• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Ofisi |
    • Malalamiko |
    • eoffice |
Dodoma Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Taasisi
      • Huduma Zetu
    • Huduma Zetu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Seksheni
      • Administration and Human Resource Management Section
      • Planning and Coordination
      • Infrastructure section
      • Management Monitoring and Inspection section;
      • Education and vocational Training section
      • Economic and productive sectors section;
      • Health, Social welfare and Nutrition services section
      • Industry, Trade and Investment section
    • Vitengo
      • Information Communication Technology (lcT) and Statistics
      • Government Communication Unit
      • Finance and Accounts unit;
      • Internal Audit unit
      • Legal services unit;
      • Procurement Management unit;
  • Wilaya
    • Bahi
    • Chamwino
    • Kongwa
    • Mpwapwa
    • Kondoa
    • Dodoma Mjini
    • Chemba
  • Mamlaka za Serikali za mitaa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bahi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chemba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa
    • Halmashauri ya Wilaya Mpwapwa
    • Halmashauri ya Mji Kondoa
    • The City Council of Dodoma (CCD)
  • Uwekezaji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Habari kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WADAU WA MALEZI YA WATOTO WAKUTANA DODOMA

Imetumwa : September 14th, 2023



Wadau wanaoshughulika na malezi na makuzi ya watoto wametakiwa kushirikiana ili kufanikisha malengo ya Programu Jumuishi ya Malezi Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto (PJT -MMMAM) ili kupunguza udumavu na utapiamlo kwa watoto wa Mkoa wa Dodoma

Hayo yamebainishwa na Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma Bw. Ally Gugu wakati wa ufunguzi kikao cha wadau hao kutoka katika Halmashauri za Mkoa wa Dodoma kilichofanyika leo Septemba 14, 2023 katika ukumbi wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma kujadili afua mbalimbali za namna ya kuboresha malezi na makuzi ya watoto.

"Mradi huu unagusa maeneo tofauti tofauti ikiwemo lishe ya Mtoto, malezi kuanzia ujauzito hadi miaka 8 na fursa za ujifunzaji wa malezi ya awali ya Mtoto. Dodoma ina takribani wadau 410 wanaoshirikiana na Serikali katika kufanikisha program hii, hivyo ni muhimu kushirikiana kwani bado hatujafanya vizuri kama Mkoa kwenye takwimu za lishe kwa watoto" Amesema Bw. Gugu

Aidha, ameongeza kwa kuwaasa kina mama na walezi kuzingatia nafundisho ya lishe yanayotolewa na wataalamu kuanzia kipindi cha ujauzito hadi malezi ya Mtoto.

" Kwa kipindi cha 2022/2023 jumla ya kina mama / walezi 191,662 kati ya 200,981 walio na watoto wenye umri wa miezi 0 - 23 walipewa unasihi juu ya ulishaji wa watoto uliofanywa na watoa huduma ya afya sawa na asilimia 104.60 hii ninaonyesha ni kwa namna gani unapomlinda mtoto kwa kumpa lishe bora, itasaidia katika makuzi yake" Ameongeza Bw. Gugu.

Akizungumzia lengo kuu la kikao hicho, Mratibu wa Malezi na makuzi ya watoto Bi. Stella Matemu amesema,
" Lengo kuu la kikao hicho ni kuwatambua wadau pamoja na kujadili afua mbalimbali zinazopatikana kwenye mradi huu ulioazinduliwa rasmi mwaka 2021 kitaifa ambapo kwa Mkoa wa Dodoma ulizinduliwa Septemba 2022 ukihusisha maeneo matano ambayo yanahusiana na malezi na makuzi ya Mtoto kuanzia miaka 0 - 8 nayo ni Elimu, afya, lishe , malezi na mwitikio." Bi. Matemu

Hata hivyo, mwakilishi kutoka Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Wanawake, Watoto na Makundi maalumu Bw. Joel Mwakapala amesema kuwa asilimia 90 ya ubongo wa mtoto unakua akiwa katika umri wa miaka 0 hadi 8 huku akielezea namna program hii inavyoleta matokeo chanya kwa jamii.

" Uwepo wa program hii umesaidia kuboreshwa kwa mazingira wezeshi ya kufanya uratibu wenye ufanisi na pia mifumo ya utoaji huduma Jumuishi za MMMAM na uthibiti ubora imeimarishwa" Amesema Bw. Mwakapala.

MWISHOw

Matangazo

  • "WANANCHI JITOKEZENI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU 2025" - RC SENYAMULE February 17, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATANZANIA WATAKIWA KUILINDA NA KUIDUMISHA AMANI NI KURUHUSU MAENDELEO NCHINI

    May 15, 2025
  • MKURUGENZI WA ‘WATER FOR PEOPLE ‘ AMTEMBELEA RAS MMUYA

    May 16, 2025
  • WANAFUNZI KIDATO CHA SITA WAASWA SAFARI YA ELIMU BADO NI NDEFU

    May 17, 2025
  • RC SENYAMULE AZUNGUMZA NA MAKUNDI MBALIMBALI MKOANI KWAKE

    May 15, 2025
  • Tazama Zote

Video

RC SENYAMULE AKIZUNGUMZA KWENYE UZINDUZI WA SERA YA ELIMU NA MAFUNZO YA MWAKA 2014 TOLEO LA 2023.
Video Nyinginezo

Kurasa za Karibu

  • Speeches
  • mission and vision
  • Photo Gallery
  • Videos
  • Press Releases
  • Organization Structure
  • Reports
  • Client Service Charter
  • Acts

Tovuti Muhimu

  • PO-RALG
  • Public Service Management
  • Parliament of Tanzania
  • UDOM
  • Government Portal
  • Prime Minister's Office Website

World Visitors Tracker

world map hits counter

Rejesta ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Jengo la Mkapa (Mkapa House) Barabara ya Hospitali ya Mkoa

    Anuani ya Posta: 914 DODOMA

    Simu: +255 26 232 4343/232

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@dodoma.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya eneo

Hakimiliki©2016 GWF . Haki zote zimehifadhiwa.