• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Ofisi |
    • Malalamiko |
    • eoffice |
Dodoma Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Taasisi
      • Huduma Zetu
    • Huduma Zetu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Seksheni
      • Administration and Human Resource Management Section
      • Planning and Coordination
      • Infrastructure section
      • Management Monitoring and Inspection section;
      • Education and vocational Training section
      • Economic and productive sectors section;
      • Health, Social welfare and Nutrition services section
      • Industry, Trade and Investment section
    • Vitengo
      • Information Communication Technology (lcT) and Statistics
      • Government Communication Unit
      • Finance and Accounts unit;
      • Internal Audit unit
      • Legal services unit;
      • Procurement Management unit;
  • Wilaya
    • Bahi
    • Chamwino
    • Kongwa
    • Mpwapwa
    • Kondoa
    • Dodoma Mjini
    • Chemba
  • Mamlaka za Serikali za mitaa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bahi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chemba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa
    • Halmashauri ya Wilaya Mpwapwa
    • Halmashauri ya Mji Kondoa
    • The City Council of Dodoma (CCD)
  • Uwekezaji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Habari kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC SENYAMULE ATOA MSAADA WA MABATI KWA WAHITAJI

Imetumwa : January 27th, 2025

Na. Hellen M. Minja,

       Habari – DODOMA RS

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule, leo Januari 27, 2025, ametoa msaada wa mabati na fedha taslimu shilingi Milioni Moja kwa wakazi wawili wa Mkoa wake wenye mahitaji maalum ambao wote wamefanikiwa kujenga nyumba hadi hatua ya lenta lakini wameshindwa kupaua kutokana na changamoto mbalimbali zinazowakabili.

Akikabidhi msaada huo, kwenye viwanja vya ofisi yake Jengo la Mkapa Jijini Dodoma, Mhe. Senyamule amesema Mkoa unayo sababu ya kuwasaidia kumalizia pale walipofikia kwani tayari wameonesha juhudi za kuanza ujenzi wa nyumba na kuongeza kuwa Mhe. Rais anajali makundi yote katika jamii.

“Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan anajali makundi yote, ya kina mama na watu wenye ulemavu, ni makundi ambayo Serikali inayapa uzito wa pekee ndio maana tuliposikia uhitaji huu, tukaona tunayo sababu ya kupokea maelekezo ya Mhe. Rais ya kutekeleza yale ambayo yeye anatamani kuyaona kuhakikisha makundi haya yanakaa mahali salama”

“Kupitia kuweka mabati kwenye nyumba zenu, naamini sasa mtakua salama. Niwaombe muende mkatumie mabati haya kwa lengo lililokusudiwa kama mlivyoomba. Wataalamu wa Ustawi wa jamii mpo hapa, mtakwenda kuwatembelea kuona kazi ambayo wameifanya kutokana na hiki kidogo walichokipata” Ameongeza Mhe. Senyamule

Kadhalika, Bw. Kombo Jumbe ambaye ni mnufaika mwenye ulemavu wa miguu, ameishukuru Serikali ya Mkoa kwa msaada na kuonesha kuwajali watu wa makundi maalumu kwani alianza kujenga nyumba lakini kutokana na changamoto aliyonayo, ameshindwa kumalizia kuezeka hivyo, msaada alioupata utamtosha kumalizia nyumba yake.

Nae Bi. Farida Saidi, Mkazi wa Mkonze Jijini Dodoma, ambaye pia ni mnufaika wa mabati kwa ajili ya kuezekea nyumba yake, ametoa shukrani zake kwa Serikali ya Mkoa kwa kuonesha kuguswa na kadhia anayoipata hasa kipindi cha mvua kwani alijenga nyumba lakini akakwama kuezeka hali iliyopelekea kuweka maturubai pekee.


#dodomafahariyawatanzania

#keroyakowajibuwangu

#mtiwangubirthdayyangu

Matangazo

  • "WANANCHI JITOKEZENI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU 2025" - RC SENYAMULE February 17, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI HODARI 2025 KUTOKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA DODOMA WAPONGEZWA

    May 09, 2025
  • MRADI WA KUIMARISHA HUDUMA ZA KIFAFA WAZINDULIWA DODOMA

    May 08, 2025
  • UBALOZI WA UINGEREZA NCHINI TANZANIA WAADHIMISHA MAFANIKIO YA MWAKA MMOJA NCHINI

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI YA ‘ DIPLOMATIC CAPITAL CITY TOUR’ YAIVA

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

RC SENYAMULE AKIZUNGUMZA KWENYE UZINDUZI WA SERA YA ELIMU NA MAFUNZO YA MWAKA 2014 TOLEO LA 2023.
Video Nyinginezo

Kurasa za Karibu

  • Speeches
  • mission and vision
  • Photo Gallery
  • Videos
  • Press Releases
  • Organization Structure
  • Reports
  • Client Service Charter
  • Acts

Tovuti Muhimu

  • PO-RALG
  • Public Service Management
  • Parliament of Tanzania
  • UDOM
  • Government Portal
  • Prime Minister's Office Website

World Visitors Tracker

world map hits counter

Rejesta ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Jengo la Mkapa (Mkapa House) Barabara ya Hospitali ya Mkoa

    Anuani ya Posta: 914 DODOMA

    Simu: +255 26 232 4343/232

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@dodoma.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya eneo

Hakimiliki©2016 GWF . Haki zote zimehifadhiwa.