• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Ofisi |
    • Malalamiko |
    • eoffice |
Dodoma Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Taasisi
      • Huduma Zetu
    • Huduma Zetu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Seksheni
      • Administration and Human Resource Management Section
      • Planning and Coordination
      • Infrastructure section
      • Management Monitoring and Inspection section;
      • Education and vocational Training section
      • Economic and productive sectors section;
      • Health, Social welfare and Nutrition services section
      • Industry, Trade and Investment section
    • Vitengo
      • Information Communication Technology (lcT) and Statistics
      • Government Communication Unit
      • Finance and Accounts unit;
      • Internal Audit unit
      • Legal services unit;
      • Procurement Management unit;
  • Wilaya
    • Bahi
    • Chamwino
    • Kongwa
    • Mpwapwa
    • Kondoa
    • Dodoma Mjini
    • Chemba
  • Mamlaka za Serikali za mitaa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bahi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chemba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa
    • Halmashauri ya Wilaya Mpwapwa
    • Halmashauri ya Mji Kondoa
    • The City Council of Dodoma (CCD)
  • Uwekezaji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Habari kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

CHEMBA WAASWA KUTOFANYA KAZI KWA MAZOEA

Imetumwa : May 27th, 2023


Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule amemuagiza Mkuu wa Wilaya Chemba kusimamia kwa karibu ukamilishaji wa ujenzi wa madarasa katika Wilaya yake ndani ya muda uliopangwa.

Senyamule ametoa agizo hilo leo tarehe 27 Mei, 2023 baada ya kufanya ziara ya kikazi katika Wilaya ya Chemba na Kondoa kukagua ujenzi wa madarasa kupitia fedha za boost.

Akiwa Wilayani Chemba katika Shule ya Msingi Soya Senyamule ameonyesha kutoridhishwa na maendeleo ya ujenzi katika Shule hiyo na kuhoji endapo wanajua ni lini madarasa hayo yanatakiwa kukamilika.

"Sijafurahishwa kabisa na kasi ya ujenzi wa vyumba vya madarasa katika Shule hii, tunapotoa maelekezo ni lazima yazingatiwe. Tarehe 20 Juni 2023 kazi inatakiwa kukamilika, Wilaya ikabidhi kwa Mkoa tupate muda wa kufanya ukaguzi ili nasi tarehe 30 Juni 2023, tukabidhi TAMISEMI" Senyamule alisisitiza.

Senyamule amesema nia na dhamira ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni kuhakikisha miradi hususan ya ujenzi wa Shule na Vyumba vya madarasa unakamilika kwa wakati, hivyo ni vema kila mtendaji kuhakikisha anaenda sawia na spidi ya Mheshimiwa Rais.

Akiwa Wilayani Kondoa Senyamule amekagua pia ujenzi wa Shule mpya ya msingi yenye madarasa 7 na madarasa 2 ya awali katika eneo la ‘Maji ya Shamba’ na Shule ya Msingi Miningani ambapo ujenzi wa madarasa 6 unaendelea.

"Nahitaji kupewa taarifa ya kila siku ya mwenendo wa ujenzi wa Shule hizi na madarasa yake. Tunaposema kukamilika, tukabidhiwe darasa na madawati yake ndani" Senyamule alifafanua.

Mkuu wa Wilaya ya Chemba Mhe. Gerald Mongella na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Kondoa Bw. Paul Sweya wamemhakikiashia Mkuu wa Mkoa kuwa watahakikisha usimamizi madhubuti wa ujenzi na Shule na madarasa ili yaweze kukamilika kwa mujibu wa mpango kazi.

Mkoa wa Dodoma kupitia mradi wa Boost umepokea kiasi cha Shilingi Bilioni 10.6 kwa ajili ujenzi wa Shule mpya 16, vyumba vya madasa ya msingi 163, madarasa ya awali 16, ujenzi wa vyoo 106, nyumba za walimu 03 na darasa 01 la elimu maalumu. Wilaya ya Chemba imepokea kiasi cha shilingi Bilioni 1.3 na Kondoa Mji na Halmashauri Shilingi Bilioni 1.7

Matangazo

  • "WANANCHI JITOKEZENI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU 2025" - RC SENYAMULE February 17, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATANZANIA WATAKIWA KUILINDA NA KUIDUMISHA AMANI NI KURUHUSU MAENDELEO NCHINI

    May 15, 2025
  • MKURUGENZI WA ‘WATER FOR PEOPLE ‘ AMTEMBELEA RAS MMUYA

    May 16, 2025
  • WANAFUNZI KIDATO CHA SITA WAASWA SAFARI YA ELIMU BADO NI NDEFU

    May 17, 2025
  • RC SENYAMULE AZUNGUMZA NA MAKUNDI MBALIMBALI MKOANI KWAKE

    May 15, 2025
  • Tazama Zote

Video

RC SENYAMULE AKIZUNGUMZA KWENYE UZINDUZI WA SERA YA ELIMU NA MAFUNZO YA MWAKA 2014 TOLEO LA 2023.
Video Nyinginezo

Kurasa za Karibu

  • Speeches
  • mission and vision
  • Photo Gallery
  • Videos
  • Press Releases
  • Organization Structure
  • Reports
  • Client Service Charter
  • Acts

Tovuti Muhimu

  • PO-RALG
  • Public Service Management
  • Parliament of Tanzania
  • UDOM
  • Government Portal
  • Prime Minister's Office Website

World Visitors Tracker

world map hits counter

Rejesta ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Jengo la Mkapa (Mkapa House) Barabara ya Hospitali ya Mkoa

    Anuani ya Posta: 914 DODOMA

    Simu: +255 26 232 4343/232

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@dodoma.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya eneo

Hakimiliki©2016 GWF . Haki zote zimehifadhiwa.