• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Ofisi |
    • Malalamiko |
    • eoffice |
Dodoma Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Taasisi
      • Huduma Zetu
    • Huduma Zetu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Seksheni
      • Administration and Human Resource Management Section
      • Planning and Coordination
      • Infrastructure section
      • Management Monitoring and Inspection section;
      • Education and vocational Training section
      • Economic and productive sectors section;
      • Health, Social welfare and Nutrition services section
      • Industry, Trade and Investment section
    • Vitengo
      • Information Communication Technology (lcT) and Statistics
      • Government Communication Unit
      • Finance and Accounts unit;
      • Internal Audit unit
      • Legal services unit;
      • Procurement Management unit;
  • Wilaya
    • Bahi
    • Chamwino
    • Kongwa
    • Mpwapwa
    • Kondoa
    • Dodoma Mjini
    • Chemba
  • Mamlaka za Serikali za mitaa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bahi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chemba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa
    • Halmashauri ya Wilaya Mpwapwa
    • Halmashauri ya Mji Kondoa
    • The City Council of Dodoma (CCD)
  • Uwekezaji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Habari kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

KAMPENI YA 'GURUDUMU LA MAMA SAMIA '- MATOKEO YA IMANI YA SERIKALI KWA SEKTA BINAFSI

Imetumwa : May 28th, 2025

Na. Hellen M. Minja

       Habari – DODOMA RS

Rais wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ametajwa kutengeneza mazingira rafiki kwa Sekta Binafsi kujenga imani kubwa kwa Serikali hasa linapokuja suala la mikopo ambapo kampuni ya ‘Road Master’ kupitia kampeni ya ‘Gurudumu la Mama Samia’ inakopesha magurudumu ya Pikipiki kwa gharama nafuu na kwa malipo kidogo kidogo.

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule, ameyasema hayo leo Mei 28, 2025 alipokua akizindua Kampeni hiyo katika hafla fupi iliyofanyika kwenye viwanja vya soko la Machinga lililopo ‘Bahi Road’ Jijini humu ambapo magurudumu hayo yanakopeshwa kwa Maafisa usafirishaji wa Pikipiki maarufu kama Bodaboda.

“Sekta binafsi zimejenga Imani kubwa kwa Serikali kwa sababu ya dhamira ya Mhe. Rais kuwa yapo mambo ambayo yanatakiwa yafanywe na sekta binafsi lakini, ili sekta binafsi awe na Imani kuwa bodaboda nitawakopesha na kuwa amini kabla hajamaliza kulipa hela ni lazima itengeneze mazingira mazuri”.

Kadhalika, Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mhe. Jabir Shekimweri amempongeza Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini Mhe. Anthony Mavunde kwa kuendelea kujitoa kila wakati kusaidia wananchi wake kwani usaidizi huo, unakwenda kuokoa maisha na kuimarisha biashara za vijana hao siku za usoni.

Hata hivyo, Mbunge huyo amesema, kampeni hiyo imeridhiwa na Mhe. Rais kwa kuwagusa waendesha Bodaboda na Bajaji nchi nzima kwa kutambua changamoto kubwa waliyonayo ya upatikanaji wa matairi mapya kwa wakati, ikilenga kuwapunguzia mzigo vijana hao na mpango huo utaamsha ari ya vijana wengi kuzingatia sheria na kufuata taratibu hivyo kupunguza ajali za barabarani.

Naye, Mkurugenzi wa ‘Road Master’, Kampuni iliyoanzisha kampeni hiyo Bw. Fuein Makamba amesema kampuni yake imeitikia wito wa kumuunga mkono Mhe. Rais kupitia uwezeshaji wa haki za vijana hasa kundi la bodaboda na bajaji nchini kwani kupitia uwezeshaji huo, imeanzisha kampeni hiyo yenye lengo la kuchochea maendeleo ya vijana hao Mkoani hapa.  

Kupitia Mpango huo, Afisa usafirishaji wa Bodaboda au Bajaji ambaye atahitajika kununua tairi mpya lakini hana fedha kwa wakati mmoja, kupitia mpango huo ataweza kutoa shilingi 10,000 akapata tairi mpya ya shilingi 70,000 na fedha iliyobaki atailipa kidogo kidogo kwa siku 30 awe amemaliza kiasi chote kinachohitajika.


#dodomafahariyawatanzania

#wekezadodomastawishadodoma

#keroyakowajibuwangu

#mtiwangubirthdayyangu

Matangazo

  • "WANANCHI JITOKEZENI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU 2025" - RC SENYAMULE February 17, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MMUYA AHIMIZA UDHIBITI VIFO VYA MAMA NA MTOTO

    May 26, 2025
  • UHAKIKI ANUANI ZA MAKAZI KUANZA MEI 28 DODOMA

    May 26, 2025
  • WAWEKEZAJI WA VIWANDA KUTOKA DUBAI WABISHA HODI DODOMA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI KUTOKA TUME YA MADINI WAMTEMBELEA RAS MMUYA

    May 28, 2025
  • Tazama Zote

Video

RC SENYAMULE AKIZUNGUMZA KWENYE UZINDUZI WA SERA YA ELIMU NA MAFUNZO YA MWAKA 2014 TOLEO LA 2023.
Video Nyinginezo

Kurasa za Karibu

  • Speeches
  • mission and vision
  • Photo Gallery
  • Videos
  • Press Releases
  • Organization Structure
  • Reports
  • Client Service Charter
  • Acts

Tovuti Muhimu

  • PO-RALG
  • Public Service Management
  • Parliament of Tanzania
  • UDOM
  • Government Portal
  • Prime Minister's Office Website

World Visitors Tracker

world map hits counter

Rejesta ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Jengo la Mkapa (Mkapa House) Barabara ya Hospitali ya Mkoa

    Anuani ya Posta: 914 DODOMA

    Simu: +255 26 232 4343/232

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@dodoma.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya eneo

Hakimiliki©2016 GWF . Haki zote zimehifadhiwa.