• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Ofisi |
    • Malalamiko |
    • eoffice |
Dodoma Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Taasisi
      • Huduma Zetu
    • Huduma Zetu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Seksheni
      • Administration and Human Resource Management Section
      • Planning and Coordination
      • Infrastructure section
      • Management Monitoring and Inspection section;
      • Education and vocational Training section
      • Economic and productive sectors section;
      • Health, Social welfare and Nutrition services section
      • Industry, Trade and Investment section
    • Vitengo
      • Information Communication Technology (lcT) and Statistics
      • Government Communication Unit
      • Finance and Accounts unit;
      • Internal Audit unit
      • Legal services unit;
      • Procurement Management unit;
  • Wilaya
    • Bahi
    • Chamwino
    • Kongwa
    • Mpwapwa
    • Kondoa
    • Dodoma Mjini
    • Chemba
  • Mamlaka za Serikali za mitaa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bahi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chemba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa
    • Halmashauri ya Wilaya Mpwapwa
    • Halmashauri ya Mji Kondoa
    • The City Council of Dodoma (CCD)
  • Uwekezaji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Habari kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MADAKTARI BINGWA WA DKT. SAMIA KUTOA HUDUMA ZA KIBINGWA HOSPITALI ZA WILAYA DODOMA

Imetumwa : June 2nd, 2025

Na. Hellen M. Minja

       Habari – DODOMA RS

Wananchi wa Mkoa wa Dodoma wenye changamoto mbalimbali za kiafya hasa zile za kuhitaji Madaktari Bingwa, wametakiwa kufika kwenye Hospitali zao za Wilaya kuanzia leo June 02, 2025, kwa ajili ya kupata huduma, kwani Wataalamu wa Kibingwa wamefika Mkoani hapa na watakua kwenye Hospitali hizo kwa ajili ya Huduma za Kibingwa.

Hayo yameelezwa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule alipokua akiwapokea ‘Madaktari Bingwa wa Samia’ ambao wamefika ofisini kwake leo tayari kwa ajili ya kutoa huduma kwenye Mkoa wake kwa muda wa siku 06 ( hadi Jumamosi June 07, 2025).

“Madaktari Bingwa watakua katika Hospitali zetu za Wilaya ambapo watawapa huduma kwa ukaribu na kwa unafuu. Kama una ugonjwa wa meno ambao unasema huu ni gharama kwenda hospitali, kama una ugonjwa wa Koo, masikio, Moyo, magonjwa ya kina mama, nenda Hospitali utapewa huduma badala ya kuchelewa fursa hii ambayo itakuwepo tarehe 02 leo mpaka 06”.

Kadhalika, Mganga Mkuu wa Mkoa Dkt. Thomas Rutachunzibwa amesema kwa Mkoa wa Dodoma hii ni awamu ya tatu ambapo awamu mbili zilizofanyika  mwaka jana zilikwenda vizuri na sasa timu hii itakwenda kutoa huduma kwenye Halmashauri 7 za Mkoa huu ambazo ni Bahi, Chamwino, Chemba, Kondoa DC, Kondoa TC, Kongwa na Mpwapwa.

Naye, Mwakilishi kutoka Wizara ya Afya Dr. Mathew Mushi, amesema wamepokea Madaktari Bingwa 50 wa kada mbalimbali ambazo ni Magonjwa ya kina mama, watoto na watoto wachanga, Magonjwa ya ndani, Kinywa na Meno, Mabingwa wa usingizi na ganzi salama, pua, koo na masikio pamoja na Wauguzi Bobezi. Kila Halmashauri itapokea Madaktari 7 ila Mpwapwa itapokea madaktari 8

Hata hivyo, Kiongozi wa Timu hiyo ambaye ni Dkt. Bingwa wa Magonjwa ya ndani Dr. Patrick Bilikundi, amesema Serikali imewekeza katika vifaa tiba ikiwemo dawa na Wataalamu wanashirikishwa kufika sehemu ambazo wananchi wanapata ugumu kutembelea Hospitali kubwa kupata huduma za kibingwa na kibingwa bobezi hivyo wanategemea mwitikio mkubwa kutoka kwa Wananchi wa Mkoa huu.



#dodomafahariyawatanzania

#wekezadodomastawishadodoma

#keroyakowajibuwangu

#mtiwangubirthdayyangu

Matangazo

  • "WANANCHI JITOKEZENI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU 2025" - RC SENYAMULE February 17, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RAS MMUYA AWAAHIDI ZAWADI NONO WANAMICHEZO - UMITASHUMTA

    June 17, 2025
  • WAMILIKI WA MAABARA BINAFSI WATAKIWA KUTOA MAJIBU SAHIHI YA VIPIMO KWA WAGONJWA

    June 17, 2025
  • TAASISI ZA UMMA ZATAKIWA KUJIUNGA NA MFUMO KURAHISISHA HUDUMA KWA WANANCHI

    June 17, 2025
  • DODOMA MOTO MKALI MASHINDANO UMITASHUMTA

    June 14, 2025
  • Tazama Zote

Video

RC SENYAMULE AKIZUNGUMZA KWENYE UZINDUZI WA SERA YA ELIMU NA MAFUNZO YA MWAKA 2014 TOLEO LA 2023.
Video Nyinginezo

Kurasa za Karibu

  • Speeches
  • mission and vision
  • Photo Gallery
  • Videos
  • Press Releases
  • Organization Structure
  • Reports
  • Client Service Charter
  • Acts

Tovuti Muhimu

  • PO-RALG
  • Public Service Management
  • Parliament of Tanzania
  • UDOM
  • Government Portal
  • Prime Minister's Office Website

World Visitors Tracker

world map hits counter

Rejesta ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Jengo la Mkapa (Mkapa House) Barabara ya Hospitali ya Mkoa

    Anuani ya Posta: 914 DODOMA

    Simu: +255 26 232 4343/232

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@dodoma.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya eneo

Hakimiliki©2016 GWF . Haki zote zimehifadhiwa.