• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Ofisi |
    • Malalamiko |
    • eoffice |
Dodoma Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Taasisi
      • Huduma Zetu
    • Huduma Zetu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Seksheni
      • Administration and Human Resource Management Section
      • Planning and Coordination
      • Infrastructure section
      • Management Monitoring and Inspection section;
      • Education and vocational Training section
      • Economic and productive sectors section;
      • Health, Social welfare and Nutrition services section
      • Industry, Trade and Investment section
    • Vitengo
      • Information Communication Technology (lcT) and Statistics
      • Government Communication Unit
      • Finance and Accounts unit;
      • Internal Audit unit
      • Legal services unit;
      • Procurement Management unit;
  • Wilaya
    • Bahi
    • Chamwino
    • Kongwa
    • Mpwapwa
    • Kondoa
    • Dodoma Mjini
    • Chemba
  • Mamlaka za Serikali za mitaa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bahi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chemba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa
    • Halmashauri ya Wilaya Mpwapwa
    • Halmashauri ya Mji Kondoa
    • The City Council of Dodoma (CCD)
  • Uwekezaji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Habari kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

VITUO VYA ‘KILIMO ANGA’NCHINI,KUPATA NDEGE MPYA ZA KUDHIBITI VISUMBUFU VYA MIMEA

Imetumwa : May 30th, 2025

Na. Hellen M. Minja

       Habari – DODOMA RS

Waziri wa Kilimo Mhe. Hussein Bashe, ametoa maelekezo kwa Watendaji wa Wizara yake kuanza mchakato wa ununuzi wa ndege mpya tatu kwa ajili ya  vituo vya Kilimo Anga vya kanda vilivyopo katika mikoa ya Arusha,Mbeya na Mwanza lengo likiwa ni kudhibiti visumbufu vya mimea.

Maelekezo hayo ameyatoa wakati wa hafla ya mapokezi ya ndege moja ya kudhibiti visumbufu vya mimea iliyonunuliwa na Serikali chini ya Wizara hiyo kwenye Kiwanja kidogo cha ndege Mkoani Dodoma Mei 30, 2025 ambayo itatumika katika kituo cha Kanda ya Kati.

“Vituo vyote hivi vinatakiwa viwe vina ndege na ‘drones’ kwa hiyo, mchakato wa kununua ndege tatu nyingine uanze sasa hivi. Ni lazima kama Nchi ijitegemee, dunia ya kubebana haipo. Lazima tuweze kutoa huduma, tumeshaanza kununua ‘drones’ za kufanya ‘survilence’, mwaka huu tunanunua drone kwa ajili ya ‘spraying’.” Mhe. Bashe.

Kadhalika, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania (TPHPA) Prof. Joseph Ndunguru, amesema ndege hiyo inalenga kuleta mageuzi makubwa katika Sekta ya Kilimo kwa kuleta tija, ajira na kupanua masoko lakini pia kuimarisha hali ya chakula hapa nchini na kuongeza kuwa visumbufu vya mimea ni moja ya jitihada za Mamlaka katika kuleta tija kwenye sekta hiyo.

Hata hivyo, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe Rosemary Senyamule ameishukuru Wizara ya Kilimo kwa ununuzi wa Ndege hiyo ambayo italeta matumaini kwa Mkulima.

“Utashi huu unakwenda kuleta matumaini kwa Mkulima ambaye si mvivu, kwani amelima na kutunza mazao yake halafu mwishoni ndege anakula. Kwa Mkoa wa Dodoma itatuongezea upatikanaji wa chakula na wale wavivu sasa wataanza kulima kwani Dodoma pia tunapata athari ya Nzige maeneo ya Bahi na Kwelea kwelea maeneo ya Chemba, Kondoa na Kongwa.”

Ndege hiyo aina ya ‘Thrush 510 P2’iliyonunuliwa kwa gharama ya Shilingi 6,000,000,000 ina uwezo wa kukaa angani kwa zaidi ya saa 4 kutokana na tenki lake kubeba mafuta yenye ujazo wa lita 863, uwezo wa kubeba viuatilifu lita 1,930 uwezo wa kufanya udhibiti kwenye eneo la ekari 2400 kwa mara moja huku ikiwa na vifaa vya kisasa kwa ajili ya kutolea takwimu zinazowezesha mpango wa uthibiti wadudu na ndege waharibifu wa mazao na mimea.


#dodomafahariyawatanzania

#wekezadodomastawishadodoma

#keroyakowajibuwangu

#mtiwangubirthdayyangu

Matangazo

  • No records found
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RAIS DKT. SAMIA ASISITIZA KUIMARISHWA KWA KILIMO ILI KUJIHAKIKISHIA USALAMA WA CHAKULA

    June 28, 2025
  • SERIKALI IMEJIZATITI KULETA MAENDELEO KWA KUIMARISHA MAZINGIRA YA UWEKEZAJI NA BIASHARA

    June 25, 2025
  • TANZANIA SIYO SALAMA KWA WAUZAJI , WASAFIRISHA, WALIMAJI NA WATUMIAJI WA DAWA ZA KULEVYA” - MHE. MAJALIWA

    June 26, 2025
  • SHUGHULI ZA KIBINADAMU ZATAJWA KUWA TISHIO KWA CHANZO CHA MAJI BONDE LA MAKUTUPORA JIJINI DODOMA

    June 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

RC SENYAMULE AKIZUNGUMZA KWENYE UZINDUZI WA SERA YA ELIMU NA MAFUNZO YA MWAKA 2014 TOLEO LA 2023.
Video Nyinginezo

Kurasa za Karibu

  • Speeches
  • mission and vision
  • Photo Gallery
  • Videos
  • Press Releases
  • Organization Structure
  • Reports
  • Client Service Charter
  • Acts

Tovuti Muhimu

  • PO-RALG
  • Public Service Management
  • Parliament of Tanzania
  • UDOM
  • Government Portal
  • Prime Minister's Office Website

World Visitors Tracker

world map hits counter

Rejesta ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Jengo la Mkapa (Mkapa House) Barabara ya Hospitali ya Mkoa

    Anuani ya Posta: 914 DODOMA

    Simu: +255 26 232 4343/232

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@dodoma.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya eneo

Hakimiliki©2016 GWF . Haki zote zimehifadhiwa.