• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Ofisi |
    • Malalamiko |
    • eoffice |
Dodoma Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Taasisi
      • Huduma Zetu
    • Huduma Zetu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Seksheni
      • Administration and Human Resource Management Section
      • Planning and Coordination
      • Infrastructure section
      • Management Monitoring and Inspection section;
      • Education and vocational Training section
      • Economic and productive sectors section;
      • Health, Social welfare and Nutrition services section
      • Industry, Trade and Investment section
    • Vitengo
      • Information Communication Technology (lcT) and Statistics
      • Government Communication Unit
      • Finance and Accounts unit;
      • Internal Audit unit
      • Legal services unit;
      • Procurement Management unit;
  • Wilaya
    • Bahi
    • Chamwino
    • Kongwa
    • Mpwapwa
    • Kondoa
    • Dodoma Mjini
    • Chemba
  • Mamlaka za Serikali za mitaa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bahi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chemba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa
    • Halmashauri ya Wilaya Mpwapwa
    • Halmashauri ya Mji Kondoa
    • The City Council of Dodoma (CCD)
  • Uwekezaji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Habari kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WAZAZI WAHIMIZWA KUANDIKISHA WATOTO MAPEMA MUHULA MPYA WA MASOMO 2025

Imetumwa : January 15th, 2025

Na. Hellen M. Minja,

       Habari – DODOMA RS

Kufuatia maelekezo aliyoyatoa Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule juu ya wazazi kupeleka watoto shuleni pindi muhula mpya utakapoanza, leo Januari 15, 2025, Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma Bw. Kaspar K. Mmuya, amefanya ziara ya kikazi kutembelea shule ya msingi Kisasa kujionea utekelezaji wa maelekezo hayo.

Akiwa shuleni hapo, Katibu Tawala huyo alizungumza na walimu pamoja na wanafunzi juu ya umuhimu wa wazazi kuwaandikisha watoto wao mapema ili kutopunguza siku zao za masomo zilizopo kwenye kalenda ya mwaka.

“Elimu inatolewa kisayansi tukifahamu mwanafunzi katika mwaka mmoja anatakiwa kuhudhuria shuleni kwa idadi ya siku, na mtoto akihudhuria siku zote anaweza kupata kiwango kilichokadiriwa na walimu. Mzazi ukichelewa kumleta mtoto shule, jinsi unavyochelewa ndivyo idadi ya siku za mtoto kuhudhuria shuleni unavyozipunguza” Bw. Mmuya

Akitoa taarifa ya shule hiyo, Mwalimu Mkuu Bi. Jesca Mwarabu amesema shule yake ilianzishwa mwaka 2007, kwa sasa ina jumla ya wanafunzi 2,479 na walimu 57. Shule inatekeleza mtaala ulioandaliwa na Wizara ya Elimu na kwa miaka mitano mfululizo imekua na ufaulu mzuri kwa 90% na zaidi katika mitihani ya kumaliza elimu ya msingi huku uandikishaji wa darasa la awali na la kwanza 2025 ukivuka lengo kwa zaidi ya 100%.

Kwa upande mwingine, Kiongozi huyo amefanya ziara ya kukagua mradi wa ujenzi wa shule mpya ya msingi Sokoine (Mahungu) yenye mkondo mmoja, iliyopo katika Kata ya Nala Jijini Dodoma inayojengwa kwa fedha shilingi 321,800,000 kutoka programu ya BOOST kwa mwaka 2024/2025 ,na mradi upo kwenye hatua za umaliziaji.

Aidha, ziara hiyo ilitamatika kwa kutembelea Hospitali ya Wilaya ya Dodoma Mjini iliyojengwa katika Kata ya Nala ambapo mradi umetekelezwa kutokana na changamoto ya muda mrefu kwa wakazi wa Jiji la Dodoma kukosa Hospitali ya ngazi hiyo. Mradi  umegharimu shilingi 1,500,000,000 fedha kutoka Serikali kuu na 480,000,000 kutoka Halmashauri ya Jiji na mpaka sasa mradi umekamilika kwa 98


#dodomafahariyawatanzania

#keroyakowajibuwangu                               #mtiwangubirthdayyangu

Matangazo

  • "WANANCHI JITOKEZENI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU 2025" - RC SENYAMULE February 17, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATANZANIA WATAKIWA KUILINDA NA KUIDUMISHA AMANI NI KURUHUSU MAENDELEO NCHINI

    May 15, 2025
  • MKURUGENZI WA ‘WATER FOR PEOPLE ‘ AMTEMBELEA RAS MMUYA

    May 16, 2025
  • WANAFUNZI KIDATO CHA SITA WAASWA SAFARI YA ELIMU BADO NI NDEFU

    May 17, 2025
  • RC SENYAMULE AZUNGUMZA NA MAKUNDI MBALIMBALI MKOANI KWAKE

    May 15, 2025
  • Tazama Zote

Video

RC SENYAMULE AKIZUNGUMZA KWENYE UZINDUZI WA SERA YA ELIMU NA MAFUNZO YA MWAKA 2014 TOLEO LA 2023.
Video Nyinginezo

Kurasa za Karibu

  • Speeches
  • mission and vision
  • Photo Gallery
  • Videos
  • Press Releases
  • Organization Structure
  • Reports
  • Client Service Charter
  • Acts

Tovuti Muhimu

  • PO-RALG
  • Public Service Management
  • Parliament of Tanzania
  • UDOM
  • Government Portal
  • Prime Minister's Office Website

World Visitors Tracker

world map hits counter

Rejesta ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Jengo la Mkapa (Mkapa House) Barabara ya Hospitali ya Mkoa

    Anuani ya Posta: 914 DODOMA

    Simu: +255 26 232 4343/232

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@dodoma.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya eneo

Hakimiliki©2016 GWF . Haki zote zimehifadhiwa.