• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Ofisi |
    • Malalamiko |
    • eoffice |
Dodoma Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Taasisi
      • Huduma Zetu
    • Huduma Zetu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Seksheni
      • Administration and Human Resource Management Section
      • Planning and Coordination
      • Infrastructure section
      • Management Monitoring and Inspection section;
      • Education and vocational Training section
      • Economic and productive sectors section;
      • Health, Social welfare and Nutrition services section
      • Industry, Trade and Investment section
    • Vitengo
      • Information Communication Technology (lcT) and Statistics
      • Government Communication Unit
      • Finance and Accounts unit;
      • Internal Audit unit
      • Legal services unit;
      • Procurement Management unit;
  • Wilaya
    • Bahi
    • Chamwino
    • Kongwa
    • Mpwapwa
    • Kondoa
    • Dodoma Mjini
    • Chemba
  • Mamlaka za Serikali za mitaa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bahi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chemba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa
    • Halmashauri ya Wilaya Mpwapwa
    • Halmashauri ya Mji Kondoa
    • The City Council of Dodoma (CCD)
  • Uwekezaji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Habari kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

UZALENDO WAHITAJIKA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA SERIKALI

Imetumwa : October 30th, 2023


Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe Rosemary Senyamule, leo Oktoba 30, 2023, amehudhuria kama mgeni rasmi hafla ya utekelezaji wa Mradi wa uboreshaji wa miundombinu ya Miji Tanzania ikihusisha ushindani (TACTIC) kwa Mkoa wa Dodoma unaotekelezwa na Kampuni ya CHINA GEO ENGINEERING CORP chini ya Mhandisi Msimamizi HONG - IK CONSULTANT CO. LTD kwa kushirikiana na GAUZE- PRO CONSULT (T) LTD na G & Y ENGINEERING CONSULT PLC hafla ambayo imefanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma.

Mradi huo unaotekelezwa na Serikali kuu chini ya ufadhili wa Benki ya Dunia, una lengo la kuboresha miundombinu ya Barabara, madaraja, mitaro, majengo mbalimbali, vivuko vya barabara n.k pia una lengo la kujengeana uwezo kwa Taasisi tofauti tofauti.

Akizungumzia wakati wa hafla hiyo, Mhe. Senyamule amesema Dodoma ina hadhi ya Miji ya Kimataifa kutokana na vipimo vya hadhi hiyo hivyo miradi hii izingatie hadhi ya Jiji hili.

"Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ana maono na utashi mkubwa kwa Dodoma hivyo tunataka Jiji la Dodoma kuwa na hadhi ya Kimataifa kwani Mkoa huu umepimwa kwa asilimia 80 lakini tunataka kufikia asilimia 100. Dodoma haifananishwi na majiji mengine bali Miji mikubwa ulimwenguni hivyo, miradi hii ijengwe kwa hadhi hiyo na ubora huo wa Kimataifa. Nataka Mradi huu uwe moja ya miradi tunayopata taarifa yake kila mwezi" Mhe. Senyamule.

Hata hivyo, Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mhe. Jabir Shekimweri, amesisitiza uzalendo kwa wasimamizi wa mradi huu pia matumizi mazuri ya fedha kwani zinatoka moja kwa moja kutoka Benki ya Dunia.

"Mradi huu si wa Jiji pekee Bali na wadau ambao ni Taasisi za miundombinu. Hatuhitaji ucheleweshwaji wa kukamilika kwake kwani mradi unasimamiwa na Jiji lakini fedha inatoka Benki ya Dunia hivyo kusiwepo na minong'ono ya fulani anakula fedha kwani hakuna ambaye itapita mikononi mwake. Tutangulize uzalendo kwenye hii kazi, tunataka tuone thamani ya fedha na kukamilika kwa mradi kwa wakati" Mhe. Shekimweri

Aidha, Mbunge wa Jiji la Dodoma Mhe. Anthony Mavunde amebainisha kuwa Dodoma ni kati ya mikoa inayoongoza kwa kuwa na mtandao mrefu wa barabara unaofikia takribani Km 70 hivyo miradi hii itasaidia kuliboresha Jiji la Dodoma kwa hadhi yake ya Makao makuu ya nchi. Pia amesema, miradi hii inakwenda kuboresha upatikanaji wa huduma mbalimbali za kijamii. Ametoa Rai kwa viongozi kusimamia miradi hii kwa dhati ili wananchi waweze kushuhudia matokeo yake.

Mradi wa TACTIC ulisainiwa mara ya kwanza tarehe 13 Septemba 2023 chini ya Waziri wa TAMISEMI Mhe. Mohamed Mchengerwa ambapo unahusisha ujenzi wa miundombinu kwa awamu tatu ambapo awamu ya kwanza inahusisha ujenzi wa masoko, mitaro, vivuko, stendi za mabasi, n.k na mpaka sasa maeneo yote yatakayojengwa chini ya Mradi huu yameshafanyiwa usanifu na tayari mkandarasi yupo katika hatua ya maandalizi kwa kufikisha vifaa kwenye eneo la ujenzi . Mradi unagharimu kiasi cha Shilingi Bilioni 24 bila Kodi ya ongezeko la thamani ( VAT) na unatarajiwa kutumia kipindi cha miezi 15


Matangazo

  • "WANANCHI JITOKEZENI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU 2025" - RC SENYAMULE February 17, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATANZANIA WATAKIWA KUILINDA NA KUIDUMISHA AMANI NI KURUHUSU MAENDELEO NCHINI

    May 15, 2025
  • MKURUGENZI WA ‘WATER FOR PEOPLE ‘ AMTEMBELEA RAS MMUYA

    May 16, 2025
  • WANAFUNZI KIDATO CHA SITA WAASWA SAFARI YA ELIMU BADO NI NDEFU

    May 17, 2025
  • RC SENYAMULE AZUNGUMZA NA MAKUNDI MBALIMBALI MKOANI KWAKE

    May 15, 2025
  • Tazama Zote

Video

RC SENYAMULE AKIZUNGUMZA KWENYE UZINDUZI WA SERA YA ELIMU NA MAFUNZO YA MWAKA 2014 TOLEO LA 2023.
Video Nyinginezo

Kurasa za Karibu

  • Speeches
  • mission and vision
  • Photo Gallery
  • Videos
  • Press Releases
  • Organization Structure
  • Reports
  • Client Service Charter
  • Acts

Tovuti Muhimu

  • PO-RALG
  • Public Service Management
  • Parliament of Tanzania
  • UDOM
  • Government Portal
  • Prime Minister's Office Website

World Visitors Tracker

world map hits counter

Rejesta ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Jengo la Mkapa (Mkapa House) Barabara ya Hospitali ya Mkoa

    Anuani ya Posta: 914 DODOMA

    Simu: +255 26 232 4343/232

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@dodoma.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya eneo

Hakimiliki©2016 GWF . Haki zote zimehifadhiwa.