• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Ofisi |
    • Malalamiko |
    • eoffice |
Dodoma Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Taasisi
      • Huduma Zetu
    • Huduma Zetu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Seksheni
      • Administration and Human Resource Management Section
      • Planning and Coordination
      • Infrastructure section
      • Management Monitoring and Inspection section;
      • Education and vocational Training section
      • Economic and productive sectors section;
      • Health, Social welfare and Nutrition services section
      • Industry, Trade and Investment section
    • Vitengo
      • Information Communication Technology (lcT) and Statistics
      • Government Communication Unit
      • Finance and Accounts unit;
      • Internal Audit unit
      • Legal services unit;
      • Procurement Management unit;
  • Wilaya
    • Bahi
    • Chamwino
    • Kongwa
    • Mpwapwa
    • Kondoa
    • Dodoma Mjini
    • Chemba
  • Mamlaka za Serikali za mitaa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bahi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chemba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa
    • Halmashauri ya Wilaya Mpwapwa
    • Halmashauri ya Mji Kondoa
    • The City Council of Dodoma (CCD)
  • Uwekezaji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Habari kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

TIMU YA ITIFAKI KUTAMBULIWA NA VIONGOZI WAO

Imetumwa : December 15th, 2023

Vijana wanaosimamia Itifaki kwenye dhifa mbalimbali za Kiserikali na hata za Taasisi binafsi wametakiwa kujitambulisha kwenye ofisi zao ili waweze kutambulika na kutumika kwa ajili ya kusimamia taratibu na ustaarabu wakati wa shughuli tofauti tofauti zinazotekelezwa Mkoa wa Dodoma na Mikoa mingine pia pindi huduma yao inapohitajika.

Hayo yameelezwa Leo Desemba 15, 2023 na Mhe. Rosemary Senyamule wakati akifungua mafunzo siku tatu yanayotolewa kwa timu ya huduma ya Itifaki yanayofanyika kwenye ukumbi wa Chuo kikuu cha Mipango kilichopo Jijini Dodoma.

"Nimetiwa Moyo na vijana hawa kwa kuweza kuhudhuria mafunzo haya. Dodoma ikiwa ndio makao makuu ya nchi, Kuna takribani ofisi 100 za Serikali hapa hali inayopelekea kuwa na matukio mengi yenye uhitaji wa huduma hii. Kumekua na changamoto kwenye suala la usimamizi wa Itifaki kwenye dhifa mbalimbali.

"Mafunzo haya yatawasaidia huko muendapo na nitoe Wito kwenu, baada ya mafunzo haya, mukajitambulishe kwenye ofisi zenu ili mukihitajika muweze kutumika. Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, anahimiza kufanyika mikutano mbalimbali hali inayopelekea kuhitajika watu wenye sifa kama zenu. Mafunzo yenu yatakua na faida kubwa kwa Dodoma" Amesema Mhe. Senyamule.

Awali akitoa hotuba fupi ya Timu hii, Mwenyekiti wake Bw. Hussein Aboubakar Hussein, amesema vijana hawa wanashauku kubwa ya kufanya maendeleo kwenye sekta ya kilimo hivyo ametoa ombi kwa Mhe. Mkuu wa Mkoa kupatiwa shamba la Hekari 50 na Mhe. Senyamule ameridhia ombi hilo na kuahidi kuwapatia kwa kuzingatia Mradi mkubwa wa Serikali wa BBT ulioanzishwa na Wizara ya Kilimo unaolenga vijana kujikita kwenye uwekezaji wa kilimo.

Pia timu hii imepata mafanikio kadhaa ikiwemo kutambulika na Mamlaka mbalimbali, kusimamia na kushiriki Itifaki wakati wa mbio za Mwenge, kupata usajili wa Kiserikali pamoja na kuandaa mradi wa kuwezesha watoto kwenda shule inayotarajiwa kuwa msaada kwa watoto ambao wanahitaji kwenda shule lakini wanakabiliwa na changamoto mbalimbali.

Timu ya Itifaki imesajiliwa tarehe 13 Machi 2023 kwa lengo kuu la kutoa huduma za kiitifaki na uendeshaji wa mikutano na dhifa mbalimbali ina washiriki 81 wakiwemo Maafisa Itifaki kutoka sehemu mbalimbali, waajiriwa na wasio waajiriwa kutoka Mikoa tofauti tofauti nchini.

Matangazo

  • "WANANCHI JITOKEZENI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU 2025" - RC SENYAMULE February 17, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATANZANIA WATAKIWA KUILINDA NA KUIDUMISHA AMANI NI KURUHUSU MAENDELEO NCHINI

    May 15, 2025
  • MKURUGENZI WA ‘WATER FOR PEOPLE ‘ AMTEMBELEA RAS MMUYA

    May 16, 2025
  • WANAFUNZI KIDATO CHA SITA WAASWA SAFARI YA ELIMU BADO NI NDEFU

    May 17, 2025
  • RC SENYAMULE AZUNGUMZA NA MAKUNDI MBALIMBALI MKOANI KWAKE

    May 15, 2025
  • Tazama Zote

Video

RC SENYAMULE AKIZUNGUMZA KWENYE UZINDUZI WA SERA YA ELIMU NA MAFUNZO YA MWAKA 2014 TOLEO LA 2023.
Video Nyinginezo

Kurasa za Karibu

  • Speeches
  • mission and vision
  • Photo Gallery
  • Videos
  • Press Releases
  • Organization Structure
  • Reports
  • Client Service Charter
  • Acts

Tovuti Muhimu

  • PO-RALG
  • Public Service Management
  • Parliament of Tanzania
  • UDOM
  • Government Portal
  • Prime Minister's Office Website

World Visitors Tracker

world map hits counter

Rejesta ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Jengo la Mkapa (Mkapa House) Barabara ya Hospitali ya Mkoa

    Anuani ya Posta: 914 DODOMA

    Simu: +255 26 232 4343/232

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@dodoma.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya eneo

Hakimiliki©2016 GWF . Haki zote zimehifadhiwa.