• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Ofisi |
    • Malalamiko |
    • eoffice |
Dodoma Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Taasisi
      • Huduma Zetu
    • Huduma Zetu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Seksheni
      • Administration and Human Resource Management Section
      • Planning and Coordination
      • Infrastructure section
      • Management Monitoring and Inspection section;
      • Education and vocational Training section
      • Economic and productive sectors section;
      • Health, Social welfare and Nutrition services section
      • Industry, Trade and Investment section
    • Vitengo
      • Information Communication Technology (lcT) and Statistics
      • Government Communication Unit
      • Finance and Accounts unit;
      • Internal Audit unit
      • Legal services unit;
      • Procurement Management unit;
  • Wilaya
    • Bahi
    • Chamwino
    • Kongwa
    • Mpwapwa
    • Kondoa
    • Dodoma Mjini
    • Chemba
  • Mamlaka za Serikali za mitaa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bahi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chemba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa
    • Halmashauri ya Wilaya Mpwapwa
    • Halmashauri ya Mji Kondoa
    • The City Council of Dodoma (CCD)
  • Uwekezaji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Habari kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

DODOMA YAJIPANGA KUKABILIANA NA UTORO SHULENI 2023

Imetumwa : December 21st, 2022

Mkoa wa Dodoma umejidhatiti kukabiliana na utoro wa wanafunzi shuleni kupitia maazimio yaliyowekwa kwa mwaka 2023 kupitia kikao cha pili cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa kilichofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa jengo la Mkapa chini ya Mwenyekiti wake Mhe. Rosemary Senyamule, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma.

Katika kikao hicho, agenda ya elimu imejadiliwa kwa kina na kupewa msukumo madhubuti ikiwa ni miongoni mwa ajenda nane za kikao hicho kilichojadili masuala mbalimbali ya maendeleo ikiwemo bajeti ya Mkoa, Elimu, Afya, Kilimo, Maji na Mazingira.  

Mkoa wa Dodoma unakabiliwa na changamoto kubwa ya utoro kwa wanafunzi wa Shule za Msingi na Sekondari huku sababu kubwa zikitajwa kuwa ni ukosefu wa chakula shuleni, Wazazi/Walezi kutoipa thamani stahiki elimu hivyo kutowajibika kwa malezi ya watoto wao, Viongozi wa Vijiji kushindwa kutimiza wajibu wao wa kudhibiti utoro shuleni na umbali mrefu wa kwenda na kurudi.

Akizungumza katika kikao hicho, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule amesema licha ya changamoto hizo katika sekta ya elimu, Wilaya ya Bahi imefanikiwa kushika nafasi ya kumi kitaifa katika matokeo ya darasa la saba mwaka 2022.

“Naipongeza sana Halmashauri ya Bahi kwa kushika nafasi ya kumi kwa mpangilio wa ufaulu wa Halmashauri kitaifa kwani wameifaharisha Mkoa mzima wa Dodoma. Natoa shime kwa Halmashauri nyingine kwenda kujifunza Bahi namna walivyofanya na kufanikiwa kuingia kwenye kumi bora za kitaifa. Pia tukafanye kazi kubwa kuhakikisha watoro wanarudi shuleni mwaka 2023” Amesema Mheshimiwa Senyamule.

Kwa upande wake, Katibu Tawala Mkoa Dkt. Fatuma Mganga naye ametoa rai kwa Wakurugenzi wa Halmashauri za Mkoa wa Dodoma kutoa msukumo kwa walimu kufundisha kwa bidii kwa lengo la kuongeza kiwango cha ufaulu.

Akitoa maoni yake juu ya maazimio ya mwaka 2023, Afisa Elimu Mkoa Bw. Gift Kyando amesema “Mwaka ujao tunaazimia wanafunzi wote watakaomaliza elimu ya msingi kurudi mapema shuleni kwa ajili ya kujiandaa na masomo ya kidato cha kwanza tofauti na ilivyokua mwaka huu kwani mitihani ilichelewa badala ya kufanyika mwezi Septemba imefanyika mwezi Oktoba ila mwakani itafanyika kama kawaida mwezi Septemba”

Katika kikao hicho Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule ameziagiza Halmashauri kuongeze kasi ya kukusanya mapato na kutoa asilimia kumi. “Naziagiza Halmashauri zote kwa kushirikiana na wadau kuendelee kutengeneza madawati ili kupunguza upungufu uliopo, Halmashauri zikamilishe usimamizi wa sheria ndogondogo za upatikanaji wa chakula shuleni pamoja na kudhibiti utoro, kila shule itenge eneo la kuzalishia chakula kwa wanafunzi, vyuo vya ufundi viimarishwe” Alisisitiza Mhe. Senyamule.

MWISHO

Matangazo

  • "WANANCHI JITOKEZENI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU 2025" - RC SENYAMULE February 17, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATANZANIA WATAKIWA KUILINDA NA KUIDUMISHA AMANI NI KURUHUSU MAENDELEO NCHINI

    May 15, 2025
  • MKURUGENZI WA ‘WATER FOR PEOPLE ‘ AMTEMBELEA RAS MMUYA

    May 16, 2025
  • WANAFUNZI KIDATO CHA SITA WAASWA SAFARI YA ELIMU BADO NI NDEFU

    May 17, 2025
  • RC SENYAMULE AZUNGUMZA NA MAKUNDI MBALIMBALI MKOANI KWAKE

    May 15, 2025
  • Tazama Zote

Video

RC SENYAMULE AKIZUNGUMZA KWENYE UZINDUZI WA SERA YA ELIMU NA MAFUNZO YA MWAKA 2014 TOLEO LA 2023.
Video Nyinginezo

Kurasa za Karibu

  • Speeches
  • mission and vision
  • Photo Gallery
  • Videos
  • Press Releases
  • Organization Structure
  • Reports
  • Client Service Charter
  • Acts

Tovuti Muhimu

  • PO-RALG
  • Public Service Management
  • Parliament of Tanzania
  • UDOM
  • Government Portal
  • Prime Minister's Office Website

World Visitors Tracker

world map hits counter

Rejesta ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Jengo la Mkapa (Mkapa House) Barabara ya Hospitali ya Mkoa

    Anuani ya Posta: 914 DODOMA

    Simu: +255 26 232 4343/232

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@dodoma.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya eneo

Hakimiliki©2016 GWF . Haki zote zimehifadhiwa.