• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Ofisi |
    • Malalamiko |
    • eoffice |
Dodoma Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Taasisi
      • Huduma Zetu
    • Huduma Zetu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Seksheni
      • Administration and Human Resource Management Section
      • Planning and Coordination
      • Infrastructure section
      • Management Monitoring and Inspection section;
      • Education and vocational Training section
      • Economic and productive sectors section;
      • Health, Social welfare and Nutrition services section
      • Industry, Trade and Investment section
    • Vitengo
      • Information Communication Technology (lcT) and Statistics
      • Government Communication Unit
      • Finance and Accounts unit;
      • Internal Audit unit
      • Legal services unit;
      • Procurement Management unit;
  • Wilaya
    • Bahi
    • Chamwino
    • Kongwa
    • Mpwapwa
    • Kondoa
    • Dodoma Mjini
    • Chemba
  • Mamlaka za Serikali za mitaa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bahi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chemba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa
    • Halmashauri ya Wilaya Mpwapwa
    • Halmashauri ya Mji Kondoa
    • The City Council of Dodoma (CCD)
  • Uwekezaji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Habari kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

TANROADS WATAKIWA KUTAFUTA NJIA MBADALA KWA WANANCHI WAKATI WA UJENZI WA DARAJA LA MORENA

Imetumwa : April 29th, 2025

Na. Hellen M. Minja

       Habari – DODOMA RS

Maelekezo yametolewa kwa Wakala wa Barabara nchini (TANROADS)Mkoa wa Dodoma ambao unasimamia Mradi wa upanuzi wa daraja la Morena, kutafuta njia mbadala itakayotumiwa na wananchi watakaohitaji huduma upande wa pili wa daraja baada ya barabara iliyokua ikiunganishwa na daraja hilo kufungwa kwa muda ili kupisha ujenzi.

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule ametoa maelekezo hayo leo Aprili 29, 2025 alipofanya ziara fupi ya kutembelea eneo hilo la mradi lililopo kwenye makutano ya barabara ya kuelekea Morena na Mkoa wa Morogoro (Shabiby) ili kujionea maendeleo ya ujenzi huo.

“Hapa mmepata mawazo ya kutafuta sehemu nyingine ambazo zinaweza kuwa ‘altenative’, muiwekee vibao ili mtu aone ana ‘option’ tofauti tofauti za kufika katika hilo eneo. Hilo lifanyeni, tarehe 1 tupate taarifa kuwa hawa wananchi wanapita wapi maeneo mengine ili kulifikia hili eneo”.

Awali Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mhe. Jabir Shekimweri amepongeza upanuzi wa daraja hilo kwani utamaliza changamoto ya mafuriko kwenye makazi ya watu kipindi cha mvua kubwa lakini pia litaondoa changamoto za kiafya kutokana na kuzaliana kwa mbu pindi maji ya mvua yanapotuama eneo hilo sambamba na magonjwa ya mlipuko.

Aidha, akitoa taarifa ya Mradi kwa Mhe. Senyamule, Meneja wa TANROADS Mkoa wa Dodoma Mhandisi Zuhura Amani, amesema utekelezaji wa Mradi huo umefikia 80% huku akitoa ahadi kwa wananchi kuwa pamoja na kuzingatia ubora, wataendelea kumhimiza Mkandarasi kukamilisha kazi hiyo mapema ili wananchi waone matunda yake.

Mradi huo ambao umefadhiliwa na Benki ya Dunia kwa gharama ya shilingi 1.5 unatarajiwa kukamilika Novemba 2025 na kwa sasa Mkandarasi amemaliza ujenzi wa daraja kubwa pamoja na makalavati madogo. Ujenzi wa barabara unganishi unatarajiwa kuendelea ndani ya siku 14 huku ukizalisha ajira 40 kwa wazawa.


#dodomafahariyawatanzania

#keroyakowajibuwangu

#mtiwangubirthdayyangu

Matangazo

  • "WANANCHI JITOKEZENI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU 2025" - RC SENYAMULE February 17, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATANZANIA WATAKIWA KUILINDA NA KUIDUMISHA AMANI NI KURUHUSU MAENDELEO NCHINI

    May 15, 2025
  • MKURUGENZI WA ‘WATER FOR PEOPLE ‘ AMTEMBELEA RAS MMUYA

    May 16, 2025
  • WANAFUNZI KIDATO CHA SITA WAASWA SAFARI YA ELIMU BADO NI NDEFU

    May 17, 2025
  • RC SENYAMULE AZUNGUMZA NA MAKUNDI MBALIMBALI MKOANI KWAKE

    May 15, 2025
  • Tazama Zote

Video

RC SENYAMULE AKIZUNGUMZA KWENYE UZINDUZI WA SERA YA ELIMU NA MAFUNZO YA MWAKA 2014 TOLEO LA 2023.
Video Nyinginezo

Kurasa za Karibu

  • Speeches
  • mission and vision
  • Photo Gallery
  • Videos
  • Press Releases
  • Organization Structure
  • Reports
  • Client Service Charter
  • Acts

Tovuti Muhimu

  • PO-RALG
  • Public Service Management
  • Parliament of Tanzania
  • UDOM
  • Government Portal
  • Prime Minister's Office Website

World Visitors Tracker

world map hits counter

Rejesta ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Jengo la Mkapa (Mkapa House) Barabara ya Hospitali ya Mkoa

    Anuani ya Posta: 914 DODOMA

    Simu: +255 26 232 4343/232

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@dodoma.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya eneo

Hakimiliki©2016 GWF . Haki zote zimehifadhiwa.