• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Ofisi |
    • Malalamiko |
    • eoffice |
Dodoma Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Taasisi
      • Huduma Zetu
    • Huduma Zetu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Seksheni
      • Administration and Human Resource Management Section
      • Planning and Coordination
      • Infrastructure section
      • Management Monitoring and Inspection section;
      • Education and vocational Training section
      • Economic and productive sectors section;
      • Health, Social welfare and Nutrition services section
      • Industry, Trade and Investment section
    • Vitengo
      • Information Communication Technology (lcT) and Statistics
      • Government Communication Unit
      • Finance and Accounts unit;
      • Internal Audit unit
      • Legal services unit;
      • Procurement Management unit;
  • Wilaya
    • Bahi
    • Chamwino
    • Kongwa
    • Mpwapwa
    • Kondoa
    • Dodoma Mjini
    • Chemba
  • Mamlaka za Serikali za mitaa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bahi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chemba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa
    • Halmashauri ya Wilaya Mpwapwa
    • Halmashauri ya Mji Kondoa
    • The City Council of Dodoma (CCD)
  • Uwekezaji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Habari kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC SENYAMULE NA STAMICO WASHIRIKI CHAKULA CHA PAMOJA SAMARIA - HOMBOLO

Imetumwa : December 24th, 2024

Na. Hellen M. Minja,

       Habari – DODOMA RS

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule, Disemba 23, 2024, alipata fursa ya kushiriki chakula cha pamoja na kundi la wazee wenye ugonjwa wa ukoma wanaoishi katika eneo la Samaria katika Mtaa wa Kolimba, Kata ya Hombolo Bwawani, Jijini Dodoma

Chakula hicho cha pamoja kilichoambatana na ugawaji wa mahitaji mbalimbali ya muhimu, kiliandaliwa na Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) kupitia Mkurugenzi Mtendaji wake kwa kushirikiana na kikundi cha Wanawake na Samia Mkoa wa Dodoma ambao kwa pamoja wamejitolea kuwa walezi wa wazee.

Akizungumza na wazee hao, Mhe. Senyamule amesema kuwa kundi hilo ni la muhimu katika jamii kama walivyo watu wengine hivyo jamii inapaswa kulipa thamani na kushirikiana nalo katika shughuli nyanja zote stahiki.

“Leo tumekuja kula na nyinyi na kuwaonesha hii Tanzania ni ya kwenu sote na nyinyi na sisi ni watu tunaofanana kwa maana ya mahitaji ya kibinadamu. Nyinyi ni watu wa thamani na pekee. Mhe. Rais anatamani watu wote wapate haki sawa kama binadamu, waishi kwa furaha na amani” Amesema Mhe. Senyamule.

Aidha, Mhe. Senyamule ameagiza kitengo cha Ustawi wa Jamii kuandaa programu kwa wanasamaria kupatiwa elimu ya uzalishaji na ujasiriamali ili waweze kujikwamua bila kutegemea misaada kwani Mhe. Rais ameanzisha programu nyingi za kusaidia makundi maalum.

Hata hivyo, Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) Dkt. Venance Mwase, aliongelea umuhimu wa jukumu la kusaidia wenye mahitaji ili kuleta usawa katika jamii.

“Aliyetuumba hakuchagua kupeleka wengine wakateseka na wengine wakafurahie, dhumuni la Mungu lilikua tuwe na fursa sawa lakini mwisho wake tuwe na furaha na amani. Sisi tuna wajibu wa kuwaangalia wale ambao wapo kwenye changamoto angalau waje kwenye furaha na amani.

Naye, Mwenyekiti wa Wanawake na Samia Mkoa wa Dodoma Bi. Fatma Madidi alieleza namna alivyolifahamu eneo hilo na kugundua uwepo wa wahitaji kwani walipofika hapo walikuta hali ya maisha sio ya kuridhisha hivyo walishirikisha Serikali ya Mkoa na Shirika la STAMICO na kuandaa utaratibu wa kuwashika mkono wazee hao hasa kwa kutoa mahitaji ya chakula, vifaa tiba na dawa.

Kijiji cha Samaria linakaliwa na wakazi takribani 180 likiwa na Kaya 23 ambazo zinaishi kwa kutegemea misaada kutoka kwa wahisani kutokana na kukosa nguvu kazi ya kutosha kutokana na ulemavu walionao uliotokana na ugojwa wa ukoma hivyo, tangu kujitokeza kwa STAMICO, limekua msaada kwao kwa mahitaji muhimu.






#dodomafahariyawatanzania                                 #keroyakowajibuwangu #mtiwangubirthdayyangu

Matangazo

  • "WANANCHI JITOKEZENI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU 2025" - RC SENYAMULE February 17, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATANZANIA WATAKIWA KUILINDA NA KUIDUMISHA AMANI NI KURUHUSU MAENDELEO NCHINI

    May 15, 2025
  • MKURUGENZI WA ‘WATER FOR PEOPLE ‘ AMTEMBELEA RAS MMUYA

    May 16, 2025
  • WANAFUNZI KIDATO CHA SITA WAASWA SAFARI YA ELIMU BADO NI NDEFU

    May 17, 2025
  • RC SENYAMULE AZUNGUMZA NA MAKUNDI MBALIMBALI MKOANI KWAKE

    May 15, 2025
  • Tazama Zote

Video

RC SENYAMULE AKIZUNGUMZA KWENYE UZINDUZI WA SERA YA ELIMU NA MAFUNZO YA MWAKA 2014 TOLEO LA 2023.
Video Nyinginezo

Kurasa za Karibu

  • Speeches
  • mission and vision
  • Photo Gallery
  • Videos
  • Press Releases
  • Organization Structure
  • Reports
  • Client Service Charter
  • Acts

Tovuti Muhimu

  • PO-RALG
  • Public Service Management
  • Parliament of Tanzania
  • UDOM
  • Government Portal
  • Prime Minister's Office Website

World Visitors Tracker

world map hits counter

Rejesta ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Jengo la Mkapa (Mkapa House) Barabara ya Hospitali ya Mkoa

    Anuani ya Posta: 914 DODOMA

    Simu: +255 26 232 4343/232

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@dodoma.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya eneo

Hakimiliki©2016 GWF . Haki zote zimehifadhiwa.