• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Ofisi |
    • Malalamiko |
    • eoffice |
Dodoma Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Taasisi
      • Huduma Zetu
    • Huduma Zetu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Seksheni
      • Administration and Human Resource Management Section
      • Planning and Coordination
      • Infrastructure section
      • Management Monitoring and Inspection section;
      • Education and vocational Training section
      • Economic and productive sectors section;
      • Health, Social welfare and Nutrition services section
      • Industry, Trade and Investment section
    • Vitengo
      • Information Communication Technology (lcT) and Statistics
      • Government Communication Unit
      • Finance and Accounts unit;
      • Internal Audit unit
      • Legal services unit;
      • Procurement Management unit;
  • Wilaya
    • Bahi
    • Chamwino
    • Kongwa
    • Mpwapwa
    • Kondoa
    • Dodoma Mjini
    • Chemba
  • Mamlaka za Serikali za mitaa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bahi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chemba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa
    • Halmashauri ya Wilaya Mpwapwa
    • Halmashauri ya Mji Kondoa
    • The City Council of Dodoma (CCD)
  • Uwekezaji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Habari kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WANAWAKE NA SAMIA 3000 MKOA WA DODOMA KUPATA MAFUNZO VETA

Imetumwa : March 24th, 2025

Na. Hellen M. Minja,

       Habari – DODOMA RS


Chuo cha Mafunzo ya Ufundi Stadi(VETA) Mkoa wa Dodoma, kinatarajia kutoa mafunzo kwa kundi la ‘Wanawake na Samia’ wapatao 3000 linalounga mkono matamanio ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kuleta Usawa wa kijamii na kijinsia ambayo ni kufikia mwaka 2030, ifike 50 kwa 50 kwa kila kundi kupata haki sawa.


Hayo yamesemwa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule alipokua akifungua mafunzo mbalimbali ya muda mfupi kwa ajili ya kundi la Wanawake na Samia Mkoa wa Dodoma, zitakazotolewa kwa kundi hilo na Chuo cha Mafunzo ya Ufundi Stadi (Veta) tawi la Jijini  Dodoma.


“Mhe. Dkt Samia amekua akitamani kila kundi la Mtanzania lipate haki sawa ndio maana anasema hataachwa mtu nyuma awe ni mwanamke, mtu? mwenye ulemavu, mzee, kijana au mtoto. Anatamani Wanawake wa Tanzania washike uchumi sawa na wanaume, Makundi maalum ambayo yapo nyuma yashike uchumi sawa na makundi mengine”.


Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mhe. Jabir Shekimweri, amekipongeza Chuo cha VETA Dodoma kwa kuandaa mafunzo hayo ambayo kwa sehemu yake yatahusu utalii, ujasiriamali na maadili kwa kundi hilo ambalo linatunza heshima ya jina la Mhe. Dkt Samia na lipo Makao Makuu ya Nchi ambayo inazidi kukua na kujengeka.


Vilevile, Mkurugenzi Mkuu wa VETA CPA Anthony Mzee Kasore, amesema Chuo chake kinatoa mafunzo mbalimbali na eneo linalowekewa mkazo ni kuhakikisha wanawake wanaodahiliwa katika vyuo vya ufundi stadi wanaongezeka hadi kufikia 45% ambapo kwa sasa wapo asilimia 25 hadi 37 na wameanzisha programu za uwezeshaji wajasiriamali kwa akina mama ili kufikia lengo hilo.


Akizungumzia dhumuni la mafunzo hayo kwa kundi hilo, Mkuu wa VETA Dodoma Bw. Deodatus Orotha, amesema ni kuwapatia ujuzi wanawake wa Mkoa wa Dodoma ili waweze kutatua changamoto zao pamoja na familia lakini pia kuleta tija kwa Taifa. Amesema tayari wameshajisajili na mafunzo yataanza Machi 26, 2025 kwa muda wa wiki nne.


Nae, Mwenyekiti wa Wanawake na Samia Mkoa wa Dodoma Bi. Fatma Madidi amesema kuwa kundi lake linatoa shukrani kwa VETA kwa kukubali kutoa mafunzo hayo kwani kumsomesha mwanamke ni kuisomesha jamii na kupitia mafunzo hayo, watakwenda kutoa Wataalamu watakaosaidia Mkoa wa Dodoma, Tanzania na Dunia kwa ujumla.


Mafunzo hayo ambayo yatagharamiwa na VETA Dodoma, yanatarajiwa kuwanufaisha wanawake 3000 wa kundi hilo ambao watasoma kwa awamu ya wanawake 250 mpaka watakapokamilika ambapo wazo la kufanya mafunzo hayo lilitolewa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule





#dodomafahariyawatanzania

#keroyakowajibuwangu#mtiwangubirthdayyangu

Matangazo

  • "WANANCHI JITOKEZENI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU 2025" - RC SENYAMULE February 17, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATANZANIA WATAKIWA KUILINDA NA KUIDUMISHA AMANI NI KURUHUSU MAENDELEO NCHINI

    May 15, 2025
  • MKURUGENZI WA ‘WATER FOR PEOPLE ‘ AMTEMBELEA RAS MMUYA

    May 16, 2025
  • WANAFUNZI KIDATO CHA SITA WAASWA SAFARI YA ELIMU BADO NI NDEFU

    May 17, 2025
  • RC SENYAMULE AZUNGUMZA NA MAKUNDI MBALIMBALI MKOANI KWAKE

    May 15, 2025
  • Tazama Zote

Video

RC SENYAMULE AKIZUNGUMZA KWENYE UZINDUZI WA SERA YA ELIMU NA MAFUNZO YA MWAKA 2014 TOLEO LA 2023.
Video Nyinginezo

Kurasa za Karibu

  • Speeches
  • mission and vision
  • Photo Gallery
  • Videos
  • Press Releases
  • Organization Structure
  • Reports
  • Client Service Charter
  • Acts

Tovuti Muhimu

  • PO-RALG
  • Public Service Management
  • Parliament of Tanzania
  • UDOM
  • Government Portal
  • Prime Minister's Office Website

World Visitors Tracker

world map hits counter

Rejesta ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Jengo la Mkapa (Mkapa House) Barabara ya Hospitali ya Mkoa

    Anuani ya Posta: 914 DODOMA

    Simu: +255 26 232 4343/232

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@dodoma.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya eneo

Hakimiliki©2016 GWF . Haki zote zimehifadhiwa.