• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Ofisi |
    • Malalamiko |
    • eoffice |
Dodoma Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Taasisi
      • Huduma Zetu
    • Huduma Zetu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Seksheni
      • Administration and Human Resource Management Section
      • Planning and Coordination
      • Infrastructure section
      • Management Monitoring and Inspection section;
      • Education and vocational Training section
      • Economic and productive sectors section;
      • Health, Social welfare and Nutrition services section
      • Industry, Trade and Investment section
    • Vitengo
      • Information Communication Technology (lcT) and Statistics
      • Government Communication Unit
      • Finance and Accounts unit;
      • Internal Audit unit
      • Legal services unit;
      • Procurement Management unit;
  • Wilaya
    • Bahi
    • Chamwino
    • Kongwa
    • Mpwapwa
    • Kondoa
    • Dodoma Mjini
    • Chemba
  • Mamlaka za Serikali za mitaa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bahi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chemba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa
    • Halmashauri ya Wilaya Mpwapwa
    • Halmashauri ya Mji Kondoa
    • The City Council of Dodoma (CCD)
  • Uwekezaji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Habari kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

KILELE CHA MAADHIMISHO YA MUUNGANO WA TANZANIA ; MSISITIZO WATOLEWA JUU YA ULINZI WA MUUNGANO

Imetumwa : April 26th, 2025

Na. Hellen M. Minja,

       Habari - DODOMA RS

Ikiwa ni kilele cha Maadhimisho ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar Aprili 26, 2025 ambayo yamekwenda sanjari na hitimisho la ziara ya siku nne (4) ya Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Ndugu Stephen Wasira katika Mkoa wa Dodoma, ametembelea miradi kadhaa ya maendeleo katika Halmashauri za Chemba, Kondoa na Kondoa Mji sambamba na kuongea na wananchi kwenye Halmashauri hizo.

Katika kilele cha Maadhimisho hayo, Ndugu Wasira ameendelea kusisitiza juu ya kutunza Muungano wetu ambao waasisi wake Hayati Mwl. Nyerere, Rais wa kwanza wa Tanganyika na Hayati Abeid Karume, Rais wa kwanza wa Zanzibar waliupigania na kuzaliwa nchi ya Tanzania kwa ajili ya kutunza Amani na maendeleo ya vizazi vyote.

"Kuwa na nchi mbili kama hazielewani, matatizo ya kiusalama ni makubwa sana, moja ya sababu zilizofanya tukaungana ni kuweka nguvu ya pamoja kwa ajili ya kuweka amani ambayo ndio msingi wa Maendeleo yote mnayoyaona na tumeungana kwa sababu ya kuweka maendeleo ya kizazi cha wakati ule, cha sasa na vinavyokuja" Ndugu Wasira.

Aidha, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dodoma Alhaji Adam Kimbisa amesema, Rais wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameleta miradi mingi ya elimu, Afya na maji kwenye Halmashauri za Chemba na Kondoa ikiwa ni katika kutimiza wajibu wake kwa wananchi hao hivyo wanapaswa kuonesha shukrani zao kwake.

Hata hivyo, Mkuu wa Wilaya ya Kondoa Mhe. Fatma Nyangasa, amesema "Muungano umeendelea kuwa Tunu katika Taifa letu na katika kipindi cha miaka minne ya Mhe. Dkt. Samia, Wilaya yetu imepokea na kutumia jumla ya shilingi Bilioni 71.9 katika maeneo mbalimbali ya maendeleo katika Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa na Halmashauri ya Mji Kondoa".

Katika Halmashauri ya Wilaya ya Chemba, Ndugu Wasira ametembelea Mradi wa Ujenzi wa shule maalumu ya wavulana ya Kanda inayojengwa Chemba kwa gharama ya shilingi Bilioni 4.1, kupitia Mpango wa kuboresha Elimu Sekondari (SEQUIP) ikiwa na majengo 38 na unatarajiwa kupunguza changamoto za Elimu kwa wanafunzi 960 wa Kanda ya Kati kwa ngazi za O- level na A-level.

Akiwa Wilaya ya Kondoa, alitembelea Mradi wa Hospitali ya Wilaya ambayo ilianza mwaka 2021 kwa gharama ya shilingi Bilioni 6.5 lakini mpaka Sasa Halmashauri imepokea Bilioni 3.5. Hospitali hiyo inahudumia zaidi ya watu 250,000 wa ndani na nje ya Wilaya hiyo. Mradi mwingine ambao pia uliwekwa jiwe la msingi ni Ujenzi wa shule ya Sekondari ya Kata ya Suruke ambao umegharimu kiasi cha shilingi Milioni 544.2



#dodomafahariyawatanzania

#keroyakowajibuwangu

#mtiwangubirthdayyangu

#karibumwengewauhuru2025mkoawadodoma

#miaka61yamuunganowatanzania2025

Matangazo

  • "WANANCHI JITOKEZENI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU 2025" - RC SENYAMULE February 17, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATANZANIA WATAKIWA KUILINDA NA KUIDUMISHA AMANI NI KURUHUSU MAENDELEO NCHINI

    May 15, 2025
  • MKURUGENZI WA ‘WATER FOR PEOPLE ‘ AMTEMBELEA RAS MMUYA

    May 16, 2025
  • WANAFUNZI KIDATO CHA SITA WAASWA SAFARI YA ELIMU BADO NI NDEFU

    May 17, 2025
  • RC SENYAMULE AZUNGUMZA NA MAKUNDI MBALIMBALI MKOANI KWAKE

    May 15, 2025
  • Tazama Zote

Video

RC SENYAMULE AKIZUNGUMZA KWENYE UZINDUZI WA SERA YA ELIMU NA MAFUNZO YA MWAKA 2014 TOLEO LA 2023.
Video Nyinginezo

Kurasa za Karibu

  • Speeches
  • mission and vision
  • Photo Gallery
  • Videos
  • Press Releases
  • Organization Structure
  • Reports
  • Client Service Charter
  • Acts

Tovuti Muhimu

  • PO-RALG
  • Public Service Management
  • Parliament of Tanzania
  • UDOM
  • Government Portal
  • Prime Minister's Office Website

World Visitors Tracker

world map hits counter

Rejesta ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Jengo la Mkapa (Mkapa House) Barabara ya Hospitali ya Mkoa

    Anuani ya Posta: 914 DODOMA

    Simu: +255 26 232 4343/232

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@dodoma.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya eneo

Hakimiliki©2016 GWF . Haki zote zimehifadhiwa.