• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Ofisi |
    • Malalamiko |
    • eoffice |
Dodoma Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Taasisi
      • Huduma Zetu
    • Huduma Zetu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Seksheni
      • Administration and Human Resource Management Section
      • Planning and Coordination
      • Infrastructure section
      • Management Monitoring and Inspection section;
      • Education and vocational Training section
      • Economic and productive sectors section;
      • Health, Social welfare and Nutrition services section
      • Industry, Trade and Investment section
    • Vitengo
      • Information Communication Technology (lcT) and Statistics
      • Government Communication Unit
      • Finance and Accounts unit;
      • Internal Audit unit
      • Legal services unit;
      • Procurement Management unit;
  • Wilaya
    • Bahi
    • Chamwino
    • Kongwa
    • Mpwapwa
    • Kondoa
    • Dodoma Mjini
    • Chemba
  • Mamlaka za Serikali za mitaa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bahi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chemba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa
    • Halmashauri ya Wilaya Mpwapwa
    • Halmashauri ya Mji Kondoa
    • The City Council of Dodoma (CCD)
  • Uwekezaji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Habari kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC SENYAMULE AZINDUA BODI YA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA.

Imetumwa : January 29th, 2025

Na. Hellen M. Minja,

       Habari – DODOMA RS

Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma (General) imepata Bodi mpya ya ushauri itakayofanya kazi kwa karibu na Uongozi wa Taasisi hiyo ambayo imezinduliwa leo na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule katika hafla fupi iliyofanyika kwenye ukumbi wa Hospitali hiyo Jijini Dodoma.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Mhe. Senyamule amesema, ana Imani na bodi hiyo iliyo chini ya Mwenyekiti wake Dkt. Ezekiel Mpuya kwamba itakwenda kutatua changamoto mbalimbali zinazoikabili Hospitali hiyo.

“Nina imani na bodi hii. Ina mambo mengi lakini, ina uwezo mkubwa wa kufanya ushawishi huko kwenye Wizara husika tukaweza kufanya mabadiliko makubwa kupitia hospitali hii. Umuhimu wa kuboresha rufaa hii ni mkubwa kwani hatuhudumii tu wakazi wa Dodoma bali watu wengi kutoka Mataifa mbalimbali,” Mhe. Senyamule.

Kadhalika, Mganga Mfawidhi wa Hospitali na Katibu wa Bodi hiyo Dr. Ernest Ibenzi, amesema, Hospitali yake sasa inajipambanua kwa huduma bora za mifupa na inatarajia kuanzisha kitengo maalumu kwa ajili ya kutoa huduma hiyo.

“Tunatarajia kuanzisha kitengo maalumu cha huduma za mifupa hapa kitakachojulikana kama DOI yaani ‘Dodoma Orthopaedic Institute’ kama ilivyo MOI pale Muhimbili kwa kua huduma za kibingwa kwa wagonjwa wa mivunjiko na mifupa zinazotambulika Kimataifa, zinafanyika hapa. Hospitali imewezesha upatikanaji wa vifaa tiba na uanzishwaji wa huduma za upasuaji mifupa katika hospitali za rufaa za Mikoa ya Arusha, Geita, Njombe, Bukoba, Shinyanga, Mwananyamala, Iringa, Tumbi, na Morogoro lengo ni kuzifikia hospitali zote za Mikoa ambazo hazina huduma hii,” Dkt. Ibenzi

Hata hivyo, akitoa shukrani zake kwa mgeni rasmi kwa niaba ya Wajumbe wa Bodi, Mwenyekiti huyo amesema uwepo wa Mjumbe wa Kamati kuu umeipa uzito Bodi hiyo katika utekelezaji wa majukumu yake kwa kuwa itaweza kufanya kazi kwa urahisi na kuwafikia watoa maamuzi kwa haraka na kuahidi kutekeleza majukumu yao kwa weledi.


#dodomafahariyawatanzania

#keroyakowajibuwangu

#mtiwangubirthdayyangu

Matangazo

  • "WANANCHI JITOKEZENI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU 2025" - RC SENYAMULE February 17, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MAANDALIZI YA ‘ DIPLOMATIC CAPITAL CITY TOUR’ YAIVA

    May 08, 2025
  • DODOMA YADHAMIRIA KUJIKITA KWENYE KILIMO CHA MATUFAHA (APPLES) KUINUA UCHUMI

    May 08, 2025
  • MAAFISA MAZINGIRA WAPEWA HEKO NA RAS MMUYA

    May 06, 2025
  • RAS MMUYA AFUNGUA KIKAO KAZI CHA MAAFISA UTUMISHI MKOA WA DODOMA

    May 05, 2025
  • Tazama Zote

Video

RC SENYAMULE AKIZUNGUMZA KWENYE UZINDUZI WA SERA YA ELIMU NA MAFUNZO YA MWAKA 2014 TOLEO LA 2023.
Video Nyinginezo

Kurasa za Karibu

  • Speeches
  • mission and vision
  • Photo Gallery
  • Videos
  • Press Releases
  • Organization Structure
  • Reports
  • Client Service Charter
  • Acts

Tovuti Muhimu

  • PO-RALG
  • Public Service Management
  • Parliament of Tanzania
  • UDOM
  • Government Portal
  • Prime Minister's Office Website

World Visitors Tracker

world map hits counter

Rejesta ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Jengo la Mkapa (Mkapa House) Barabara ya Hospitali ya Mkoa

    Anuani ya Posta: 914 DODOMA

    Simu: +255 26 232 4343/232

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@dodoma.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya eneo

Hakimiliki©2016 GWF . Haki zote zimehifadhiwa.