• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Ofisi |
    • Malalamiko |
    • eoffice |
Dodoma Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Taasisi
      • Huduma Zetu
    • Huduma Zetu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Seksheni
      • Administration and Human Resource Management Section
      • Planning and Coordination
      • Infrastructure section
      • Management Monitoring and Inspection section;
      • Education and vocational Training section
      • Economic and productive sectors section;
      • Health, Social welfare and Nutrition services section
      • Industry, Trade and Investment section
    • Vitengo
      • Information Communication Technology (lcT) and Statistics
      • Government Communication Unit
      • Finance and Accounts unit;
      • Internal Audit unit
      • Legal services unit;
      • Procurement Management unit;
  • Wilaya
    • Bahi
    • Chamwino
    • Kongwa
    • Mpwapwa
    • Kondoa
    • Dodoma Mjini
    • Chemba
  • Mamlaka za Serikali za mitaa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bahi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chemba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa
    • Halmashauri ya Wilaya Mpwapwa
    • Halmashauri ya Mji Kondoa
    • The City Council of Dodoma (CCD)
  • Uwekezaji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Habari kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MAKUTANO YA BARABARA YA KONGWA - MPWAPWA KUJENGWA

Imetumwa : December 20th, 2023

Bodi ya Barabara Mkoa wa Dodoma leo Desemba 20, 2023 imefanya kikao chake cha kwanza mwaka 2023/24 kuwasilisha, kujadili na kushauri juu ya utekelezaji wa miradi ya Barabara za Mkoa kwa kipindi cha Julai hadi Novemba. Kikao hicho kilichoongozwa na Mwenyekiti wake Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule, kimefanyika kwenye ukumbi wa ofisi ya Mkoa jengo la Mkapa Jijini Dodoma 

Katika kikao hicho, Mwenyekiti amewasilisha taarifa ya bajeti ya jumla ya Mkoa kwenye ujenzi wa miundombinu ya Barabara na kuwataka wajumbe kwa niaba ya wananchi kufanya maendeleo ili kuinua Uchumi kulingana na maendeleo yaliyopatikana.

"Mkoa umepata jumla ya shilingi Bilioni 230.29 kutekeleza miradi ya Barabara kwa kipindi cha miaka mitatu ambapo TANROADS wamewezeshwa kutengeneza Barabara zenye jumla ya urefu wa Km 9248.12, TARURA wamewezeshwa kutengeneza Barabara zenye urefu wa jumla ya Km 7540.9 ambapo jumla wote wamepatiwa kiasi cha Shilingi Bilioni 593 na Milioni 69.


" Utekelezaji huu wa miradi ya Barabara pamoja na miradi mingine ya Kimkakati inayotekelezwa hapa Dodoma tuifanye ifanane na matokeo yanayotarajiwa, uwepo wa barabara hizi uendane kukua kwa Uchumi wa wananchi kwani Serikali imewekeza ili kuwainua wananchi wake" Amesema Mhe. Senyamule

Awali akifungua kikao hicho, Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma Bw. Ally Gugu, amezungumzia lengo na kazi za bodi ya Barabara ya Mkoa.

"Bodi ya Barabara ya Mkoa ina kazi ya kushauri na kutoa maelekezo juu ya maendeleo ya Barabara, kutekeleza miradi ya Barabara inayoletwa na Serikali, kupokea ushauri kuhusu miradi ya Barabara za Mkoa na Halmashauri pamoja na kutekeleza maelekezo yanayotolewa na Waziri mwenye dhamana" Amesema Bw. Gugu.

Kikao kimefikia maazimio kadhaa yakiwemo TANROADS, TARURA kwa kushirikiana na Halmashauri waendelee kuchukua tahadhari juu ya mvua zinazoendelea kunyesha ili kuepuka madhara kwa Barabara, TANROADS na TARURA ziwasilishe jumla ya fidia zinazodaiwa na wananchi wanaopitiwa na miradi ya Barabara na ujenzi wa Barabara ya makutano ya Kongwa- Mpwapwa ukamilike huku ahadi ya kuanzia Mpwapwa itekelezwe.

Mkoa wa Dodoma una mtandao wa Barabara wenye urefu wa jumla wa Km 9248.12 ambao upo chini ya Wakala wa Barabara Nchini TANROADS pamoja na Wakala wa Barabara za Mijini na vijijini TARURA ambao kwa kipindi chote cha miaka mitatu wamekua wakitekeleza miradi ya kimkakati ndani ya Mkoa ikiwemo ujenzi wa Barabara za mzunguko wa nje pamoja na Mradi wa ujenzi wa kiwanja cha ndege cha Kimataifa Msalato.













ReplyForward






Matangazo

  • "WANANCHI JITOKEZENI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU 2025" - RC SENYAMULE February 17, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATANZANIA WATAKIWA KUILINDA NA KUIDUMISHA AMANI NI KURUHUSU MAENDELEO NCHINI

    May 15, 2025
  • MKURUGENZI WA ‘WATER FOR PEOPLE ‘ AMTEMBELEA RAS MMUYA

    May 16, 2025
  • WANAFUNZI KIDATO CHA SITA WAASWA SAFARI YA ELIMU BADO NI NDEFU

    May 17, 2025
  • RC SENYAMULE AZUNGUMZA NA MAKUNDI MBALIMBALI MKOANI KWAKE

    May 15, 2025
  • Tazama Zote

Video

RC SENYAMULE AKIZUNGUMZA KWENYE UZINDUZI WA SERA YA ELIMU NA MAFUNZO YA MWAKA 2014 TOLEO LA 2023.
Video Nyinginezo

Kurasa za Karibu

  • Speeches
  • mission and vision
  • Photo Gallery
  • Videos
  • Press Releases
  • Organization Structure
  • Reports
  • Client Service Charter
  • Acts

Tovuti Muhimu

  • PO-RALG
  • Public Service Management
  • Parliament of Tanzania
  • UDOM
  • Government Portal
  • Prime Minister's Office Website

World Visitors Tracker

world map hits counter

Rejesta ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Jengo la Mkapa (Mkapa House) Barabara ya Hospitali ya Mkoa

    Anuani ya Posta: 914 DODOMA

    Simu: +255 26 232 4343/232

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@dodoma.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya eneo

Hakimiliki©2016 GWF . Haki zote zimehifadhiwa.