• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Ofisi |
    • Malalamiko |
Dodoma Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Taasisi
      • Huduma Zetu
    • Huduma Zetu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Seksheni
      • Administration and Human Resource Management Section
      • Planning and Coordination
      • Infrastructure section
      • Management Monitoring and Inspection section;
      • Education and vocational Training section
      • Economic and productive sectors section;
      • Health, Social welfare and Nutrition services section
      • Industry, Trade and Investment section
    • Vitengo
      • Information Communication Technology (lcT) and Statistics
      • Government Communication Unit
      • Finance and Accounts unit;
      • Internal Audit unit
      • Legal services unit;
      • Procurement Management unit;
  • Wilaya
    • Bahi
    • Chamwino
    • Kongwa
    • Mpwapwa
    • Kondoa
    • Dodoma Mjini
    • Chemba
  • Mamlaka za Serikali za mitaa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bahi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chemba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa
    • Halmashauri ya Wilaya Mpwapwa
    • Halmashauri ya Mji Kondoa
    • The City Council of Dodoma (CCD)
  • Uwekezaji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Habari kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

UKILETWA DODOMA UMELETWA KUJENGA MAKAO MAKUU YA NCHI

Imetumwa : January 30th, 2023


Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule amemuapisha Mkuu wa Wilaya ya Chemba Mhe. Gerald R. Mongella pamoja na kuwapokea Wakuu wa Wilaya wapya wawili waliohamishiwa Mkoa wa Dodoma kwenye hafla iliyofanyika kwenye ukumbi wa jengo la Mkapa zilipo Ofisi za Mkuu wa Mkoa.

Mhe. Senyamule amewaasa Wakuu hao wa Wilaya kuheshimu nafasi waliyopewa na Mhe. Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwani wameaminika kuitumikia nafasi hiyo. “Nafasi ya Ukuu wa Wilaya ina madaraka na dhamana kubwa sana, ukiyatumia kwa tija yanaleta manufaa ila ukiyatumia vibaya utakwenda kupata matokeo mabaya”

Aidha Mhe. Senyamule amesema kuwa Dodoma ni Makao Makuu ya nchi na nafasi waliyopewa wakuu hao  ni kuja kuijenga Makao Makuu.

“Kuja Dodoma ni bahati kwakuwa mnakuwa sehemu ya kujenga Makao Makuu ya nchi. Yeyote aliyekuja hapa, ajue amepata nafasi ya kujenga Makao Makuu kwani viongozi wetu wakuu wana matarajio makubwa na sisi. Mkoa umejipanga kuifanya Makao Makuu kama yalivyo matarajio ya viongozi wetu” Mhe. Senyamule

Vilevile Mhe. Senyamule amegusia changamoto zinazoukabili Mkoa wa Dodoma kwenye sekta ya elimu ikiwemo utoro, ufaulu hafifu, ukosefu wa chakula shuleni na upungufu wa miundombinu ya elimu na kuwaagiza Wakuu hao wapya kwenda kusimamia kikamilifu utatuzi wa changamoto hizo kwa kushirikiana na watendaji na wenyeviti wa Vijiji na Kata.

“Halmashauri zetu zina changamoto kubwa kwa upande wa elimu ambazo tunajitahidi kukabiliana nazo kwa mwaka huu. Kwenye upungufu wa miundombinu, nimetoa maagizo kwa wenyeviti wa Kata na Vijiji kukaa vikao na kukubaliana kujenga maboma mawili kwa kila Kijiji kwa mwaka, nendeni mkasimamie agizo hili” Amesisitiza Mhe. Senyamule

Naye Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Fatuma Mganga, amepata fursa ya kutoa neno kwa Wakuu hao wapya wa Wilaya wakati wa hafla hiyo;

“Bahi imejipambanua vizuri kwa elimu, miradi na mambo mengine mengi hivyo tunaamini Mkuu wa Wilaya Mpya atakwenda kuendeleza hayo. Wilaya ya Mpwapwa bado ipo nyuma kwenye uandikishwaji wa wanafunzi wanaoingia kidato cha kwanza mwaka huu hivyo tunategemea utakwenda kuhimiza zaidi. Tunategemea Wilaya iwe na vitendo Zaidi kuliko nadharia” Dkt. Mganga

Katika salamu zao za shukrani, wakuu wa Wilaya ya Chemba na Mpwapwa wameahidi kufanya kazi kwa weledi na uaminifu kama viapo walivyoapa vinavyowataka huku wakitekeleza ilani ya Chama Tawala pia wamesema kuwa dhamana waliyopewa ni deni kwa Mhe. Rais aliyewaamini kwa kuwapa na fasi hizo na wanapaswa kulilipa. Wameahidi kuviishi viapo vyao na kwenda kutekeleza maagizo yote ya Mkuu wa Mkoa huku wakiwa tayari kutumika wakati wowote.

Uapisho huo umekwenda sambamba na kumuaga aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Bahi Mhe. Mwanahamisi Munkunda aliyehamishiwa  katika Wilaya ya Temeke Mkoani Dar es Salaam. Wengine waliokaribishwa ni Mkuu wa Wilaya ya Bahi Mhe. Godwin Gondwe pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa Mhe. Sophia Kizigo.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE (CSEE) 2020 January 15, 2021
  • MATOKEO YA MTIHANI WA MAARIFA (QT) 2020 January 15, 2021
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021 SHULE ZA BWENI (WASICHANA NA WANAUME) . December 20, 2020
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA YA KIDATO CHA PILI (FTNA) 2020 January 15, 2021
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • KATIBU TAWALA SINGIDA AKABIDHI OFISI KWA KATIBU TAWALA DODOMA

    March 23, 2023
  • MACHINGA DODOMA WAMPONGEZA DKT. SAMIA SULUHU HASSAN

    March 23, 2023
  • KIWANDA CHA AINA YAKE KUJENGWA KONGWA

    March 17, 2023
  • WAFANYAKAZI WAASWA MSHIKAMANO MAHALA PA KAZI

    March 15, 2023
  • Tazama Zote

Video

Mkuu wa Mkoa akiongoza siku ya maombi jijini Dodoma
Video Nyinginezo

Kurasa za Karibu

  • Speeches
  • mission and vision
  • Photo Gallery
  • Videos
  • Press Releases
  • Organization Structure
  • Reports
  • Client Service Charter
  • Acts

Tovuti Muhimu

  • PO-RALG
  • Public Service Management
  • Parliament of Tanzania
  • UDOM
  • Government Portal
  • Prime Minister's Office Website

World Visitors Tracker

world map hits counter

Rejesta ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Jengo la Mkapa (Mkapa House) Barabara ya Hospitali ya Mkoa

    Anuani ya Posta: 914 DODOMA

    Simu: +255 26 232 4343/232

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@dodoma.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya eneo

Hakimiliki©2016 GWF . Haki zote zimehifadhiwa.