• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Ofisi |
    • Malalamiko |
    • eoffice |
Dodoma Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Taasisi
      • Huduma Zetu
    • Huduma Zetu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Seksheni
      • Administration and Human Resource Management Section
      • Planning and Coordination
      • Infrastructure section
      • Management Monitoring and Inspection section;
      • Education and vocational Training section
      • Economic and productive sectors section;
      • Health, Social welfare and Nutrition services section
      • Industry, Trade and Investment section
    • Vitengo
      • Information Communication Technology (lcT) and Statistics
      • Government Communication Unit
      • Finance and Accounts unit;
      • Internal Audit unit
      • Legal services unit;
      • Procurement Management unit;
  • Wilaya
    • Bahi
    • Chamwino
    • Kongwa
    • Mpwapwa
    • Kondoa
    • Dodoma Mjini
    • Chemba
  • Mamlaka za Serikali za mitaa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bahi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chemba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa
    • Halmashauri ya Wilaya Mpwapwa
    • Halmashauri ya Mji Kondoa
    • The City Council of Dodoma (CCD)
  • Uwekezaji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Habari kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WAFUGAJI WAASWA KUFUGA KWA KUZINGATIA UWEZO WA MALISHO ILI KUPATA TIJA

Imetumwa : August 13th, 2025

Na. Hellen M. Minja

       Habari – DODOMA RS

Mwenyekiti wa Baraza la kumshauri Rais kuhusu masuala ya Chakula na Kilimo nchini Tanzania ambaye pia ni Waziri Mkuu Mstaafu Mhe. Mizengo Pinda, amewaasa wafugaji kufuga kwa kuzingatia uwezo wa malisho ili kupata tija ya ufugaji ikiwa ni pamoja na kupata maziwa na mazao mengine ya ufugaji.

Hayo yamebainishwa na Mwenyekiti huyo alipokua akifungua Mkutano wa Wadau wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi Kanda ya Kati uliofanyika Agosti 13, 2025 katika ukumbi wa Hoteli ya Morena Jijini Dodoma ambapo mbali na ufugaji wenye kuzingatia eneo la malisho, amesema Tanzania ina eneo la hekari Milioni 44 kwa ajili ya kilimo na kwenye eneo hilo ni 15% ndio inafaa kwa kilimo.

“Fuga kulingana na eneo la malisho ili uweze kupata Ng’ombe wenye sifa na wanaosimamiwa vizuri. Tuna hekta zenye kufaa kwa kilimo Milioni 44 katika eneo hilo lote, eneo la ardhi linalolimwa ni 15% na Sekta za kilimo, Uvuvi na Ufugaji zimechangia kutoa ajira kwa wananchi asilimia 65 mpaka 70”. Mhe. Pinda

Aidha, Katibu wa Baraza hilo Dr. Florence Turuka amesema katika Mikutano ya viongozi wa nchi za Afrika, Serikali ziliazimia kuwa Afrika itumie fursa zilizopo katika kilimo na ichangie kulisha watu Bilioni 9 watakao kuwepo hapa ulimwenguni ifikapo mwaka 2050 ambapo Waafrika watakua wamefikia takribani watu Bilioni 2.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule amempongeza Mhe. Rais kupitia Wizara ya kilimo kwa kuwekeza kwenye miundombinu ya kilimo na kuufanya Mkoa huu kuwa sehemu ya uzalishaji wa chakula nchini kwani ameanzisha miradi ya uchimbaji visima kwenye kila Wilaya ili kuwezesha kilimo cha umwagiliaji.

Akiwasilisha taarifa ya hali ya uchumi ya mwaka 2024, Katibu Tawala Msaidizi Seksheni za Uchumi na Uzalishaji Mkoa wa Dodoma Bi. Aziza Mumba amesema sekta za Mazao, Mifugo, Uvuvi na Misitu zinachangia takribani 39% ya Pato la Mkoa na kusababisha soko kuongezeka hivyo pia uzalishaji unatakiwa kuongezeka.

Baraza la kumshauri Rais kuhusu masuala ya Chakula na Kilimo lilianzishwa Machi 14, 2023 na Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa lengo la kuimarisha usalama wa chakula na kuongeza tija ya kilimo likiwa na jukumu la kushauri kuhusu mikakati ya kuongeza thamani ya mazao, kukuza ubunifu katika sekta ya kilimo na kurahisisha upatikanaji wa mitaji kwa wakulima na wawekezaji.


#dodomafahariyawatanzania

#wekezadodomastawishadodoma

#keroyakowajibuwangu

#mtiwangubirthdayyangu

Matangazo

  • No records found
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • ASASI ZA KIRAIA ZAPEWA MAFUNZO YA KUZUIA UTAKATISHAJI FEDHA HARAMU NA VITENDO VYA KIGAIDI

    August 14, 2025
  • WAFANYAKAZI WA TANESCO WATAKIWA KUWA MABALOZI WA MATUMIZI YA NISHATI YA UMEME KUPIKIA

    August 14, 2025
  • WAFUGAJI WAASWA KUFUGA KWA KUZINGATIA UWEZO WA MALISHO ILI KUPATA TIJA

    August 13, 2025
  • MASHIRIKA YASIYO YA KISERIKALI NI CHACHU YA MAENDELEO KWA WANANCHI

    August 14, 2025
  • Tazama Zote

Video

RC SENYAMULE AKIZUNGUMZA KWENYE UZINDUZI WA SERA YA ELIMU NA MAFUNZO YA MWAKA 2014 TOLEO LA 2023.
Video Nyinginezo

Kurasa za Karibu

  • Speeches
  • mission and vision
  • Photo Gallery
  • Videos
  • Press Releases
  • Organization Structure
  • Reports
  • Client Service Charter
  • Acts

Tovuti Muhimu

  • PO-RALG
  • Public Service Management
  • Parliament of Tanzania
  • UDOM
  • Government Portal
  • Prime Minister's Office Website

World Visitors Tracker

world map hits counter

Rejesta ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Jengo la Mkapa (Mkapa House) Barabara ya Hospitali ya Mkoa

    Anuani ya Posta: 914 DODOMA

    Simu: +255 26 232 4343/232

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@dodoma.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya eneo

Hakimiliki©2016 GWF . Haki zote zimehifadhiwa.