• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Ofisi |
    • Malalamiko |
    • eoffice |
Dodoma Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Taasisi
      • Huduma Zetu
    • Huduma Zetu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Seksheni
      • Administration and Human Resource Management Section
      • Planning and Coordination
      • Infrastructure section
      • Management Monitoring and Inspection section;
      • Education and vocational Training section
      • Economic and productive sectors section;
      • Health, Social welfare and Nutrition services section
      • Industry, Trade and Investment section
    • Vitengo
      • Information Communication Technology (lcT) and Statistics
      • Government Communication Unit
      • Finance and Accounts unit;
      • Internal Audit unit
      • Legal services unit;
      • Procurement Management unit;
  • Wilaya
    • Bahi
    • Chamwino
    • Kongwa
    • Mpwapwa
    • Kondoa
    • Dodoma Mjini
    • Chemba
  • Mamlaka za Serikali za mitaa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bahi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chemba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa
    • Halmashauri ya Wilaya Mpwapwa
    • Halmashauri ya Mji Kondoa
    • The City Council of Dodoma (CCD)
  • Uwekezaji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Habari kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC SENYAMULE ATAKA HATUA KALI ZICHUKULIWE DHIDI YA WANAOHUJUMU MIUNDOMBINU YA SERIKALI

Imetumwa : December 18th, 2024

Na. Hellen M. Minja,

       Habari – DODOMA RS

Kufuatia wimbi la wizi wa vifaa vya miundombinu ya Taasisi za Serikali, agizo limetolewa kwa Wakuu wa Wilaya za Mkoa wa Dodoma kukaa na kupanga mkakati wa namna ya kukabiliana na changamoto hiyo inayowagharimu wananchi kwa kukosa huduma za msingi, lakini pia kuitia Serikali hasara kubwa.

Agizo hilo limetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule wakati wa kikao cha kwanza kwa mwaka 2024/2025 cha Bodi ya Barabara Mkoa wa Dodoma kilichofanyika Disemba 18, 2024 katika ukumbi wa ofisi yake Jijini Dodoma.

“Suala la wizi wa miundombinu linasikitisha sana, si kiashiria kizuri kuendelea kukifumbia macho na tupeane majukumu, wakuu wa Wilaya  nendeni katika Wilaya zenu mkakae, mje na mikakati ya namna gani mnakwenda kukabiliana na wizi wa miundombinu ya Serikali na ninawapa muda, mpaka mwishoni mwa mwezi Desemba ” Mhe. Senyamule.

Aidha, Mkuu huyo wa Mkoa amesisitiza umuhimu wa kushirikisha Wananchi kwenye miradi inayotekelezwa katika maeneo yao ili kila mmoja  awe sehemu ya miradi hiyo kwani wao ndio wanufaika na walinzi pia.

“Kuna utaratibu ambao upo kwenye miradi ya Serikali unaosema, kila mradi unapokwenda kwenye Kijiji, Kata, ni lazima wananchi washirikishwe kwenye mradi husika, lazima taarifa ibandikwe kwenye Serikali ya kijiji, ofisi au Kata ili kila mwanakijiji ajue na awe sehemu ya mradi” Amesisitiza Mhe. Senyamule

Akizungumzia hali ya Barabara za Mkoa hasa kipindi hiki cha mvua, Meneja wa Wakala wa Barabara Tanzania TANROADS, Mhandisi Zuhura H. Amani amesema;

“Sehemu kubwa ya mtandao wa barabara za Mkoa ziko katika hali nzuri,isipokua baadhi ya barabara ambazo ziliharibiwa na mvua hali iliyosababisha baadhi ya maeneo kutopitika ,na mengine kupitika kwa shida. Hadi kufikia mwishoni mwa Novemba, 2024, matengenezo ya kuimarisha au kurudisha mawasiliano yamefanyika na mengine yanaendelea” Mhandisi Zuhura.

Katika wasilisho la Wakala wa Barabara za Mijini na Vijijini (TARURA),pamoja na mambo mengine, lilizungumzia mapitio ya mpango na bajeti kwa mwaka wa fedha 2024/2025, ambapo kwenye utekelezaji wa Mpango wa Bajeti ya matengenezo ya barabara zimetenga jumla ya shilingi 36,152,430,180.00 kati ya fedha hizi, shilingi 34,545,682,494.00 ni kwa ajili ya matengenezo na ujenzi wa miundombinu ya barabara na 1,606,747,686.00 kwa ajili ya shughuli za utawala, usimamizi, ufuatiliaji na Tathmini ya utekelezaji wa miradi ya matengenezo ya miundombinu ya barabara ngazi ya Mkoa na Wilaya.

Awali, katibu tawala Mkoa wa Dodoma Bw. Kaspar Mmuya alikumbusha kuwa vikao vya bodi ya barabara ambavyo hufanyika mara mbili kwa mwaka ni kwa mujibu wa sheria na moja ya jukumu la bodi hiyo ni kushauri na kutoa mapendekezo kwa Waziri mwenye dhamana ya barabara kuhusiana na ujenzi au uendelezaji wa mtandao wa barabara katika Mkoa husika  

&&&


#dodomafahariyawatanzania

#keroyakowajibuwangu

 #mtiwangubirthdayyangu

Matangazo

  • "WANANCHI JITOKEZENI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU 2025" - RC SENYAMULE February 17, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MADEREVA WA SERIKALI WATAKIWA KUZINGATIA SHERIA ZA USALAMA BARABARANI

    May 17, 2025
  • WATANZANIA WATAKIWA KUILINDA NA KUIDUMISHA AMANI NI KURUHUSU MAENDELEO NCHINI

    May 15, 2025
  • MKURUGENZI WA ‘WATER FOR PEOPLE ‘ AMTEMBELEA RAS MMUYA

    May 16, 2025
  • WANAFUNZI KIDATO CHA SITA WAASWA SAFARI YA ELIMU BADO NI NDEFU

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

RC SENYAMULE AKIZUNGUMZA KWENYE UZINDUZI WA SERA YA ELIMU NA MAFUNZO YA MWAKA 2014 TOLEO LA 2023.
Video Nyinginezo

Kurasa za Karibu

  • Speeches
  • mission and vision
  • Photo Gallery
  • Videos
  • Press Releases
  • Organization Structure
  • Reports
  • Client Service Charter
  • Acts

Tovuti Muhimu

  • PO-RALG
  • Public Service Management
  • Parliament of Tanzania
  • UDOM
  • Government Portal
  • Prime Minister's Office Website

World Visitors Tracker

world map hits counter

Rejesta ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Jengo la Mkapa (Mkapa House) Barabara ya Hospitali ya Mkoa

    Anuani ya Posta: 914 DODOMA

    Simu: +255 26 232 4343/232

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@dodoma.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya eneo

Hakimiliki©2016 GWF . Haki zote zimehifadhiwa.