• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Ofisi |
    • Malalamiko |
    • eoffice |
Dodoma Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Taasisi
      • Huduma Zetu
    • Huduma Zetu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Seksheni
      • Administration and Human Resource Management Section
      • Planning and Coordination
      • Infrastructure section
      • Management Monitoring and Inspection section;
      • Education and vocational Training section
      • Economic and productive sectors section;
      • Health, Social welfare and Nutrition services section
      • Industry, Trade and Investment section
    • Vitengo
      • Information Communication Technology (lcT) and Statistics
      • Government Communication Unit
      • Finance and Accounts unit;
      • Internal Audit unit
      • Legal services unit;
      • Procurement Management unit;
  • Wilaya
    • Bahi
    • Chamwino
    • Kongwa
    • Mpwapwa
    • Kondoa
    • Dodoma Mjini
    • Chemba
  • Mamlaka za Serikali za mitaa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bahi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chemba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa
    • Halmashauri ya Wilaya Mpwapwa
    • Halmashauri ya Mji Kondoa
    • The City Council of Dodoma (CCD)
  • Uwekezaji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Habari kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RAS-Dodoma- Wakumbukeni Idara za Elimu katika PlanRep Mpya

Imetumwa : August 29th, 2017

Serikali mkoani hapa imesema ili mpango wa PlanRep uweze kufanikiwa kwa ufasaha hakuna budi kuzijumuisha idara za Elimu katika mafunzo yanayoendelea mkoani Dodoma yanayo wajumuisha wataalam wa mipango pamoja na afya kutoka mikoa mitano ya Tanga, Tabora, Manyara, Singida na wenyeji Dodoma kwa ajili ya maandalizi ya bajeti kwakutumia mfumo mpya wa PlanRep na FFARS.

Akifungua mafunzo ya siku nane mkoani hapa, Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma, Bibi Rehema Madenge, amesema moja ya vitu vilivyokuwa vikikwamisha masuala ya bajeti ni pamoja na kutokuwa na takwimu sahihi huku akinyooshea kidole takwimu za idara za elimu.

“Ninatamani sana takwimu za elimu ziwe sahihi hasa katika uwasilishaji wa taarifa za mitihani ili ziweze kuendana na idadi ya wanafunzi na fedha zinazo ombwa, kuepusha madudu yanayo wasilishwa” alisema madange na kuongeza kuwa katika sekta ya elimu ndipo kuna sarakasi ambazo hata mruka sarakasi mwenyewe hata yeye hamjui.

Madenge ambaye kwa taaluma ni Mchumi na aliyeshughulika na kuratibu shughuli za bajeti kwa muda mrefu, amesema ili mipango iweze kuendana na mahitaji suala la kuwa na takwimu sahihi haliepukiki na kuamini kuwa chini ya PlanRep mpya itakuwa mwarobaini katika kutatua changamoto hizo.

Madenge amesema mfumo wa PlanRep ulioboreshwa pia unaenda kutumika kuanzia ngazi ya msingi yaani vituo vyetu vya kutolea huduma ambapo utawezesha kuandaa mipango na bajeti kutokana na vipaumbele na mahitaji ya wananchi ambao ndio waathirika.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa mifumo ya TEHAMA wa PS3, Desderi Wangaa, amesema, PlanRep mpya iliyoboreshwa imefanyia kazi changamoto kwa kuhakikisha kwamba mipango na bajeti unaingizwa kwa kila mtoa huduma, na unaingiza namba za utambulisho kwa kila mtoa huduma mmoja mmoja kwa kila sekta lakini pia mfumo huu umeweka nafasi ya kila mtoa huduma kuainisha matokeo yanayotegemewa (Service Outputs).

Awali akitoa maelezo ya utangulizi, Mkurugenzi wa TEHAMA wa OR-TAMISEMI, Erick Kitali, alisema mfumo umezingatia mahitaji ya idara zote za mamlaka za serikali za mitaa na ambao ni fungamanifu unaotumia muda mfupi kukamilisha kazi za uratibu wa bajeti na taarifa za hesabu toka vituo vya huduma.

“Kutokana na kuwa fungamanifu hatutegemei kuona Serikali za Mitaa zikikwama katika uandaaji wa bajeti, na tuna uhakika na ufanisi wa hali ya juu katika kazi hii usahihi unaotakiwa” alisema Erick na kuongeza (Efficient and Effective)

Awali akimkaribisha Katibu Tawala wa Mkoa, Mkurugenzi wa mamalaka za serikali za Mitaa Beatrice Kimoleta, alisema kuwa na mfumo ni jambo moja na utendaji ni suala linguine hivyo suala la kujituma katika kuhakikisha mifumo inafanya kazi vema kila mmoja lazima awiwe katika utendaji wake.

“Tulitumia muda mwingi katika kuandaa bajeti na muda mfupi ukatumika katika kusimamia lakini katika PlanRep hii mpya mtaona muda wa uandaaji bajeti utakuwa utakuwa mfupi na muda mwingi utatumika katika suala la ufatiliaji na usimamizi”. Rai yangu niwasihi sote tuwe makini wakati wote wa mafunzo ili tukitoka hapa basi mipango yetu iwe yenye kuzingatia mahitaji.

PS3 kwakushirikiana na OR-TAMISEMI tayari wametoa mafunzo kwa mikoa na Halmashauri zote nchini na katika awamu hii ya mwisho inahusisha wataalamu kutoka mikoa ya Tanga, Tabora, Singida Manyara na Dodoma ambayo ni mwenyeji.

Aidha uzinduzi wa PlanRep mpya utafanyika 5 Septemba, 2017 na Mgeni Rasmi anatazamiwa kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Majaliwa Kassimu Majaliwa (MB).

Matangazo

  • "WANANCHI JITOKEZENI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU 2025" - RC SENYAMULE February 17, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATANZANIA WATAKIWA KUILINDA NA KUIDUMISHA AMANI NI KURUHUSU MAENDELEO NCHINI

    May 15, 2025
  • MKURUGENZI WA ‘WATER FOR PEOPLE ‘ AMTEMBELEA RAS MMUYA

    May 16, 2025
  • WANAFUNZI KIDATO CHA SITA WAASWA SAFARI YA ELIMU BADO NI NDEFU

    May 17, 2025
  • RC SENYAMULE AZUNGUMZA NA MAKUNDI MBALIMBALI MKOANI KWAKE

    May 15, 2025
  • Tazama Zote

Video

RC SENYAMULE AKIZUNGUMZA KWENYE UZINDUZI WA SERA YA ELIMU NA MAFUNZO YA MWAKA 2014 TOLEO LA 2023.
Video Nyinginezo

Kurasa za Karibu

  • Speeches
  • mission and vision
  • Photo Gallery
  • Videos
  • Press Releases
  • Organization Structure
  • Reports
  • Client Service Charter
  • Acts

Tovuti Muhimu

  • PO-RALG
  • Public Service Management
  • Parliament of Tanzania
  • UDOM
  • Government Portal
  • Prime Minister's Office Website

World Visitors Tracker

world map hits counter

Rejesta ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Jengo la Mkapa (Mkapa House) Barabara ya Hospitali ya Mkoa

    Anuani ya Posta: 914 DODOMA

    Simu: +255 26 232 4343/232

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@dodoma.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya eneo

Hakimiliki©2016 GWF . Haki zote zimehifadhiwa.