• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Ofisi |
    • Malalamiko |
    • eoffice |
Dodoma Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Taasisi
      • Huduma Zetu
    • Huduma Zetu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Seksheni
      • Administration and Human Resource Management Section
      • Planning and Coordination
      • Infrastructure section
      • Management Monitoring and Inspection section;
      • Education and vocational Training section
      • Economic and productive sectors section;
      • Health, Social welfare and Nutrition services section
      • Industry, Trade and Investment section
    • Vitengo
      • Information Communication Technology (lcT) and Statistics
      • Government Communication Unit
      • Finance and Accounts unit;
      • Internal Audit unit
      • Legal services unit;
      • Procurement Management unit;
  • Wilaya
    • Bahi
    • Chamwino
    • Kongwa
    • Mpwapwa
    • Kondoa
    • Dodoma Mjini
    • Chemba
  • Mamlaka za Serikali za mitaa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bahi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chemba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa
    • Halmashauri ya Wilaya Mpwapwa
    • Halmashauri ya Mji Kondoa
    • The City Council of Dodoma (CCD)
  • Uwekezaji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Habari kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

DODOMA WAPANDA MITI 1,480 KUADHIMISHA BIRTHDAY YA MHE. RAIS

Imetumwa : January 27th, 2025

Na. Hellen M. Minja,

       Habari – DODOMA RS

Katika kuadhimisha kumbukizi ya kuzaliwa kwa  Rais wa Jamhuri ya Muunga o wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo Januari 27, 2025, Watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Taasisi na vikundi mbalimbali wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa huu Mhe. Rosemary Senyamule, wamepanda miti 1,480 katika eneo la viwanja vya Nanenane, Nzuguni Jijini Dodoma.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo iliyoambatana na ukataji keki pamoja na shampeni, Mhe. Senyamule amemtaja Mhe. Dkt Samia kama muasisi wa kampeni ya kukijanisha Dodoma.

“Mhe. Dkt. Samia ndiye alianzisha kazi ya kukijanisha Dodoma alipozindua upandaji miti na neno la ‘Dodoma ya Kijani’ lilianza wakati huo akiwa Makamu wa Rais mwaka 2017 pale Mzakwe ambapo alipanda miti. Tangu wakati huo, tuliendelea na kauli mbiu ya kusema Dodoma ya Kijani na yeye akisema dhamira yake ya kutamani Dodoma kuwa ya kijani”

Aidha, amehimiza kufuatwa kwa sheria zilizowekwa juu ya upandaji miti kwa mtu mmoja mmoja miti mitano na Taasisi miti 20;

“Leo tumejikumbusha kupitia siku ya kuzaliwa Mhe. Rais ambaye kwa umoja wetu tumeona thamani ya kukutana hapa. Jiji na Halmashauri, tusimamie sheria hizi kwa sababu miti ni uhai ili baadae, kila mtu ajivunie kuwa sehemu ya kubadilisha mazingira ya Dodoma” Mhe. Senyamule.

Nae, Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma Bw. Kaspar K. Mmuya, amesema, kati ya miti iliyopandwa siku ya leo, miti 20 ni ya tiba asili ambapo chama cha tiba asili kimefika Mkoa wa Dodoma kuunga mkono juhudi za kutunza mazingira na kuifanya Dodoma kuwa ya kijani ili kufanana na Makao Makuu ya nchi.

Hata hivyo, Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mjini Mhe. Jabir Shekimweri amesema kumekua na mwitikio mkubwa kwa wakazi wa Dodoma kwenye zoezi la upandaji miti huku akitoa rai kwa kila mmoja kupanda miti wakati wa kumbukizi yake ya kuzaliwa kwani kwa kufanya hivyo, ajenda ya kukijanisha Dodoma itafanikiwa kwa haraka zaidi.


#dodomafahariyawatanzania

#27yamamamtiwangubirthdayyangu

Matangazo

  • "WANANCHI JITOKEZENI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU 2025" - RC SENYAMULE February 17, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • UBALOZI WA UINGEREZA NCHINI TANZANIA WAADHIMISHA MAFANIKIO YA MWAKA MMOJA NCHINI

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI YA ‘ DIPLOMATIC CAPITAL CITY TOUR’ YAIVA

    May 08, 2025
  • DODOMA YADHAMIRIA KUJIKITA KWENYE KILIMO CHA MATUFAHA (APPLES) KUINUA UCHUMI

    May 08, 2025
  • MAAFISA MAZINGIRA WAPEWA HEKO NA RAS MMUYA

    May 06, 2025
  • Tazama Zote

Video

RC SENYAMULE AKIZUNGUMZA KWENYE UZINDUZI WA SERA YA ELIMU NA MAFUNZO YA MWAKA 2014 TOLEO LA 2023.
Video Nyinginezo

Kurasa za Karibu

  • Speeches
  • mission and vision
  • Photo Gallery
  • Videos
  • Press Releases
  • Organization Structure
  • Reports
  • Client Service Charter
  • Acts

Tovuti Muhimu

  • PO-RALG
  • Public Service Management
  • Parliament of Tanzania
  • UDOM
  • Government Portal
  • Prime Minister's Office Website

World Visitors Tracker

world map hits counter

Rejesta ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Jengo la Mkapa (Mkapa House) Barabara ya Hospitali ya Mkoa

    Anuani ya Posta: 914 DODOMA

    Simu: +255 26 232 4343/232

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@dodoma.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya eneo

Hakimiliki©2016 GWF . Haki zote zimehifadhiwa.