GWF . Haki zote zimehifadhiwa.