• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Ofisi |
    • Malalamiko |
    • eoffice |
Dodoma Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Taasisi
      • Huduma Zetu
    • Huduma Zetu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Seksheni
      • Administration and Human Resource Management Section
      • Planning and Coordination
      • Infrastructure section
      • Management Monitoring and Inspection section;
      • Education and vocational Training section
      • Economic and productive sectors section;
      • Health, Social welfare and Nutrition services section
      • Industry, Trade and Investment section
    • Vitengo
      • Information Communication Technology (lcT) and Statistics
      • Government Communication Unit
      • Finance and Accounts unit;
      • Internal Audit unit
      • Legal services unit;
      • Procurement Management unit;
  • Wilaya
    • Bahi
    • Chamwino
    • Kongwa
    • Mpwapwa
    • Kondoa
    • Dodoma Mjini
    • Chemba
  • Mamlaka za Serikali za mitaa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bahi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chemba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa
    • Halmashauri ya Wilaya Mpwapwa
    • Halmashauri ya Mji Kondoa
    • The City Council of Dodoma (CCD)
  • Uwekezaji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Habari kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

SHUGHULI ZA KIBINADAMU ZATAJWA KUWA TISHIO KWA CHANZO CHA MAJI BONDE LA MAKUTUPORA JIJINI DODOMA

Imetumwa : June 25th, 2025

Na. Hellen M. Minja

       Habari – DODOMA RS

Uvamizi wa vyanzo vya maji kwa shughuli za kibinadamu unatajwa kuwa changamoto inayoendelea kuvikabili vyanzo vya Maji hususan kile cha Bonde la Makutupora (Kidakio cha Kinyasungwe).

Hayo yamebainishwa wakati wa kikao cha jukwaa la Wadau wa maji sekta Mtambuka Kidakio cha Kinyasungwe Jijini Dodoma.

Kikao hicho kilichoongozwa na Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma Bw. Kaspar K. Mmuya, kimefanyika kwenye ukumbi wa hoteli ya ‘Midland View Inn’ Kisasa Jijini hapa, kimelenga kujadili mambo kadhaa yanayokikabili Kidakio hicho ambacho ni chanzo muhimu cha maji kwa Jiji la Dodoma.

“Kuna uvamizi wa vyanzo vya maji vinavyotegemewa na Jiji la Dodoma kama vile maeneo tengefu ya hifadhi ya maji chini ya ardhi. Uvamizi huu upo maeneo mengi mno, kuna wengine wanakwenda kulima, kukata miti na shughuli nyingine. Hii changamoto ishughulikiwe, eneo lile litunzwe kwani faida yake tunayo sisi Wanadodoma”. Bw. Mmuya

Kadhalika, Mkurugenzi wa Bodi ya Maji Bonde la Wami Ruvu Mhandishi Elibariki Mmasy, amesema maendeleo ya Jiji la Dodoma yanategemea uwepo wa maji katika vyanzo vya Makutupora, Nzuguni na Chamwino hivyo kama Taasisi wana wajibu wa kuwakusanya Wadau na kujadili ni jinsi gani wanalinda vyanzo hivyo.

Jiji la Dodoma linaangukia ndani ya Hifadhi ya Maji ya Kinyasungwe (Makutupora) ambapo linanufaika na maji yanayopatikana katika eneo hilo kwa 100% hali inayochagiza ukuaji wa uchumi na Maendeleo ya Jiji hili hivyo ni muhimu kutunza chanzo hiki ili kuepusha migogoro ya mara kwa mara kwa mustakabali wa Taifa kwa ujumla.



#dodomafahariyawatanzania

#wekezadodomastawishadodoma

#keroyakowajibuwangu

#mtiwangubirthdayyangu

Matangazo

  • "WANANCHI JITOKEZENI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU 2025" - RC SENYAMULE February 17, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • SERIKALI IMEJIZATITI KULETA MAENDELEO KWA KUIMARISHA MAZINGIRA YA UWEKEZAJI NA BIASHARA

    June 25, 2025
  • TANZANIA SIYO SALAMA KWA WAUZAJI , WASAFIRISHA, WALIMAJI NA WATUMIAJI WA DAWA ZA KULEVYA” - MHE. MAJALIWA

    June 26, 2025
  • SHUGHULI ZA KIBINADAMU ZATAJWA KUWA TISHIO KWA CHANZO CHA MAJI BONDE LA MAKUTUPORA JIJINI DODOMA

    June 25, 2025
  • VODACOM TANZANIA KUPANDISHA HADHI MINARA YAO KUIMARISHA MAWASILIANO DODOMA

    June 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

RC SENYAMULE AKIZUNGUMZA KWENYE UZINDUZI WA SERA YA ELIMU NA MAFUNZO YA MWAKA 2014 TOLEO LA 2023.
Video Nyinginezo

Kurasa za Karibu

  • Speeches
  • mission and vision
  • Photo Gallery
  • Videos
  • Press Releases
  • Organization Structure
  • Reports
  • Client Service Charter
  • Acts

Tovuti Muhimu

  • PO-RALG
  • Public Service Management
  • Parliament of Tanzania
  • UDOM
  • Government Portal
  • Prime Minister's Office Website

World Visitors Tracker

world map hits counter

Rejesta ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Jengo la Mkapa (Mkapa House) Barabara ya Hospitali ya Mkoa

    Anuani ya Posta: 914 DODOMA

    Simu: +255 26 232 4343/232

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@dodoma.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya eneo

Hakimiliki©2016 GWF . Haki zote zimehifadhiwa.