• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Ofisi |
    • Malalamiko |
    • eoffice |
Dodoma Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Taasisi
      • Huduma Zetu
    • Huduma Zetu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Seksheni
      • Administration and Human Resource Management Section
      • Planning and Coordination
      • Infrastructure section
      • Management Monitoring and Inspection section;
      • Education and vocational Training section
      • Economic and productive sectors section;
      • Health, Social welfare and Nutrition services section
      • Industry, Trade and Investment section
    • Vitengo
      • Information Communication Technology (lcT) and Statistics
      • Government Communication Unit
      • Finance and Accounts unit;
      • Internal Audit unit
      • Legal services unit;
      • Procurement Management unit;
  • Wilaya
    • Bahi
    • Chamwino
    • Kongwa
    • Mpwapwa
    • Kondoa
    • Dodoma Mjini
    • Chemba
  • Mamlaka za Serikali za mitaa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bahi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chemba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa
    • Halmashauri ya Wilaya Mpwapwa
    • Halmashauri ya Mji Kondoa
    • The City Council of Dodoma (CCD)
  • Uwekezaji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Habari kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

KAMATI YA BUNGE TAMISEMI YATEMBELEA SOKO LA MACHINGA DODOMA

Imetumwa : October 28th, 2024

Na. Hellen M. Majid,

       Habari – DODOMA RS

Kamati ya Bunge ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) leo Oktoba 28, 2024, imefanya ziara ya kikazi katika  Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma na baadae  kukagua soko la wazi laWajasiriamali Wadogo (Machinga) lililojengwa katika kata ya Majengo, Mtaa wa Kitenge, tawi la Bahi Road.

Kamati hiyo iliyoongozwa na Mwenyekiti wake Mhe. Justin L. Nyamoga pamoja na naibu waziri wa TAMISEMI Mhe. Festo Dugange, imetembelea na kujionea namna soko hilo lililojengwa kwa fedha kutoka Serikali Kuu pamoja na mapato ya ndani ya Halamashauri ya Jiji la Dodoma linavyoendeshwa.

Akizungumzia ukusanyaji wa ushuru wa soko kwa mwaka wa fedha 2023/2024 wakati akitoa taarifa ya uendeshaji wa soko hilo la wazi la Machinga, Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma Dkt. Frederick D. Sagamiko amesema;

“kwa kipindi cha Julai, 2023/Juni 2024, soko la Machinga limeweza kukusanya kiasi cha shilingi Milioni 460 kati ya bilioni 1 iliyokisiwa, sawa na 46% ya lengo. Mwaka wa fedha 2024/2025, jumla ya shilingi 1,902,895,000 zimepangwa kukusanywa kutoka vyanzo mbalimbali vya mapato ndani ya soko na kwa kipindi cha robo ya kwanza, shilingi 130,346,801 zimekusanywa” Dkt. Sagamiko

Hata hivyo, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary S. Senyamule, amesema;

“Nitafuatilia idadi kamili ya watu waliopo pale ili kupata uhakika kamili wa mapato yanayozaliwa. Juhudi mbalimbali zimefanyika ili kufanya uhai wa lile soko uweze kuongezeka kwani kila mwaka tumekua tukifanya kile kinachowezekana ili kufikia mahitaji yote ambayo machinga wamekua wakiyaomba”.

Nae, Katibu wa soko hilo Bw. Marko S. Mwagale, amezungumzia changamoto kadhaa zinazoendelea kulikabili soko hilo huku akitaja uchache wa wateja wanaofika hapo kutokana na idadi ndogo ya mabasi ya abiria wa ndani maarufu kama daladala zinazopakia na kushusha abiria sokoni hapo.

Akihitimisha ziara hiyo, Mwenyekiti wa Kamati hiyo ametoa maelekezo kadhaa yakiwemo; kusitishwa kwa zoezi la kutafuta Mzabuni wa soko, kuweka mfumo wa malipo ya ushuru kwa ‘control number’, miundombinu ya eneo la wauza mbogamboga iboreshwe pia, Kamati imehitaji kupatiwa mpango juu ya eneo la Sabasaba lililopo Jijini humu.


#kurayakosautiyako              

#ujanjanikupigakura    

#dodomatukotayarikupigakura

#mtiwangubirthdayyangu

Matangazo

  • "WANANCHI JITOKEZENI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU 2025" - RC SENYAMULE February 17, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MAAFISA MAZINGIRA WAPEWA HEKO NA RAS MMUYA

    May 06, 2025
  • RAS MMUYA AFUNGUA KIKAO KAZI CHA MAAFISA UTUMISHI MKOA WA DODOMA

    May 05, 2025
  • KAMPUNI YA "CAVO'' YA CHINA YATAFUTA FURSA ZA UWEKEZAJI DODOMA

    May 05, 2025
  • TAWLA - SAUTI YA WANAWAKE NA WATOTO WALIOKOSA ULINZI WA KISHERIA KATIKA JAMII

    May 03, 2025
  • Tazama Zote

Video

RC SENYAMULE AKIZUNGUMZA KWENYE UZINDUZI WA SERA YA ELIMU NA MAFUNZO YA MWAKA 2014 TOLEO LA 2023.
Video Nyinginezo

Kurasa za Karibu

  • Speeches
  • mission and vision
  • Photo Gallery
  • Videos
  • Press Releases
  • Organization Structure
  • Reports
  • Client Service Charter
  • Acts

Tovuti Muhimu

  • PO-RALG
  • Public Service Management
  • Parliament of Tanzania
  • UDOM
  • Government Portal
  • Prime Minister's Office Website

World Visitors Tracker

world map hits counter

Rejesta ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Jengo la Mkapa (Mkapa House) Barabara ya Hospitali ya Mkoa

    Anuani ya Posta: 914 DODOMA

    Simu: +255 26 232 4343/232

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@dodoma.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya eneo

Hakimiliki©2016 GWF . Haki zote zimehifadhiwa.