• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Ofisi |
    • Malalamiko |
    • eoffice |
Dodoma Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Taasisi
      • Huduma Zetu
    • Huduma Zetu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Seksheni
      • Administration and Human Resource Management Section
      • Planning and Coordination
      • Infrastructure section
      • Management Monitoring and Inspection section;
      • Education and vocational Training section
      • Economic and productive sectors section;
      • Health, Social welfare and Nutrition services section
      • Industry, Trade and Investment section
    • Vitengo
      • Information Communication Technology (lcT) and Statistics
      • Government Communication Unit
      • Finance and Accounts unit;
      • Internal Audit unit
      • Legal services unit;
      • Procurement Management unit;
  • Wilaya
    • Bahi
    • Chamwino
    • Kongwa
    • Mpwapwa
    • Kondoa
    • Dodoma Mjini
    • Chemba
  • Mamlaka za Serikali za mitaa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bahi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chemba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa
    • Halmashauri ya Wilaya Mpwapwa
    • Halmashauri ya Mji Kondoa
    • The City Council of Dodoma (CCD)
  • Uwekezaji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Habari kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

SERIKALI IMEJIZATITI KULETA MAENDELEO KWA KUIMARISHA MAZINGIRA YA UWEKEZAJI NA BIASHARA

Imetumwa : June 25th, 2025

Na;Happiness E. Chindiye

     Habari - Dodoma RS

Serikali ya Awamu ya Sita, chini ya Uongozi madhubuti wa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imejizatiti kuleta maendeleo edelevu katika taifa la Tsnzania, ikiwemo kuboresha na kuimarisha mazingira ya uwekezaji na biashara Nchini.

Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary S. Senyamule wakati akifunga maadhimisho ya kitaifa ya udhibiti wa bidhaa bandia Duniani yaliyofanyika katika ukumbi  wa Mabele Jijini Dodoma. Tarehe 25.06.2025.

“Kupitia uwezeshaji wa Serikali kwa wananchi waliojiunga kwenye vikundi na kupatiwa mikopo katika ngazi mbalimbali, zikiwemo Mikoa na Wilaya, vikundi vya uzalishaji vinaendelea kupata nguvu ya kutengeneza bidhaa zilizo halisi na bora, baada ya kupatiwa mafunzo ya ujasiriamali kutoka SIDO, TBS, BRELA na FCC.

“Serikali kuendelea kuiamini na kuiwezesha Tume ya Ushindani kusimamia usalama wa soko, utimamu wa miliki-bunifu za bidhaa na kumlinda mlaji dhidi ya athari za bidhaa bandia.” - ameeleza Mhe. Senyamule

Hata hivyo amezielekeza Halmashauri za Mkoa huu kushirikiana na FCC katika kutoa elimu kwa vikundi kuhusu athari za bidhaa  bandia .

“Ili kuleta uendelevu wa mafanikio haya, nawaagiza Wakurugenzi wa Halmashauri zote mkoani Dodoma kushirikiana na FCC katika kutoa elimu kwa vikundi hivyo kuhusu athari za bidhaa bandia, ili waweze kulinda shughuli zao na kuwa sehemu ya mapambano haya.” Ameelekeza Mhe. Senyamule

Pia, ameelekeza waratibu wa vikao vya ushauri vya Mkoa na Wilaya (RCC na DCC) kuhakikisha FCC wanahusishwa katika vikao hivyo ili kutoa elimu na kushiriki kwenye mijadala muhimu inayohusu ushindani na maendeleo ya biashara.

Maadhimisho ya kitaifa ya udhibiti wa bidhaa bandia duniani awali yalifunguliwa na Waziri wa Viwanda na Biashara, Dkt. Selemani Jafo na kufuatiwa na Kongamano la Wafanyabiashara.


#dodomafahariyawatanzania

#wekezadodomastawishadodoma

#keroyakowajibuwangu

#mtiwangubirthdayyangu

Matangazo

  • "WANANCHI JITOKEZENI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU 2025" - RC SENYAMULE February 17, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • SERIKALI IMEJIZATITI KULETA MAENDELEO KWA KUIMARISHA MAZINGIRA YA UWEKEZAJI NA BIASHARA

    June 25, 2025
  • TANZANIA SIYO SALAMA KWA WAUZAJI , WASAFIRISHA, WALIMAJI NA WATUMIAJI WA DAWA ZA KULEVYA” - MHE. MAJALIWA

    June 26, 2025
  • SHUGHULI ZA KIBINADAMU ZATAJWA KUWA TISHIO KWA CHANZO CHA MAJI BONDE LA MAKUTUPORA JIJINI DODOMA

    June 25, 2025
  • VODACOM TANZANIA KUPANDISHA HADHI MINARA YAO KUIMARISHA MAWASILIANO DODOMA

    June 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

RC SENYAMULE AKIZUNGUMZA KWENYE UZINDUZI WA SERA YA ELIMU NA MAFUNZO YA MWAKA 2014 TOLEO LA 2023.
Video Nyinginezo

Kurasa za Karibu

  • Speeches
  • mission and vision
  • Photo Gallery
  • Videos
  • Press Releases
  • Organization Structure
  • Reports
  • Client Service Charter
  • Acts

Tovuti Muhimu

  • PO-RALG
  • Public Service Management
  • Parliament of Tanzania
  • UDOM
  • Government Portal
  • Prime Minister's Office Website

World Visitors Tracker

world map hits counter

Rejesta ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Jengo la Mkapa (Mkapa House) Barabara ya Hospitali ya Mkoa

    Anuani ya Posta: 914 DODOMA

    Simu: +255 26 232 4343/232

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@dodoma.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya eneo

Hakimiliki©2016 GWF . Haki zote zimehifadhiwa.