• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Ofisi |
    • Malalamiko |
    • eoffice |
Dodoma Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Taasisi
      • Huduma Zetu
    • Huduma Zetu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Seksheni
      • Administration and Human Resource Management Section
      • Planning and Coordination
      • Infrastructure section
      • Management Monitoring and Inspection section;
      • Education and vocational Training section
      • Economic and productive sectors section;
      • Health, Social welfare and Nutrition services section
      • Industry, Trade and Investment section
    • Vitengo
      • Information Communication Technology (lcT) and Statistics
      • Government Communication Unit
      • Finance and Accounts unit;
      • Internal Audit unit
      • Legal services unit;
      • Procurement Management unit;
  • Wilaya
    • Bahi
    • Chamwino
    • Kongwa
    • Mpwapwa
    • Kondoa
    • Dodoma Mjini
    • Chemba
  • Mamlaka za Serikali za mitaa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bahi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chemba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa
    • Halmashauri ya Wilaya Mpwapwa
    • Halmashauri ya Mji Kondoa
    • The City Council of Dodoma (CCD)
  • Uwekezaji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Habari kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MAKAMU WA RAIS AIFARIJI FAMILIA YA MAREHEMU NKONDO

Imetumwa : February 17th, 2025

Na Sofia Remmi.

Habari-Dodoma Rs

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango na mwenza wake Mama Mbonimpaye Mpango wameifariji familia na waombolezaji mbalimbali kufuatia kifo cha Bw. Johnson Nkondo aliyekuwa Msaidizi wa Ofisi Mkuu - Ofisi ya Makamu wa Rais aliyefariki tarehe 13 Februari 2025 katika Hospitali ya Benjamini Mkapa mkoani Dodoma wakati akipatiwa matibabu.

Makamu wa Rais na Mwenza wake wametoa faraja hiyo walipowasili katika makazi ya familia ya Marehemu Johnson Nkondo eneo la Veyula Mkoani Dodoma leo tarehe 16 Februari 2025.

Akizungumza na waombolezaji, Makamu wa Rais amesema marehemu Nkondo alikuwa muadilifu aliyezingatia maadili ya Utumishi wa Umma na taratibu za kiofisi wakati wote wa utumishi wake. Amesema ni vema kumuenzi marehemu Nkondo kwa kujifunza namna alivyojitolea kulitumikia Taifa kwa uadilifu mkubwa pamoja na kuhakikisha kila mmoja anatimiza wajibu wake vema, kuishi vema na ndugu, majirani na marafiki.

Makamu wa Rais amewaombea faraja ya Mwenyezi Mungu iwafikie familia, ndugu, jamaa na marafiki walioguswa na msiba huo.

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule aliyeshiriki katika msiba huo, ametoa pole kwa familia na Ofisi ya Makamu wa Rais kwa kumpoteza mtumishi hodari. Amewasihi familia na waombolezaji kuendelea kumuomba Mungu awavushe salama katika kipindi kigumu cha msiba huo.

Marehemu Johnson Nkondo alizaliwa tarehe 20 Aprili 1966 na anatarajiwa kuzikwa tarehe 17 Februari 2025 kijijini kwao Bombo Wilaya Same mkoani Kilimanjaro.

Matangazo

  • "WANANCHI JITOKEZENI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU 2025" - RC SENYAMULE February 17, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MAAFISA MAZINGIRA WAPEWA HEKO NA RAS MMUYA

    May 06, 2025
  • RAS MMUYA AFUNGUA KIKAO KAZI CHA MAAFISA UTUMISHI MKOA WA DODOMA

    May 05, 2025
  • KAMPUNI YA "CAVO'' YA CHINA YATAFUTA FURSA ZA UWEKEZAJI DODOMA

    May 05, 2025
  • TAWLA - SAUTI YA WANAWAKE NA WATOTO WALIOKOSA ULINZI WA KISHERIA KATIKA JAMII

    May 03, 2025
  • Tazama Zote

Video

RC SENYAMULE AKIZUNGUMZA KWENYE UZINDUZI WA SERA YA ELIMU NA MAFUNZO YA MWAKA 2014 TOLEO LA 2023.
Video Nyinginezo

Kurasa za Karibu

  • Speeches
  • mission and vision
  • Photo Gallery
  • Videos
  • Press Releases
  • Organization Structure
  • Reports
  • Client Service Charter
  • Acts

Tovuti Muhimu

  • PO-RALG
  • Public Service Management
  • Parliament of Tanzania
  • UDOM
  • Government Portal
  • Prime Minister's Office Website

World Visitors Tracker

world map hits counter

Rejesta ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Jengo la Mkapa (Mkapa House) Barabara ya Hospitali ya Mkoa

    Anuani ya Posta: 914 DODOMA

    Simu: +255 26 232 4343/232

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@dodoma.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya eneo

Hakimiliki©2016 GWF . Haki zote zimehifadhiwa.