• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Ofisi |
    • Malalamiko |
    • eoffice |
Dodoma Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Taasisi
      • Huduma Zetu
    • Huduma Zetu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Seksheni
      • Administration and Human Resource Management Section
      • Planning and Coordination
      • Infrastructure section
      • Management Monitoring and Inspection section;
      • Education and vocational Training section
      • Economic and productive sectors section;
      • Health, Social welfare and Nutrition services section
      • Industry, Trade and Investment section
    • Vitengo
      • Information Communication Technology (lcT) and Statistics
      • Government Communication Unit
      • Finance and Accounts unit;
      • Internal Audit unit
      • Legal services unit;
      • Procurement Management unit;
  • Wilaya
    • Bahi
    • Chamwino
    • Kongwa
    • Mpwapwa
    • Kondoa
    • Dodoma Mjini
    • Chemba
  • Mamlaka za Serikali za mitaa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bahi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chemba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa
    • Halmashauri ya Wilaya Mpwapwa
    • Halmashauri ya Mji Kondoa
    • The City Council of Dodoma (CCD)
  • Uwekezaji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Habari kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

DKT. MGANGA AFUNGUA MAFUNZO MRADI WA SHULE BORA

Imetumwa : January 27th, 2023

Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma Dkt Fatuma Mganga ametoa rai kwa waandishi wa habari wanaofanya kazi ndani ya Mkoa huo kutangaza mafanikio yaliyopatikana katika sekta ya elimu pamoja na kuyatangaza kwa jamii.

Rai hiyo ameitoa Januari 27, 2023 Wilayani Kondoa wakati akifungua mafunzo ya Siku Moja kwa maafisa habari na waandishi wa habari, yenye lengo la kuwajengea uwezo kufahamu Mradi wa Shule Bora na kuhamasisha jamii kushiriki kikamilifu Katika masuala ya elimu.

Akizungumzia suala la maendeleo ya Elimu Katika Mkoa amesema suala la Elimu katika Mkoa wa Dodoma bado halijatangazwa vizuri na kuwataka waandishi wa habari wakawe chachu cha kuielimisha jamii.

Pia amempongeza Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa jitihada zake za dhati za kuongeza pesa za maendeleo katika mkoa wa Dodoma ambapo shilingi bilioni 7.8 zimetolewa na kuwezesha kujenga vyumba vya madarasa 393 kwa Shule za Msingi na madarasa 130 yamejengwa kwa Shule za Sekondari yamejengwa kwa gharama ya shilingi Bilioni 20

Aidha amewaeleza waandishi wa habari kuwa Rais Samia ameongeza bajeti ya Elimu bila malipo kwa Shule za Misingi na Sekondari.

Pamoja na jitihada hizo za serikali amewataka wazazi kushirikiana na serikali katika ujenzi na uhifadhi wa Miundombinu ya elimu ikiwemo ya madarasa ambapo ameeleza Mkoa kuwa na upungufu wa vyumba vya madarasa 7000, ambapo mwaka huu peke yake wanatarajia zaidi ya wanafunzi elfu 90 kuanza masomo.

Aidha amewaomba wazazi wawapeleke watoto shule, wasiwafiche na kuwatumikisha Shughuli za kilimo na kazi za ndani.

Mbali na hilo amekemea dhana iliyozoeleka kwamba Mkoa wa Dodoma ni wa kutoa Wasaidizi wa Shughuli za ndani.

Mpaka kufikia Januari 26 , 2023 ni asilimia 89.7 ya wanafunzi wa madarasa ya awali wameripoti shule, asilimia 94.2 Kwa darasa la kwanza na asilimia 66.95 kidato Cha kwanza.

“Mwisho nawaomba waandishi wa habari mkasaidie kutangaza mafanikio ya Mkoa  yaliyopatikana katika sekta ya elimu, ili jamii iweze kuyafahamu pia kurahisisha serikali kuendelea kutuunga Mkono katika jitihada zetu hizi”. Alisema Dkt. Mganga

Matangazo

  • "WANANCHI JITOKEZENI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU 2025" - RC SENYAMULE February 17, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATANZANIA WATAKIWA KUILINDA NA KUIDUMISHA AMANI NI KURUHUSU MAENDELEO NCHINI

    May 15, 2025
  • MKURUGENZI WA ‘WATER FOR PEOPLE ‘ AMTEMBELEA RAS MMUYA

    May 16, 2025
  • WANAFUNZI KIDATO CHA SITA WAASWA SAFARI YA ELIMU BADO NI NDEFU

    May 17, 2025
  • RC SENYAMULE AZUNGUMZA NA MAKUNDI MBALIMBALI MKOANI KWAKE

    May 15, 2025
  • Tazama Zote

Video

RC SENYAMULE AKIZUNGUMZA KWENYE UZINDUZI WA SERA YA ELIMU NA MAFUNZO YA MWAKA 2014 TOLEO LA 2023.
Video Nyinginezo

Kurasa za Karibu

  • Speeches
  • mission and vision
  • Photo Gallery
  • Videos
  • Press Releases
  • Organization Structure
  • Reports
  • Client Service Charter
  • Acts

Tovuti Muhimu

  • PO-RALG
  • Public Service Management
  • Parliament of Tanzania
  • UDOM
  • Government Portal
  • Prime Minister's Office Website

World Visitors Tracker

world map hits counter

Rejesta ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Jengo la Mkapa (Mkapa House) Barabara ya Hospitali ya Mkoa

    Anuani ya Posta: 914 DODOMA

    Simu: +255 26 232 4343/232

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@dodoma.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya eneo

Hakimiliki©2016 GWF . Haki zote zimehifadhiwa.