• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Ofisi |
    • Malalamiko |
Dodoma Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Taasisi
      • Huduma Zetu
    • Huduma Zetu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Seksheni
      • Administration and Human Resource Management Section
      • Planning and Coordination
      • Infrastructure section
      • Management Monitoring and Inspection section;
      • Education and vocational Training section
      • Economic and productive sectors section;
      • Health, Social welfare and Nutrition services section
      • Industry, Trade and Investment section
    • Vitengo
      • Information Communication Technology (lcT) and Statistics
      • Government Communication Unit
      • Finance and Accounts unit;
      • Internal Audit unit
      • Legal services unit;
      • Procurement Management unit;
  • Wilaya
    • Bahi
    • Chamwino
    • Kongwa
    • Mpwapwa
    • Kondoa
    • Dodoma Mjini
    • Chemba
  • Mamlaka za Serikali za mitaa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bahi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chemba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa
    • Halmashauri ya Wilaya Mpwapwa
    • Halmashauri ya Mji Kondoa
    • The City Council of Dodoma (CCD)
  • Uwekezaji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Habari kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

TANROADS YATENGA BILIONI 17.8 MIRADI YA BARABARA DODOMA

Imetumwa : December 19th, 2022

Wakala wa Barabara nchini Mkoa wa Dodoma imetenga kiasi cha Shilingi bilioni 17.8 kwa ajili ya ujenzi wa barabara zenye jumla ya urefu wa Kilometa 1,707.02 ambapo utekelezaji wake unafanywa chini ya ufadhili wa Benki ya Dunia.

Hayo yamebainishwa katika kikao cha pili cha mwaka cha Bodi ya barabara kilichojadili utelekezaji wa miradi ya barabara za Mkoa chini ya mwenyekiti wake Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule.

Akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa kazi kwa kipindi cha nusu mwaka Kaimu Meneja wa Wakala wa Barabara Mkoa Mhandisi Salome Kabunda amesema licha ya maendeleo mazuri ya utekelezaji wa miradi ya barabara katika Mkoa wa Dodoma bado kuna changamoto zinazoikabili Taasisi katika utekelezaji wake.

Amezitaja changamoto hizo kuwa ni pamoja na uvamizi wa wananchi kwa kujenga kwenye hifadhi za barabara, uswagaji wa mifugo barabarani, utupaji taka kwenye mifereji ya mvua na kusababisha mafuriko kutokana na kuziba kwa mifereji, ufinyu wa bajeti pamoja na uegeshaji holela wa magari unaopelekea uharibifu wa barabara.

Kwa upande wa Wakala wa ujenzi wa barabara Mijini na Vijijini TARURA, Meneja wa TARURA Mkoa wa Dodoma Mhandisi Lusako Kilembe amesema wamedhamiria kujenga barabara zenye urefu wa Km 7,504.94 pamoja na barabara zinazolisha barabara kuu zenye urefu wa Km 900.56.

“Jumla ya mikataba 67 ya utengenezaji wa barabara yenye thamani ya shilingi Bilioni 23.65 imeidhinishwa. Pia katika ujenzi wa Barabara hizi, matumizi ya teknolojia ya ECOROADS na POLYMER zimetumika ikiwa ni pamoja na matumizi ya mawe kwenye maeneo ambayo upatikanaji wake ni rahisi ili kupunguza matumizi ya saruji na nondo” Alisisitiza Mhandisi Kilembe.

Kikao hicho kimeazimia Wakala wa Barabara nchini kufuatilia utaratibu wa kuhamisha shule ya Unkunku iliyopo Kondoa Mji ili kupisha mradi wa barabara, kuidhinishwa ujenzi wa barabara ya Simanjiro – Kongwa, kujenga maegesho ya magari eneo la Chimulata Wilaya ya Kongwa na kutumia Sheria katika kudhibiti na kupambana na waharibifu wa miundombinu kwa kupitisha mifugo kwenye barabara.

Mwenyekiti wa kikao hicho, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule ameiagiza TANROADS kutoa elimu kwa wananchi ya matumizi sahihi ya barabara hususan kwenye maeneo korofi ambayo wananchi hufunga barabara wakihitaji matuta hata katika barabara ambazo hazina uhitaji huo zaidi ya alama za barabarani tu ili kuzuia ajali.

Aidha amewataka wakala wa barabara TANROADS kutenga bajeti ya kufungua barabara ya kutoka Dodoma mpaka Ruaha kwa ajili ya kuchochea na kuvutia utalii, kuweka taa za usalama barabarani katika maeneo yanayohitajika na kusisitiza usimamizi madhubuti wa miradi yote ili iweze kukamilika kwa ubora na wakati.

Kikao hiki kimehudhuriwa na wajumbe wa bodi ambao ni pamoja na Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma Bi. Fatuma Mganga, wakuu wa Wilaya zote saba za Mkoa wa Dodoma, Wenyeviti wa Halmashauri Nane za Mkoa, Wakurugenzi Watendaji wa Halmashauri, Wabunge, Viongozi wa Taasisi zinazohusika na ujenzi wa barabara (TANROADS na TARURA).

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE (CSEE) 2020 January 15, 2021
  • MATOKEO YA MTIHANI WA MAARIFA (QT) 2020 January 15, 2021
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021 SHULE ZA BWENI (WASICHANA NA WANAUME) . December 20, 2020
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA YA KIDATO CHA PILI (FTNA) 2020 January 15, 2021
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • KATIBU TAWALA SINGIDA AKABIDHI OFISI KWA KATIBU TAWALA DODOMA

    March 23, 2023
  • MACHINGA DODOMA WAMPONGEZA DKT. SAMIA SULUHU HASSAN

    March 23, 2023
  • KIWANDA CHA AINA YAKE KUJENGWA KONGWA

    March 17, 2023
  • WAFANYAKAZI WAASWA MSHIKAMANO MAHALA PA KAZI

    March 15, 2023
  • Tazama Zote

Video

Mkuu wa Mkoa akiongoza siku ya maombi jijini Dodoma
Video Nyinginezo

Kurasa za Karibu

  • Speeches
  • mission and vision
  • Photo Gallery
  • Videos
  • Press Releases
  • Organization Structure
  • Reports
  • Client Service Charter
  • Acts

Tovuti Muhimu

  • PO-RALG
  • Public Service Management
  • Parliament of Tanzania
  • UDOM
  • Government Portal
  • Prime Minister's Office Website

World Visitors Tracker

world map hits counter

Rejesta ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Jengo la Mkapa (Mkapa House) Barabara ya Hospitali ya Mkoa

    Anuani ya Posta: 914 DODOMA

    Simu: +255 26 232 4343/232

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@dodoma.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya eneo

Hakimiliki©2016 GWF . Haki zote zimehifadhiwa.