• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Ofisi |
    • Malalamiko |
    • eoffice |
Dodoma Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Taasisi
      • Huduma Zetu
    • Huduma Zetu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Seksheni
      • Administration and Human Resource Management Section
      • Planning and Coordination
      • Infrastructure section
      • Management Monitoring and Inspection section;
      • Education and vocational Training section
      • Economic and productive sectors section;
      • Health, Social welfare and Nutrition services section
      • Industry, Trade and Investment section
    • Vitengo
      • Information Communication Technology (lcT) and Statistics
      • Government Communication Unit
      • Finance and Accounts unit;
      • Internal Audit unit
      • Legal services unit;
      • Procurement Management unit;
  • Wilaya
    • Bahi
    • Chamwino
    • Kongwa
    • Mpwapwa
    • Kondoa
    • Dodoma Mjini
    • Chemba
  • Mamlaka za Serikali za mitaa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bahi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chemba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa
    • Halmashauri ya Wilaya Mpwapwa
    • Halmashauri ya Mji Kondoa
    • The City Council of Dodoma (CCD)
  • Uwekezaji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Habari kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RAS DODOMA ATEMBELEA MRADI WA JP - RWEE UNAOTEKELEZWA CHAMWINO

Imetumwa : October 30th, 2024

Na. Hellen M. Minja,          

       Habari – DODOMA RS


Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma Bw. Kaspar K. Mmuya, ametembelea vikundi vya kina mama wajasiriamali wadogo pamoja na wakulima wanaowezeshwa na mashirika ya kimataifa kulima na kutengeneza bidhaa kitaalamu katika Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino Oktoba 29,2024.


Vikundi hivyo kutoka katika vijiji vya Chamwino Ikulu, Nayu na Dabalo vipo chini ya mradi unaojulikana kama JP-RWEE unaofadhiliwa na mashirika manne ya kimataifa ambayo ni FAO, IFAD, WFP na UN-WOMEN wenye lengo la kuboresha maisha ya wanawake waishio vijijini.


Akiongea na wanawake walio kwenye mradi wa kuwezeshwa kupata hati miliki za ardhi katika kijiji cha Nayu, Kata ya Badalo, Bw. Mmuya ametoa wito kwa mashirika hayo kuwashirikisha wanawake hao kwenye kila wanachokifanya ili waweze kuwa na uelewa wa kutosha.


“Shughuli zote za Serikali tunazozifanya, tuwaunganishe wananchi na Serikali yao wajue nini Serikali inawafanyia. Hiki ninachokieleza ni mpango wa Serikali kuwawezesha wananchi wake kumiliki ardhi kisheria, hiyo inatusaidia sisi kupunguza migogoro ya ardhi lakini pia kupunguza unyanyasaji wa kijinsia” Bw. Mmuya.


Aidha, akiwasilisha moja ya matokeo tarajiwa ya mradi kwa niaba ya Katibu Tawala Wilaya ya Chamwino, Afisa Kilimo wa Wilaya hiyo Bw. Living Kilawe, amesema, wanatarajia kuongezeka kwa upatikanaji wa rasilimali, mali na teknolojia muhimu kwa uzalishaji wa kilimo unaostahimili hali ya hewa na usalama wa chakula na lishe.


Kadhalika, Mratibu wa Mradi kutoka WFP Bw. Abiudi Gamba, amesema mradi wa JP-RWEE unatekelezwa kwa kipindi cha miaka mitano, umeanza mwaka 2022 na unatarajiwa kukamilika 2027 ukihamasisha kilimo cha mazao ya Mtama, mboga mboga na Alizeti lakini zaidi ya hayo kuna shughuli za kiuchumi zinazofanyika.


Mradi wa JP-RWEE unatekelezwa katika Kata 18 na Vijiji 40 ukilenga jumla ya wanawake 8,000. 3,500 kutoka Mkoa wa Singida (Ikungi), 3,500 kutoka Dodoma (Chamwino) na 1,000 kutoka Zanzibar ili kuhakikisha haki na ustawi wa wanawake unafikiwa kuelekea Agenda 2030 ya Maendeleo Endelevu.




#kurayakosautiyako              

#ujanjanikupigakura              

#dodomatukotayarikupigakura

#mtiwangubirthdayyangu

Matangazo

  • "WANANCHI JITOKEZENI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU 2025" - RC SENYAMULE February 17, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MAANDALIZI YA ‘ DIPLOMATIC CAPITAL CITY TOUR’ YAIVA

    May 08, 2025
  • DODOMA YADHAMIRIA KUJIKITA KWENYE KILIMO CHA MATUFAHA (APPLES) KUINUA UCHUMI

    May 08, 2025
  • MAAFISA MAZINGIRA WAPEWA HEKO NA RAS MMUYA

    May 06, 2025
  • RAS MMUYA AFUNGUA KIKAO KAZI CHA MAAFISA UTUMISHI MKOA WA DODOMA

    May 05, 2025
  • Tazama Zote

Video

RC SENYAMULE AKIZUNGUMZA KWENYE UZINDUZI WA SERA YA ELIMU NA MAFUNZO YA MWAKA 2014 TOLEO LA 2023.
Video Nyinginezo

Kurasa za Karibu

  • Speeches
  • mission and vision
  • Photo Gallery
  • Videos
  • Press Releases
  • Organization Structure
  • Reports
  • Client Service Charter
  • Acts

Tovuti Muhimu

  • PO-RALG
  • Public Service Management
  • Parliament of Tanzania
  • UDOM
  • Government Portal
  • Prime Minister's Office Website

World Visitors Tracker

world map hits counter

Rejesta ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Jengo la Mkapa (Mkapa House) Barabara ya Hospitali ya Mkoa

    Anuani ya Posta: 914 DODOMA

    Simu: +255 26 232 4343/232

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@dodoma.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya eneo

Hakimiliki©2016 GWF . Haki zote zimehifadhiwa.